Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 47

حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلۡيَقِينُ

Mpaka ikatufikia yakini (mauti)



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 48

فَمَا تَنفَعُهُمۡ شَفَٰعَةُ ٱلشَّـٰفِعِينَ

Basi haitowafaa uombezi wowote wa waombezi



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 49

فَمَا لَهُمۡ عَنِ ٱلتَّذۡكِرَةِ مُعۡرِضِينَ

Basi wana nini hata wanapuuza ukumbusho huu!



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 50

كَأَنَّهُمۡ حُمُرٞ مُّسۡتَنفِرَةٞ

Kama kwamba ni punda milia wenye kutimuliwa, (wenye kushtuka)



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 51

فَرَّتۡ مِن قَسۡوَرَةِۭ

Wamekimbia mbio kutokana na kumkimbia simba



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 52

بَلۡ يُرِيدُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُؤۡتَىٰ صُحُفٗا مُّنَشَّرَةٗ

Bali anataka kila mtu miongoni mwao apewe nyaraka zilizofunuliwa



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 53

كَلَّاۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ

Si hivyo! hasha! Bali hawaiogopi Akhera



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 54

كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذۡكِرَةٞ

Na sihivyo! Hakika hii (Qur’ani) ni mawaidha



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 55

فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ

Basi anayetaka atawaidhika



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 56

وَمَا يَذۡكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ هُوَ أَهۡلُ ٱلتَّقۡوَىٰ وَأَهۡلُ ٱلۡمَغۡفِرَةِ

Na hawatowaidhika isipokuwa Akitaka Allah; Yeye Ndiye mwenye kustahiki kuogopwa, na mwenye kustahiki kusamehe (madhambi)



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 1

لَآ أُقۡسِمُ بِيَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ

Nina apa kwa Siku ya Kiyama



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 2

وَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلنَّفۡسِ ٱللَّوَّامَةِ

Na nina apa kwa nafsi inayolaumu sana



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 3

أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجۡمَعَ عِظَامَهُۥ

Je, mwanadamu anadhani kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 4

بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُۥ

Ndio (tutaikusanya tu na) Tunao uwezo wa kuzifanya ziwe sawa sawa ncha za vidole vyake



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 5

بَلۡ يُرِيدُ ٱلۡإِنسَٰنُ لِيَفۡجُرَ أَمَامَهُۥ

Lakini mwanadamu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilizoko mbele yake



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 6

يَسۡـَٔلُ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلۡقِيَٰمَةِ

Anauliza: Ni lini hiyo Siku ya Kiyama?



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 7

فَإِذَا بَرِقَ ٱلۡبَصَرُ

Basi jicho litakapoduwaa (kwa kupatwa na bumbuwazi na fadhaa)



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 8

وَخَسَفَ ٱلۡقَمَرُ

Na mwezi utakapo patwa,



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 9

وَجُمِعَ ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ

Na vikakusanywa jua na mwezi ((Katika Kupatwa),



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 10

يَقُولُ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذٍ أَيۡنَ ٱلۡمَفَرُّ

Atasema Mwanadamu siku hiyo: Wapi pa kukimbilia?



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 11

كَلَّا لَا وَزَرَ

La! Hapana mahala pa kukimbilia!



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 12

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمُسۡتَقَرُّ

Kwa Mola wako siku hiyo ndio makazi ya (ya kutulia)



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 13

يُنَبَّؤُاْ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذِۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ

Siku hiyo ataambiwa Mtu yale aliyo yatanguliza na aliyo yakawiza



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 14

بَلِ ٱلۡإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٞ

Bali Mtu anajijua Vizuri Sana yeye mwenyewe



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 15

وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ

Ingawa atatoa nyudhuru chungu nzima



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 16

لَا تُحَرِّكۡ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعۡجَلَ بِهِۦٓ

Usiutikisie ulimi wako huu wahyi (ufunuo) kwa kuufanyia haraka



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 17

إِنَّ عَلَيۡنَا جَمۡعَهُۥ وَقُرۡءَانَهُۥ

Hakika ni juu Yetu kuikusanya na kukuwezesha kuisoma kwake



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 18

فَإِذَا قَرَأۡنَٰهُ فَٱتَّبِعۡ قُرۡءَانَهُۥ

Basi Tunapoisoma (kupitia Jibrili), fuata kusomwa kwake



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 19

ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا بَيَانَهُۥ

Kisha ni juu yetu kuubainisha



Surah: ALQIYAAMA 

Ayah : 20

كَلَّا بَلۡ تُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ

Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,