وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
Share :
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ
Naye hakika bila ya shaka anapenda sana (kheri) mali!
۞أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ
Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ
Na yakakusanywa yaliyomo vifuani?
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ
Kwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!
ٱلۡقَارِعَةُ
Inayo gonga!
مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Nini Inayo gonga?
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Na nini kitakacho kujuilisha nini Inayo gonga?
يَوۡمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلۡفَرَاشِ ٱلۡمَبۡثُوثِ
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo (vipepeo) walio tawanyika;
وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ ٱلۡمَنفُوشِ
Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza
وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ
Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
نَارٌ حَامِيَةُۢ
Ni Moto mkali!
أَلۡهَىٰكُمُ ٱلتَّكَاثُرُ
Kumekushughulisheni kutafuta wingi
حَتَّىٰ زُرۡتُمُ ٱلۡمَقَابِرَ
Mpaka mje makaburini!
كَلَّا سَوۡفَ تَعۡلَمُونَ
Sivyo hivyo! Mtakuja kujua!
ثُمَّ كَلَّا سَوۡفَ تَعۡلَمُونَ
Tena sivyo hivyo! Mtakuja kujua!
كَلَّا لَوۡ تَعۡلَمُونَ عِلۡمَ ٱلۡيَقِينِ
Sivyo hivyo! Lau mngelijua kujua kwa yakini,
لَتَرَوُنَّ ٱلۡجَحِيمَ
Basi bila ya shaka yoyote mtaiona Jahanamu!
ثُمَّ لَتَرَوُنَّهَا عَيۡنَ ٱلۡيَقِينِ
Tena, bila ya shaka yoyote, mtaiona kwa jicho la yakini
ثُمَّ لَتُسۡـَٔلُنَّ يَوۡمَئِذٍ عَنِ ٱلنَّعِيمِ
Tena bila ya shaka yoyote mtaulizwa siku hiyo juu ya neema
وَٱلۡعَصۡرِ
Naapa kwa Zama!
إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَفِي خُسۡرٍ
Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika khasara,
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡحَقِّ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ
Ila wale walio amini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na wakausiana kusubiri
وَيۡلٞ لِّكُلِّ هُمَزَةٖ لُّمَزَةٍ
Olewake kila safihi, msengenyaji!
ٱلَّذِي جَمَعَ مَالٗا وَعَدَّدَهُۥ
Aliye kusanya mali na kuyahisabu
يَحۡسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخۡلَدَهُۥ
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!