Surah: ATTAUBA 

Ayah : 26

ثُمَّ أَنزَلَ ٱللَّهُ سَكِينَتَهُۥ عَلَىٰ رَسُولِهِۦ وَعَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَأَنزَلَ جُنُودٗا لَّمۡ تَرَوۡهَا وَعَذَّبَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ وَذَٰلِكَ جَزَآءُ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Kisha Allah akateremsha utulivu wake kwa Mtume wake na kwa Waumini, na akateremsha majeshi ambayo hamkuyaona na akawaadhibu wale waliokufuru. Na hiyo ndio malipo ya makafiri



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 27

ثُمَّ يَتُوبُ ٱللَّهُ مِنۢ بَعۡدِ ذَٰلِكَ عَلَىٰ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Kisha baada ya hayo Allah anamsamehe amtakaye. Na Allah ni Mwenye kusamehe sana, Mwenye kuhurumia mno



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 28

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِنَّمَا ٱلۡمُشۡرِكُونَ نَجَسٞ فَلَا يَقۡرَبُواْ ٱلۡمَسۡجِدَ ٱلۡحَرَامَ بَعۡدَ عَامِهِمۡ هَٰذَاۚ وَإِنۡ خِفۡتُمۡ عَيۡلَةٗ فَسَوۡفَ يُغۡنِيكُمُ ٱللَّهُ مِن فَضۡلِهِۦٓ إِن شَآءَۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمٌ حَكِيمٞ

Enyi mlioamini, hakika washiri-kina (makafiri) ni Najisi.[1] Kwa hivyo, wasiusogelee Msikiti Mtukufu (wa Makka) baada ya mwaka wao huu[2]. Na ikiwa mnachelea umasikini (kwa kukatikiwa na misaada au biashara zitokazo kwao), basi Allah atakutajirisheni kutoka katika fadhila zake akitaka. Hakika, Allah ni Mwenye kujua mno, Mwenye hekima nyingi


1- - Najisi inayokusudiwa hapa ni Najisi na uchafu wa itikadi, na sio kwamba ni uchafu wa mwili wa kutofaa kukaa pamoja, kula pamoja au kupeana mikono.


2- - Zuio na marufuku hii ilianza mwaka wa tisa wa Hijiria kwa Kalenda ya Kiislamu. Zuio hili linahusu Msikiti Mtukufu wa Makka tu. Ama misikiti mingine, kafiri anaweza kuingia ikiwa kuna sababu ya kufanya hivyo kama Mtume (Allah amshushie rehema na amani, alivyoruhusu makafiri kadhaa kuingia katika msikiti wa Madina kwa sababu mbali mbali.


Surah: ATTAUBA 

Ayah : 29

قَٰتِلُواْ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَلَا بِٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَلَا يُحَرِّمُونَ مَا حَرَّمَ ٱللَّهُ وَرَسُولُهُۥ وَلَا يَدِينُونَ دِينَ ٱلۡحَقِّ مِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ حَتَّىٰ يُعۡطُواْ ٱلۡجِزۡيَةَ عَن يَدٖ وَهُمۡ صَٰغِرُونَ

(Enyi Waislamu) Piganeni na wasiomuamini Allah wala Siku ya Mwisho na hawaharamishi alivyoviharimisha Allah na Mtume wake na hawafuati Dini ya Haki, miongoni mwa waliopewa Kitabu, mpaka watoe kodi[1] kwa hiari yao na wao wakiwa dhalili.[2]


1- - Jizia ni kodi maalumu anayoitoa kafiri mwenye uwezo wa kuitoa katika serikali ya Kiislamu kwa sababu ya huduma anazozipata ikiwemo ulinzi na usalama wa maisha yake, mwili wake, mali yake, dini yake, hadhi na heshima yake.


2- - Maana ya Aya hii ni maelekezo kwa mamlaka ya serikali ya Kiislamu ambayo imeshika hatamu. Sio maelekezo kwa mtu mmoja mmoja au kikundi kisichokuwa na mamlaka ya kisheria.


Surah: ATTAUBA 

Ayah : 30

وَقَالَتِ ٱلۡيَهُودُ عُزَيۡرٌ ٱبۡنُ ٱللَّهِ وَقَالَتِ ٱلنَّصَٰرَى ٱلۡمَسِيحُ ٱبۡنُ ٱللَّهِۖ ذَٰلِكَ قَوۡلُهُم بِأَفۡوَٰهِهِمۡۖ يُضَٰهِـُٔونَ قَوۡلَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن قَبۡلُۚ قَٰتَلَهُمُ ٱللَّهُۖ أَنَّىٰ يُؤۡفَكُونَ

Na Wayahudi walisema: Uzeri ni Mwana wa Allah. Na Wanaswara walisema: Masihi ni Mwana wa Allah (Mwana wa Mungu). Hiyo ni kauli yao (waisemayo) kwa vinywa vyao. Wanayaiga maneno ya waliokufuru kabla yao. Allah amewalaani. Inakuwaje wanapotoshwa?



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 31

ٱتَّخَذُوٓاْ أَحۡبَارَهُمۡ وَرُهۡبَٰنَهُمۡ أَرۡبَابٗا مِّن دُونِ ٱللَّهِ وَٱلۡمَسِيحَ ٱبۡنَ مَرۡيَمَ وَمَآ أُمِرُوٓاْ إِلَّا لِيَعۡبُدُوٓاْ إِلَٰهٗا وَٰحِدٗاۖ لَّآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۚ سُبۡحَٰنَهُۥ عَمَّا يُشۡرِكُونَ

(Wayahudi na Wanaswara) Wamewafanya watawa wao na makuhani wao Miungu (kwa kuwaabudu) badala ya Allah, na pia Masihi bin Mariamu (wamemfanya Mungu)[1]. Na hawakuamrishwa isipokuwa wamuabudu Mola mmoja tu. Hakuna muabudiwa (wa haki) ila Yeye tu. Ametakasika na hayo wanayomshirikisha nayo


1- - Wayahudi na Wanaswara wamewafanya watawa na wanazuoni wao Miungu badala ya Allah kwa sababu ya kuwatii katika kila jambo, hata katika yale mambo ambayo yapo tofauti na maandiko na mafundisho sahihi ya dini. Utiifu wa aina hii na utayari wa aina hii wa kutii katika kamusi ya Kiislamu unahisabika kwamba ni ibada. Hii ni tahadhari kwa Waislamu ya kuacha kuiga mwenendo huu wa kuwatii viongozi katika mambo ambayo yanapingana na maandiko na maelekezo sahihi ya dini. Utiifu usiokuwa na mipaka kwa mujibu wa Uislamu ni ibada na unatakiwa afanyiwe Allah tu.


Surah: ATTAUBA 

Ayah : 32

يُرِيدُونَ أَن يُطۡفِـُٔواْ نُورَ ٱللَّهِ بِأَفۡوَٰهِهِمۡ وَيَأۡبَى ٱللَّهُ إِلَّآ أَن يُتِمَّ نُورَهُۥ وَلَوۡ كَرِهَ ٱلۡكَٰفِرُونَ

(Makafiri) Wanataka kuizima Nuru ya Allah (Uislamu) kwa vinywa vyao, na Allah anakataa ila (ni lazima) aitimize Nuru yake (Dini yake na kumnusuru Nabii wake) na hata kama makafiri watachukia



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 33

هُوَ ٱلَّذِيٓ أَرۡسَلَ رَسُولَهُۥ بِٱلۡهُدَىٰ وَدِينِ ٱلۡحَقِّ لِيُظۡهِرَهُۥ عَلَى ٱلدِّينِ كُلِّهِۦ وَلَوۡ كَرِهَ ٱلۡمُشۡرِكُونَ

Yeye (Allah) ndiye aliyemtuma Mtume wake kwa uwongofu (Qur’an) na Dini ya Haki ili ipate kuzishinda dini zote, na hata kama washirikina watachukia