Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 17

سَأُرۡهِقُهُۥ صَعُودًا

Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 18

إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ

Kwani hakika yeye alifikiri na akapima



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 19

فَقُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ

Basi ameangamia! Namna alivyo pima



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 20

ثُمَّ قُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ

Tena ameangamia! Namna alivyo pima!



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 21

ثُمَّ نَظَرَ

Kisha akatazama



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 22

ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ

Kisha akakunja paji (la uso) na akafinya uso kwa ghadhabu



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 23

ثُمَّ أَدۡبَرَ وَٱسۡتَكۡبَرَ

Kisha akageuka nyuma, na akaipa kisogo haki, na akatakabari



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 24

فَقَالَ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ يُؤۡثَرُ

Na akasema: Hii (Qurani) si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 25

إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا قَوۡلُ ٱلۡبَشَرِ

Hii si chochote isipokuwa ni kauli ya binadamu



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 26

سَأُصۡلِيهِ سَقَرَ

Nitamuingiza (na kumuunguza) kwenye Moto wa saqar



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 27

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سَقَرُ

Na ni nini kitakujuulisha nini huo Moto wa Saqar?



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 28

لَا تُبۡقِي وَلَا تَذَرُ

Haubakishi wala hauachi, (kitu chochote)



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 29

لَوَّاحَةٞ لِّلۡبَشَرِ

Wenye kubabua vikali ngozi, (iwe nyeusi)



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 30

عَلَيۡهَا تِسۡعَةَ عَشَرَ

Juu yake wako (walinzi) kumi na tisa



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 31

وَمَا جَعَلۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَـٰٓئِكَةٗۖ وَمَا جَعَلۡنَا عِدَّتَهُمۡ إِلَّا فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيَسۡتَيۡقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَيَزۡدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِيمَٰنٗا وَلَا يَرۡتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَمَا يَعۡلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡبَشَرِ

Na Hatukuweka walinzi wa moto isipokuwa ni Malaika, na Hatukufanya idadi yao isipokuwa iwe ni mtihani kwa wale waliokufuru; ili wawe na yakini wale waliopewa Kitabu, na iwazidishie Imani wale walioamini; na wala wasitie shaka wale waliopewa Kitabu na Waumini; na ili wale waliokuwa na maradhi nyoyoni mwao (ya unafiki), na makafiri waseme: Allah Amekusudia nini kwa mfano huu? Hivyo ndivyo Allah Anavyompoteza Amtakaye na Anamuongoa Amtakaye. Na hakuna ajuaye majeshi ya Mola wako isipokuwa Yeye Peke yake, na haya hayakuwa isipokuwa ni ukumbusho tu kwa binadamu



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 32

كَلَّا وَٱلۡقَمَرِ

Sivyo hivyo! Naapa kwa mwezi



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 33

وَٱلَّيۡلِ إِذۡ أَدۡبَرَ

Na Naapa kwa usiku unapoondoka



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 34

وَٱلصُّبۡحِ إِذَآ أَسۡفَرَ

Na Naapa kwa asubuhi inapoangaza (inapo pambazuka)



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 35

إِنَّهَا لَإِحۡدَى ٱلۡكُبَرِ

Hakika huo (Moto) bila shaka ni mojawapo ya majanga makubwa kabisa



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 36

نَذِيرٗا لِّلۡبَشَرِ

Ni onyo kwa binadamu



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 37

لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَتَقَدَّمَ أَوۡ يَتَأَخَّرَ

Kwa atakaye miongoni mwenu atatangulia mbele au atachelewa nyuma



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 38

كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡ رَهِينَةٌ

Kila nafsi iko katika rehani kwa yale iliyoyachuma.[1]


1- - Kila nafsi itashikwa kwa iliyo yatenda.


Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 39

إِلَّآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡيَمِينِ

Isipokuwa watu wa kuliani



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 40

فِي جَنَّـٰتٖ يَتَسَآءَلُونَ

Hao watakuwa katika Mabustani ya Peponi, wanaulizana



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 41

عَنِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ

Kuhusu wakosefu



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 42

مَا سَلَكَكُمۡ فِي سَقَرَ

(Watawauliza): Nini kilicho kuingizeni katika Moto?



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 43

قَالُواْ لَمۡ نَكُ مِنَ ٱلۡمُصَلِّينَ

Watasema: Hatukuwa miongoni mwa wanaosali



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 44

وَلَمۡ نَكُ نُطۡعِمُ ٱلۡمِسۡكِينَ

Na wala hatukuwa tunalisha masikini



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 45

وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلۡخَآئِضِينَ

Na tulikuwa tukipiga porojo pamoja na wanaopiga porojo



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 46

وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na tulikuwa tunaikadhibisha Siku ya malipo