Surah: YUNUS 

Ayah : 24

إِنَّمَا مَثَلُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا كَمَآءٍ أَنزَلۡنَٰهُ مِنَ ٱلسَّمَآءِ فَٱخۡتَلَطَ بِهِۦ نَبَاتُ ٱلۡأَرۡضِ مِمَّا يَأۡكُلُ ٱلنَّاسُ وَٱلۡأَنۡعَٰمُ حَتَّىٰٓ إِذَآ أَخَذَتِ ٱلۡأَرۡضُ زُخۡرُفَهَا وَٱزَّيَّنَتۡ وَظَنَّ أَهۡلُهَآ أَنَّهُمۡ قَٰدِرُونَ عَلَيۡهَآ أَتَىٰهَآ أَمۡرُنَا لَيۡلًا أَوۡ نَهَارٗا فَجَعَلۡنَٰهَا حَصِيدٗا كَأَن لَّمۡ تَغۡنَ بِٱلۡأَمۡسِۚ كَذَٰلِكَ نُفَصِّلُ ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَتَفَكَّرُونَ

Hakika ilivyo ni kwamba, mfano wa maisha ya duniani ni kama maji (mvua) tuliyo yateremsha kutoka mawinguni yakachanganyika na mimea ya ardhini, ikiwa ni pamoja na mimea inayoliwa na watu na mifugo mpaka ardhi ilipokamilisha urembo wake na ikapendeza (kwa kustawi vizuri) na watu wake (wamiliki wake) wakadhani kwamba wameyaweza (mazao hayo kufanikiwa kuyafikisha hatua ya kuvuna), likawajia jambo letu usiku au mchana basi tukaifanya imevunwa (na kufyekwa) kana kwamba haikuwepo jana. Hivi ndivyo tunavyo zifafanua Aya (zetu) kwa watu wanaofikiri



Surah: YUNUS 

Ayah : 25

وَٱللَّهُ يَدۡعُوٓاْ إِلَىٰ دَارِ ٱلسَّلَٰمِ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ

Na Allah anaita (watu) kwenye nyumba ya amani na anamuongoza amtakaye kwenye njia iliyonyooka



Surah: YUNUS 

Ayah : 26

۞لِّلَّذِينَ أَحۡسَنُواْ ٱلۡحُسۡنَىٰ وَزِيَادَةٞۖ وَلَا يَرۡهَقُ وُجُوهَهُمۡ قَتَرٞ وَلَا ذِلَّةٌۚ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَنَّةِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Wale waliofanya mazuri (hapa duniani), watapata mazuri (Akhera) na ziada[1] na wala nyuso zao hazitafunikwa na vumbi na madhila. Hao ndio watu wa Peponi; humo watakaa milele


1- - Swahaba wengi, Allah awawie radhi, wametafsiri “mazuri” kwamba ni Pepo na “ziada” kwamba ni kumuona Allah Mtukufu.


Surah: YUNUS 

Ayah : 27

وَٱلَّذِينَ كَسَبُواْ ٱلسَّيِّـَٔاتِ جَزَآءُ سَيِّئَةِۭ بِمِثۡلِهَا وَتَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۖ مَّا لَهُم مِّنَ ٱللَّهِ مِنۡ عَاصِمٖۖ كَأَنَّمَآ أُغۡشِيَتۡ وُجُوهُهُمۡ قِطَعٗا مِّنَ ٱلَّيۡلِ مُظۡلِمًاۚ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Na wale waliochuma maovu, malipo ya maovu ni uovu kama huo, na yatawafika madhila, hawatakuwa na yeyote wa kuwakinga (dhidi ya) Allah (asiwaadhibu). (Hali yao itakuwa), kana kwamba nyuso zao zimefunikizwa na kipande cha usiku wa giza nene. Hao ndio watu wa motoni, watakaahumo milele



Surah: YUNUS 

Ayah : 28

وَيَوۡمَ نَحۡشُرُهُمۡ جَمِيعٗا ثُمَّ نَقُولُ لِلَّذِينَ أَشۡرَكُواْ مَكَانَكُمۡ أَنتُمۡ وَشُرَكَآؤُكُمۡۚ فَزَيَّلۡنَا بَيۡنَهُمۡۖ وَقَالَ شُرَكَآؤُهُم مَّا كُنتُمۡ إِيَّانَا تَعۡبُدُونَ

Na (kumbuka) siku tutakayo-wakusanya wote, kisha tutawaambia wale washirikina (makafiri kuwa): Simameni hapo hapo mlipo nyinyi na washirika (Miungu) wenu (mliowashirikisha na Allah), hivyo tutatenganisha baina yao. Na washirika wao watasema: Nyinyi hamkuwa mnatuabudu



Surah: YUNUS 

Ayah : 29

فَكَفَىٰ بِٱللَّهِ شَهِيدَۢا بَيۡنَنَا وَبَيۡنَكُمۡ إِن كُنَّا عَنۡ عِبَادَتِكُمۡ لَغَٰفِلِينَ

Basi Allah anatosha kuwa shahidi baina yetu na baina yenu. Hakika sisi tulikuwa hatujui chochote kuhusu ibada yenu



Surah: YUNUS 

Ayah : 30

هُنَالِكَ تَبۡلُواْ كُلُّ نَفۡسٖ مَّآ أَسۡلَفَتۡۚ وَرُدُّوٓاْ إِلَى ٱللَّهِ مَوۡلَىٰهُمُ ٱلۡحَقِّۖ وَضَلَّ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ

Huko, kila mtu atayatafuta matendo yake aliyoyatanguliza (kuyafanya; yawe ya kheri au ya shari), na watarudishwa kwa (Allah) Mola wao wa haki, na yatawapotea yale waliyokuwa wakiyazusha



Surah: YUNUS 

Ayah : 31

قُلۡ مَن يَرۡزُقُكُم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِ أَمَّن يَمۡلِكُ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡأَبۡصَٰرَ وَمَن يُخۡرِجُ ٱلۡحَيَّ مِنَ ٱلۡمَيِّتِ وَيُخۡرِجُ ٱلۡمَيِّتَ مِنَ ٱلۡحَيِّ وَمَن يُدَبِّرُ ٱلۡأَمۡرَۚ فَسَيَقُولُونَ ٱللَّهُۚ فَقُلۡ أَفَلَا تَتَّقُونَ

Sema: Ni nani anayekuruzukuni kutoka mbinguni na ardhini? Au ni nani anayemiliki masikio na macho? Na ni nani atoae kilicho hai kutoka katika kilichokufa na atoae kilichokufa kutoka katika kilicho hai? Na ni nani anaye endesha mambo yote? Bila shaka watasema: Ni Allah. Basi sema: Hivi ni kwa nini hamuwi wachaMungu?



Surah: YUNUS 

Ayah : 32

فَذَٰلِكُمُ ٱللَّهُ رَبُّكُمُ ٱلۡحَقُّۖ فَمَاذَا بَعۡدَ ٱلۡحَقِّ إِلَّا ٱلضَّلَٰلُۖ فَأَنَّىٰ تُصۡرَفُونَ

Basi huyo ndiye Allah Mola wenu Mlezi. Basi ni nini baada ya haki sio upotevu tu? Basi ni vipi mnageuzwa (mnapotoshwa)?



Surah: YUNUS 

Ayah : 33

كَذَٰلِكَ حَقَّتۡ كَلِمَتُ رَبِّكَ عَلَى ٱلَّذِينَ فَسَقُوٓاْ أَنَّهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Kama hivyo (ilivyothibiti kwamba Mola wenu ni wa haki ndio hivyo hivyo), imethibiti kauli ya Mola wako Mlezi kwa wale waliofanya uovu kwamba, wao hawaamini



Surah: YUNUS 

Ayah : 34

قُلۡ هَلۡ مِن شُرَكَآئِكُم مَّن يَبۡدَؤُاْ ٱلۡخَلۡقَ ثُمَّ يُعِيدُهُۥۚ قُلِ ٱللَّهُ يَبۡدَؤُاْ ٱلۡخَلۡقَ ثُمَّ يُعِيدُهُۥۖ فَأَنَّىٰ تُؤۡفَكُونَ

Sema: Hivi, katika washirika (Miungu) wenu mnaowashirikisha na (Allah) yupo yeyote anayeanzisha kuumba (viumbe) kisha akarudia kuumba? Sema: Allah pekee ndiye anayeanzisha kuumba kisha (Siku ya Kiyama) atavirudisha alivyoviumba (kama vilivyokuwa mwanzo). Kwanini mnapotoshwa kuhusu kumpwekesha Allah!?



Surah: YUNUS 

Ayah : 35

قُلۡ هَلۡ مِن شُرَكَآئِكُم مَّن يَهۡدِيٓ إِلَى ٱلۡحَقِّۚ قُلِ ٱللَّهُ يَهۡدِي لِلۡحَقِّۗ أَفَمَن يَهۡدِيٓ إِلَى ٱلۡحَقِّ أَحَقُّ أَن يُتَّبَعَ أَمَّن لَّا يَهِدِّيٓ إِلَّآ أَن يُهۡدَىٰۖ فَمَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ

Sema: Hivi katika washirika (Miungu) wenu (mnaowashirikisha na Allah), yupo anayeongoza kwenye haki? Sema: Allah pekee ndiye anayeongoza kwenye haki. Basi, hivi anayeongoza kwenye haki ana haki zaidi ya kufuatwa au (mwenye haki zaidi ya kufuatwa ni) yule asiyeweza kuongoza chochote isipokuwa aongozwe? Basi mnanini nyinyi? Mnahukumuje?



Surah: YUNUS 

Ayah : 36

وَمَا يَتَّبِعُ أَكۡثَرُهُمۡ إِلَّا ظَنًّاۚ إِنَّ ٱلظَّنَّ لَا يُغۡنِي مِنَ ٱلۡحَقِّ شَيۡـًٔاۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمُۢ بِمَا يَفۡعَلُونَ

Na wengi wao hawafuati isipokuwa dhana tu. Hakika, dhana haifaidishi chochote kwenye haki. Hakika, Allah ni Mjuzi wa wanayoyatenda



Surah: YUNUS 

Ayah : 37

وَمَا كَانَ هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانُ أَن يُفۡتَرَىٰ مِن دُونِ ٱللَّهِ وَلَٰكِن تَصۡدِيقَ ٱلَّذِي بَيۡنَ يَدَيۡهِ وَتَفۡصِيلَ ٱلۡكِتَٰبِ لَا رَيۡبَ فِيهِ مِن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na haiwezekani Qur’ani hii kutungwa na yeyote kinyume na Allah, lakini (Qur’ani) ni usadikisho wa yote yaliyotangulia (katika vitabu na sheria za Manabii waliotangulia), na ni ufafanuzi wa kitabu (sheria za umma wa Muhammad) kisichokuwa na shaka kutoka kwa Mola mlezi wa walimwengu wote



Surah: YUNUS 

Ayah : 38

أَمۡ يَقُولُونَ ٱفۡتَرَىٰهُۖ قُلۡ فَأۡتُواْ بِسُورَةٖ مِّثۡلِهِۦ وَٱدۡعُواْ مَنِ ٱسۡتَطَعۡتُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Au wanasema (kuwa Muhammad) ameitunga (hiyo Qur’ani)? Sema: Basi leteni sura moja tu mfano wake na waiteni muwawezao kuwaleta kinyume na Allah (wakusaidieni), kama nyinyi ni wa kweli (katika madai yenu)



Surah: YUNUS 

Ayah : 39

بَلۡ كَذَّبُواْ بِمَا لَمۡ يُحِيطُواْ بِعِلۡمِهِۦ وَلَمَّا يَأۡتِهِمۡ تَأۡوِيلُهُۥۚ كَذَٰلِكَ كَذَّبَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۖ فَٱنظُرۡ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Bali wamekadhibisha mambo wasiyoyajua undani wake, na haijawafikia tafsiri yake. Kama hivyo walikadhibisha waliokuwepo kabla yao. Basi angalia, ilikuwaje hatima ya madhalimu?



Surah: YUNUS 

Ayah : 40

وَمِنۡهُم مَّن يُؤۡمِنُ بِهِۦ وَمِنۡهُم مَّن لَّا يُؤۡمِنُ بِهِۦۚ وَرَبُّكَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُفۡسِدِينَ

Na miongoni mwao wapo wanaoiamini (Qur’ani) na miongoni mwao wapo wasioiamini. Na Mola wako Mlezi anawajua sana waharibifu



Surah: YUNUS 

Ayah : 41

وَإِن كَذَّبُوكَ فَقُل لِّي عَمَلِي وَلَكُمۡ عَمَلُكُمۡۖ أَنتُم بَرِيٓـُٔونَ مِمَّآ أَعۡمَلُ وَأَنَا۠ بَرِيٓءٞ مِّمَّا تَعۡمَلُونَ

Na kama wakikukadhibisha, basi sema: Mimi nina amali zangu na nyinyi mna amali zenu. Nyinyi si wenye kuhusika na ninayoyafanya na mimi si mwenye kuhusika na mnayoyafanya



Surah: YUNUS 

Ayah : 42

وَمِنۡهُم مَّن يَسۡتَمِعُونَ إِلَيۡكَۚ أَفَأَنتَ تُسۡمِعُ ٱلصُّمَّ وَلَوۡ كَانُواْ لَا يَعۡقِلُونَ

Na miongoni mwao wapo wanaokusikiliza. Hivi wewe utawasikilizisha viziwi na hata kama hawafahamu?[1]


1- - Aya hii inabainisha kuwa wapo baadhi ya makafiri wanaosikiliza Qur’ani kwa makini inaposomwa lakini hawaongoki na hawaifuati. Hivyo kusikiliza kwao Qur’ani bila ya kuifuta ni sawa na viziwi ambao hawasikii kabisa.


Surah: YUNUS 

Ayah : 43

وَمِنۡهُم مَّن يَنظُرُ إِلَيۡكَۚ أَفَأَنتَ تَهۡدِي ٱلۡعُمۡيَ وَلَوۡ كَانُواْ لَا يُبۡصِرُونَ

Na miongoni mwao wapo wanaokutazama (na kuona dalili za Utume wako na nuru ya imani). Hivi wewe utawaongoza vipofu na ingawa hawaoni?



Surah: YUNUS 

Ayah : 44

إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَظۡلِمُ ٱلنَّاسَ شَيۡـٔٗا وَلَٰكِنَّ ٱلنَّاسَ أَنفُسَهُمۡ يَظۡلِمُونَ

Hakika, Allah hawadhulumu watu chochote na lakini watu wanazidhulumu nafsi zao



Surah: YUNUS 

Ayah : 45

وَيَوۡمَ يَحۡشُرُهُمۡ كَأَن لَّمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا سَاعَةٗ مِّنَ ٱلنَّهَارِ يَتَعَارَفُونَ بَيۡنَهُمۡۚ قَدۡ خَسِرَ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِلِقَآءِ ٱللَّهِ وَمَا كَانُواْ مُهۡتَدِينَ

Na (kumbuka) siku (Allah) atakapowakusanya (wataona) kana kwamba hawakukaa (duniani) isipokuwa saa moja tu ya mchana (muda mdogo tu wa mchana), wakitambulishana wao kwa wao. Hakika, wamekwisha pata hasara wale walioukadhibisha (waliokanusha) kukutana na Allah, na hawakuwa wenye kuongoka



Surah: YUNUS 

Ayah : 46

وَإِمَّا نُرِيَنَّكَ بَعۡضَ ٱلَّذِي نَعِدُهُمۡ أَوۡ نَتَوَفَّيَنَّكَ فَإِلَيۡنَا مَرۡجِعُهُمۡ ثُمَّ ٱللَّهُ شَهِيدٌ عَلَىٰ مَا يَفۡعَلُونَ

Na ikiwa kwa hakika tutakuonesha baadhi ya yale tunayowaahidi au tutakufisha, basi kwetu tu ndio marejeo yao, kisha Allah ni shahidi wa yale wanayoyafanya



Surah: YUNUS 

Ayah : 47

وَلِكُلِّ أُمَّةٖ رَّسُولٞۖ فَإِذَا جَآءَ رَسُولُهُمۡ قُضِيَ بَيۡنَهُم بِٱلۡقِسۡطِ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na kila umma una Mtume (wake). Basi anapofika Mtume wao watahukumiwa baina yao kwa uadilifu nao hawatadhulumiwa



Surah: YUNUS 

Ayah : 48

وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَٰذَا ٱلۡوَعۡدُ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Na (makafiri) wanasema: Ni lini (itatokea) hii ahadi kama nyinyi ni wakweli?



Surah: YUNUS 

Ayah : 49

قُل لَّآ أَمۡلِكُ لِنَفۡسِي ضَرّٗا وَلَا نَفۡعًا إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۗ لِكُلِّ أُمَّةٍ أَجَلٌۚ إِذَا جَآءَ أَجَلُهُمۡ فَلَا يَسۡتَـٔۡخِرُونَ سَاعَةٗ وَلَا يَسۡتَقۡدِمُونَ

Sema: Siimilikii nafsi yangu madhara wala manufaa, isipokuwa tu yale ayatakayo Allah. Kila umma una muda (wake wa kuishi). Pindi ukifika muda wao, basi hawatachelewesha saa moja wala kutanguliza



Surah: YUNUS 

Ayah : 50

قُلۡ أَرَءَيۡتُمۡ إِنۡ أَتَىٰكُمۡ عَذَابُهُۥ بَيَٰتًا أَوۡ نَهَارٗا مَّاذَا يَسۡتَعۡجِلُ مِنۡهُ ٱلۡمُجۡرِمُونَ

Sema: Mnaonaje kama itakufikieni adhabu yake usiku au mchana, hivi ni kitu gani wanachokiharakia waovu?



Surah: YUNUS 

Ayah : 51

أَثُمَّ إِذَا مَا وَقَعَ ءَامَنتُم بِهِۦٓۚ ءَآلۡـَٰٔنَ وَقَدۡ كُنتُم بِهِۦ تَسۡتَعۡجِلُونَ

Hivi hapo ikishatokea ndio mnaiamini? Je, hivi sasa (ndio mnaamini) na ilhali mlikuwa mkiitaka kwa haraka?



Surah: YUNUS 

Ayah : 52

ثُمَّ قِيلَ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ ذُوقُواْ عَذَابَ ٱلۡخُلۡدِ هَلۡ تُجۡزَوۡنَ إِلَّا بِمَا كُنتُمۡ تَكۡسِبُونَ

Kisha waliodhulumu wataambiwa: “Onjeni adhabu ya milele. Hamtalipwa isipokuwa tu yale mliyokuwa mkiyachuma



Surah: YUNUS 

Ayah : 53

۞وَيَسۡتَنۢبِـُٔونَكَ أَحَقٌّ هُوَۖ قُلۡ إِي وَرَبِّيٓ إِنَّهُۥ لَحَقّٞۖ وَمَآ أَنتُم بِمُعۡجِزِينَ

Na wanataka uwaeleze: Je, ni kweli hayo (unayowaambia)? Sema: Ndio! Ninaapa kwa Mola wangu Mlezi kwamba, kwa hakika kabisa, hayo ni kweli, na ninyi si wenye kushinda!