Surah: AL-A’LAQ 

Ayah : 17

فَلۡيَدۡعُ نَادِيَهُۥ

Basi na awaite wenzake!



Surah: AL-A’LAQ 

Ayah : 18

سَنَدۡعُ ٱلزَّبَانِيَةَ

Nasi tutawaita Mazabania!



Surah: AL-A’LAQ 

Ayah : 19

كَلَّا لَا تُطِعۡهُ وَٱسۡجُدۡۤ وَٱقۡتَرِب۩

Hasha! Usimtii! Nawe sujudu na ujongee!



Surah: AL-QADRI 

Ayah : 1

إِنَّآ أَنزَلۡنَٰهُ فِي لَيۡلَةِ ٱلۡقَدۡرِ

Hakika Sisi tumeiteremsha (Qur’ani) katika Laylatul Qadri (Usikuwa mtukufu wenye Cheo)



Surah: AL-QADRI 

Ayah : 2

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا لَيۡلَةُ ٱلۡقَدۡرِ

Na nini kitakacho kujuulisha nini Laylatul Qadri?



Surah: AL-QADRI 

Ayah : 3

لَيۡلَةُ ٱلۡقَدۡرِ خَيۡرٞ مِّنۡ أَلۡفِ شَهۡرٖ

Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu



Surah: AL-QADRI 

Ayah : 4

تَنَزَّلُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ فِيهَا بِإِذۡنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمۡرٖ

Huteremka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa kila jambo



Surah: AL-QADRI 

Ayah : 5

سَلَٰمٌ هِيَ حَتَّىٰ مَطۡلَعِ ٱلۡفَجۡرِ

(Ni) amani usiku huo mpaka mapambazuko ya alfajiri



Surah: AL-BAYYINAH 

Ayah : 1

لَمۡ يَكُنِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ وَٱلۡمُشۡرِكِينَ مُنفَكِّينَ حَتَّىٰ تَأۡتِيَهُمُ ٱلۡبَيِّنَةُ

Hawakuwa walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina (makafiri) waache walio nayo mpaka iwajie bayana,



Surah: AL-BAYYINAH 

Ayah : 2

رَسُولٞ مِّنَ ٱللَّهِ يَتۡلُواْ صُحُفٗا مُّطَهَّرَةٗ

Yaani Mtume aliyetoka kwa Allah anaye wasomea kurasa zilizo takasika,



Surah: AL-BAYYINAH 

Ayah : 3

فِيهَا كُتُبٞ قَيِّمَةٞ

Ndani yake mna maandiko yaliyo nyooka



Surah: AL-BAYYINAH 

Ayah : 4

وَمَا تَفَرَّقَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَتۡهُمُ ٱلۡبَيِّنَةُ

Wala hawakufarikiana walio pewa Kitabu ila baada ya kuwajia hiyo bayana



Surah: AL-BAYYINAH 

Ayah : 5

وَمَآ أُمِرُوٓاْ إِلَّا لِيَعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَ حُنَفَآءَ وَيُقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَيُؤۡتُواْ ٱلزَّكَوٰةَۚ وَذَٰلِكَ دِينُ ٱلۡقَيِّمَةِ

Nao hawakuamrishwa kitu isipokuwa wamuabudu Allah kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu, na washike Sala, na watoe Zaka. Na hiyo ndiyo Dini madhubuti



Surah: AL-BAYYINAH 

Ayah : 6

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ وَٱلۡمُشۡرِكِينَ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَآۚ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمۡ شَرُّ ٱلۡبَرِيَّةِ

Hakika walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina wataingia katika Moto wa Jahannamu wadumu milele humo. Hao ndio viumbe waovu kabisa



Surah: AL-BAYYINAH 

Ayah : 7

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمۡ خَيۡرُ ٱلۡبَرِيَّةِ

Hakika walio amini na wakatenda mema, hao ndio bora wa viumbe



Surah: AL-BAYYINAH 

Ayah : 8

جَزَآؤُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّـٰتُ عَدۡنٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۖ رَّضِيَ ٱللَّهُ عَنۡهُمۡ وَرَضُواْ عَنۡهُۚ ذَٰلِكَ لِمَنۡ خَشِيَ رَبَّهُۥ

Malipo yao kwa Mola wao Mlezi ni Bustani za daima, zipitazo mito kati yake. Wakae humo milele. Allah yupo radhi nao, na wao waporadhi naye. Hayo ni kwa anaye muogopa Mola wake Mlezi



Surah: AZZILZAAL 

Ayah : 1

إِذَا زُلۡزِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ زِلۡزَالَهَا

Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!



Surah: AZZILZAAL 

Ayah : 2

وَأَخۡرَجَتِ ٱلۡأَرۡضُ أَثۡقَالَهَا

Na itakapo toa ardhi mizigo yake!



Surah: AZZILZAAL 

Ayah : 3

وَقَالَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا لَهَا

Na mtu akasema: Ina nini?



Surah: AZZILZAAL 

Ayah : 4

يَوۡمَئِذٖ تُحَدِّثُ أَخۡبَارَهَا

Siku hiyo itahadithia khabari zake



Surah: AZZILZAAL 

Ayah : 5

بِأَنَّ رَبَّكَ أَوۡحَىٰ لَهَا

Kwasababu Mola wake Mlezi ameifunulia!



Surah: AZZILZAAL 

Ayah : 6

يَوۡمَئِذٖ يَصۡدُرُ ٱلنَّاسُ أَشۡتَاتٗا لِّيُرَوۡاْ أَعۡمَٰلَهُمۡ

Siku hiyo watu watatoka wakiwa tofauti tofauti wakaonyweshwe vitendo vyao!



Surah: AZZILZAAL 

Ayah : 7

فَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٍ خَيۡرٗا يَرَهُۥ

Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!



Surah: AZZILZAAL 

Ayah : 8

وَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٖ شَرّٗا يَرَهُۥ

Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!



Surah: AL-AADIYAAT 

Ayah : 1

وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا

Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,



Surah: AL-AADIYAAT 

Ayah : 2

فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا

Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,



Surah: AL-AADIYAAT 

Ayah : 3

فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا

Wakishambulia wakati wa asubuhi,



Surah: AL-AADIYAAT 

Ayah : 4

فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا

Huku wakitimua vumbi,



Surah: AL-AADIYAAT 

Ayah : 5

فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا

Na wakijitoma kati ya kundi,



Surah: AL-AADIYAAT 

Ayah : 6

إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ

Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!