Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 21

فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ

Lakini aliikadhibisha na akaasi



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 22

ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ

Kisha akageuka nyuma na kufanya juhudi, (ya kukanusha)



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 23

فَحَشَرَ فَنَادَىٰ

Akakusanya watu akatangaza



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 24

فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mkuu kabisa



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 25

فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ

Basi hapo Allah akamshika na kumuadhibu kwa adhabu ya mwisho na mwanzo.[1]


1- - Allah akampa adhabu kwa kauli yake ya mwisho, nayo ni vile kusema: “Mimi ndiye Mola wenu Mlezi aliye mkubwa kabisa. Na akampa adhabu kwa kauli yake ya mwanzo, nayo ni kumkadhibisha Musa”.


Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 26

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ

Hakika katika hayo bila shaka kuna funzo kwa yule anayeogopa



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 27

ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا

Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 28

رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا

Akainua kimo chake, na akaiten-geneza vizuri



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 29

وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا

Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 30

وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ

Na ardhi baada ya hayo Akai-tandaza



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 31

أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا

Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 32

وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا

Na milima akaisimamisha,



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 33

مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ

Ni manufaa kwenu na kwa wanyama wenu wa mifugo



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 34

فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Basi itakapokuja hilo balaa kubwa kabisa



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 35

يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ

Siku ambayo mtu atakumbuka aliyoyafanya, (aliyoyakimbilia kuyafanyia juhudi)



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 36

وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ

Na moto utakapodhihirishwa wazi kwa mwenye kuona



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 37

فَأَمَّا مَن طَغَىٰ

Basi yule aliyepindukia mipaka na kuasi



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 38

وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Na akapenda zaidi maisha ya dunia



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 39

فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 40

وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ

Ama yule anayeogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake, na akaikataza nafsi yake na na matamanio



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 41

فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 42

يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا

Wanakuuliza kuhusu Kiyama lini kufika kwake?



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 43

فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ

Una nini wewe hata ukitaje hicho kiyama?



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 44

إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ

Kwa Mola wako ndio mwisho wake



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 45

إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا

Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kukiogopa hicho kiyama



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 46

كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا

Siku watakapokiona, watakuwa kana kwamba hawakubaki (duniani) isipokuwa jioni moja au mchana wake



Surah: A’BASA

Ayah : 1

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ

Alikunja paji lake la uso na akageuka



Surah: A’BASA

Ayah : 2

أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ

Kwasababu alimjia kipofu



Surah: A’BASA

Ayah : 3

وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ

Na nini kitakachokujulisha; huwenda akatakasika?



Surah: A’BASA

Ayah : 4

أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ

Au akawaidhika na yakamnufaisha mawaidha?