Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 13

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kundi kubwa katika wa mwanzo



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 14

وَقَلِيلٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na wachache katika wa mwishoni.[1]


1- - Hawa walio karibishwa mbele ni kundi la wengi katika mataifa yalio tangulia na Manabii wao, na wachache katika Umma wa Muhammad rehma na amani ziwe juu yake ukilinganishwa na hao.


Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 15

عَلَىٰ سُرُرٖ مَّوۡضُونَةٖ

watakua juu ya vitanda vilivyofumwa vizuri



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 16

مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيۡهَا مُتَقَٰبِلِينَ

hali wakiwa wameviegemea huku wakitazamana



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 17

يَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ

Watazungukiwa na vijana wenye kudumu



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 18

بِأَكۡوَابٖ وَأَبَارِيقَ وَكَأۡسٖ مِّن مَّعِينٖ

Kwa bilauri na mabirika na vikombe vya mvinyo kutoka kwenye chemchemu



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 19

لَّا يُصَدَّعُونَ عَنۡهَا وَلَا يُنزِفُونَ

Hawatapata maumivu ya kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawa-tatokwa na akili



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 20

وَفَٰكِهَةٖ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ

Na matunda watakayo pendelea wao



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 21

وَلَحۡمِ طَيۡرٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ

Na nyama za ndege katika wata-kazozitamani



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 22

وَحُورٌ عِينٞ

Na wanawake wenye macho makubwa yaliyo meupe sana na weusi sana



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 23

كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ

Kama mfano wa lulu zilizohi-fadhiwa



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 24

جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Ikiwa ni malipo kwa ambayo walikuwa wanatenda (duniani)



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 25

لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا

Hawatasikia humo maneno ya upuuzi wala yanayopelekea kupata madhambi



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 26

إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا

Isipokuwa itasemwa: Salama, na Amani!



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 27

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ

Na watu wa kuliani, ni wepi hao watu wa kuliani?



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 28

فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ

Watakuwa kwenye mikunazi isiyo na miba



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 29

وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ

Na migomba iliyopangiliwa



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 30

وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ

Na kivuli kilichotandazwa



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 31

وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ

Na maji yenye kumiminwa



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 32

وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ

Na matunda mengi



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 33

لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ

Hayana kikomo na wala hayakatazwi



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 34

وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ

Na matandiko ya kupumzikia yaliyoinuliwa



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 35

إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ

Hakika Sisi Tutawaumba (Mahurulaini) upya



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 36

فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا

Na tukawafanya kuwa bikra



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 37

عُرُبًا أَتۡرَابٗا

Wenye mahaba kwa waume zao, na wana umri unaolingana



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 38

لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Ni kwaajili ya watu wa kuliani



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 39

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kundi kubwa katika watu wa mwanzo



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 40

وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na kundi kubwa katika watu wa mwishoni



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 41

وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ

Na watu wa kushotoni, je, ni wepi watu wa kushotoni?



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 42

فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ

(Watakuwa) Kwenye moto ubabuao na maji yachemkayo