Surah: IBRAHIM 

Ayah : 36

رَبِّ إِنَّهُنَّ أَضۡلَلۡنَ كَثِيرٗا مِّنَ ٱلنَّاسِۖ فَمَن تَبِعَنِي فَإِنَّهُۥ مِنِّيۖ وَمَنۡ عَصَانِي فَإِنَّكَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Ewe Mola wangu Mlezi, hakika hayo (masanamu) yamewapoteza watu wengi mno. Basi kwa aliyenifuata mimi huyo ni wangu, na aliyeniasi, hakika Wewe ni Mwenye kusamehe mwenye kurehemu



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 37

رَّبَّنَآ إِنِّيٓ أَسۡكَنتُ مِن ذُرِّيَّتِي بِوَادٍ غَيۡرِ ذِي زَرۡعٍ عِندَ بَيۡتِكَ ٱلۡمُحَرَّمِ رَبَّنَا لِيُقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ فَٱجۡعَلۡ أَفۡـِٔدَةٗ مِّنَ ٱلنَّاسِ تَهۡوِيٓ إِلَيۡهِمۡ وَٱرۡزُقۡهُم مِّنَ ٱلثَّمَرَٰتِ لَعَلَّهُمۡ يَشۡكُرُونَ

Mola wetu Mlezi, hakika mimi nimewaweka baadhi ya dhuriya zangu (Ismaili na mama yake) kwenye bonde lisilokuwa na mimea, kwenye Nyumba yako Takatifu, ewe Mola wetu Mlezi, ili wasimamishe Swala. Basi zijaalie nyoyo za watu zielekee kwao, na waruzuku kila aina ya matunda, ili wapate kushukuru



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 38

رَبَّنَآ إِنَّكَ تَعۡلَمُ مَا نُخۡفِي وَمَا نُعۡلِنُۗ وَمَا يَخۡفَىٰ عَلَى ٱللَّهِ مِن شَيۡءٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا فِي ٱلسَّمَآءِ

Ewe Mola wetu Mlezi, hakika Wewe unajua tunayoyaficha na tunayo yadhihirisha. Na hakuna kinachofichikana kwa Allah katika ardhi wala katika mbingu



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 39

ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ ٱلَّذِي وَهَبَ لِي عَلَى ٱلۡكِبَرِ إِسۡمَٰعِيلَ وَإِسۡحَٰقَۚ إِنَّ رَبِّي لَسَمِيعُ ٱلدُّعَآءِ

Himdi zote ni za Allah aliyenitunuku (watoto) katika hali ya uzee, Ismail na Is-haq. Hakika Mola wangu Mlezi ni Mwenye kusikia maombi



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 40

رَبِّ ٱجۡعَلۡنِي مُقِيمَ ٱلصَّلَوٰةِ وَمِن ذُرِّيَّتِيۚ رَبَّنَا وَتَقَبَّلۡ دُعَآءِ

(Ewe) Mola wangu Mlezi, nijaalie niwe mwenye kusimamisha Swala, na katika watoto dhuriya zangu pia. Ewe Mola wetu Mlezi, na ipokee dua yangu



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 41

رَبَّنَا ٱغۡفِرۡ لِي وَلِوَٰلِدَيَّ وَلِلۡمُؤۡمِنِينَ يَوۡمَ يَقُومُ ٱلۡحِسَابُ

(Ewe) Mola wetu Mlezi, unisamehe mimi na wazazi wangu wote wawili[1], na Waumini (wote), Siku ya kusimama hesabu


1- - Na hii ya kuwaombea wazazi wake ilikuwa kabla ya kuwabaini kuwa ni maamdui wa Allah, kwani alipojua
alijitenga nao.


Surah: IBRAHIM 

Ayah : 42

وَلَا تَحۡسَبَنَّ ٱللَّهَ غَٰفِلًا عَمَّا يَعۡمَلُ ٱلظَّـٰلِمُونَۚ إِنَّمَا يُؤَخِّرُهُمۡ لِيَوۡمٖ تَشۡخَصُ فِيهِ ٱلۡأَبۡصَٰرُ

(Ewe Mtume) Wala usidhani kwamba Allah ameghafilika na wanayo yafanya madhalimu. Hakika Yeye anachelewesha tu (kuwaadhibu papo hapo) mpaka siku yatapo kodoka macho yao



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 43

مُهۡطِعِينَ مُقۡنِعِي رُءُوسِهِمۡ لَا يَرۡتَدُّ إِلَيۡهِمۡ طَرۡفُهُمۡۖ وَأَفۡـِٔدَتُهُمۡ هَوَآءٞ

(Utawaoana makafiri siku watakayotoka makaburini) Wako mbiombio, vichwa juu, na macho hayapepesi, na nyoyo zao tupu (kwa hofu)



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 44

وَأَنذِرِ ٱلنَّاسَ يَوۡمَ يَأۡتِيهِمُ ٱلۡعَذَابُ فَيَقُولُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ رَبَّنَآ أَخِّرۡنَآ إِلَىٰٓ أَجَلٖ قَرِيبٖ نُّجِبۡ دَعۡوَتَكَ وَنَتَّبِعِ ٱلرُّسُلَۗ أَوَلَمۡ تَكُونُوٓاْ أَقۡسَمۡتُم مِّن قَبۡلُ مَا لَكُم مِّن زَوَالٖ

Na waonye watu siku itapowajia adhabu, na waseme waliodhulumu: Ewe Mola wetu Mlezi, tupe muhula (muda kidogo angalau) tuitikie wito wako na tuwafuate Mitume. (Watajibiwa kwa shere) Kwani nyinyi si mliapa zamani kwamba hamtaondolewa (duniani na kurejeshwa Akhera)?



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 45

وَسَكَنتُمۡ فِي مَسَٰكِنِ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ وَتَبَيَّنَ لَكُمۡ كَيۡفَ فَعَلۡنَا بِهِمۡ وَضَرَبۡنَا لَكُمُ ٱلۡأَمۡثَالَ

Na mliishi kwenye maskani zile zile za waliozidhulumu nafsi zao. Na ilikudhihirikieni jinsi tulivyowatendea. Nasi tuliwapigieni mifano mingi (katika Qur’an ili mzingatie lakini wapi)



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 46

وَقَدۡ مَكَرُواْ مَكۡرَهُمۡ وَعِندَ ٱللَّهِ مَكۡرُهُمۡ وَإِن كَانَ مَكۡرُهُمۡ لِتَزُولَ مِنۡهُ ٱلۡجِبَالُ

Na kwa hakika (makafiri) walifanya vitimbi vyao, na Allah alivipindua vitimbi vyao. Ijapokuwa vitimbi vyao (kwa ukubwa na mikakati michafu vilikuwa na uwezo wa) kuondosha milima



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 47

فَلَا تَحۡسَبَنَّ ٱللَّهَ مُخۡلِفَ وَعۡدِهِۦ رُسُلَهُۥٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٞ ذُو ٱنتِقَامٖ

Basi usimdhanie Allah kuwa ni mwenye kukhalifu ahadi zake (kwa) Mitume wake. Hakika Allah ni Mwenye nguvu sana, (na) ni Mwenye kulipiza (dhidi ya maadui wake)



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 48

يَوۡمَ تُبَدَّلُ ٱلۡأَرۡضُ غَيۡرَ ٱلۡأَرۡضِ وَٱلسَّمَٰوَٰتُۖ وَبَرَزُواْ لِلَّهِ ٱلۡوَٰحِدِ ٱلۡقَهَّارِ

(Malipo yatakuwa) Siku itapogeuzwa ardhi iwe ardhi nyingine, na mbingu pia. Nao watahudhuria mbele ya Allah, Mwenye nguvu mno



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 49

وَتَرَى ٱلۡمُجۡرِمِينَ يَوۡمَئِذٖ مُّقَرَّنِينَ فِي ٱلۡأَصۡفَادِ

Na utawaona wahalifu siku hiyo wamefungwa katika minyororo



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 50

سَرَابِيلُهُم مِّن قَطِرَانٖ وَتَغۡشَىٰ وُجُوهَهُمُ ٱلنَّارُ

Mavazi yao yatakuwa ya lami (nyeusi tii na yananuka), na nyuso zao zitagubikwa na Moto



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 51

لِيَجۡزِيَ ٱللَّهُ كُلَّ نَفۡسٖ مَّا كَسَبَتۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ

(Watu watatoka makaburini) ili Allah ailipe kila nafsi kwa yale iliyo yachuma. Hakika Allah ni Mwepesi wa kuhesabu



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 52

هَٰذَا بَلَٰغٞ لِّلنَّاسِ وَلِيُنذَرُواْ بِهِۦ وَلِيَعۡلَمُوٓاْ أَنَّمَا هُوَ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞ وَلِيَذَّكَّرَ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَٰبِ

Hii (Qur’ani) ni ufikisho (wa ujumbe) kwa watu, na ili waonywe na ili wapate kujua kuwa, uhakika ni kwamba Yeye (Allah) ni Muabudiwa mmoja tu, na ili wenye akili wapate kuonyeka