Surah: AL-AALAA 

Ayah : 1

سَبِّحِ ٱسۡمَ رَبِّكَ ٱلۡأَعۡلَى

Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 2

ٱلَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ

Aliye umba, na akaweka sawa,



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 3

وَٱلَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ

Na ambaye amekadiria na akaongoa,



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 4

وَٱلَّذِيٓ أَخۡرَجَ ٱلۡمَرۡعَىٰ

Na aliye otesha malisho,



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 5

فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحۡوَىٰ

Kisha akayafanya makavu, meusi



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 6

سَنُقۡرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ

Tutakusomesha wala hutasahau,



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 7

إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلۡجَهۡرَ وَمَا يَخۡفَىٰ

Ila akipenda Allah. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 8

وَنُيَسِّرُكَ لِلۡيُسۡرَىٰ

Na tutakusahilishia yawe mepesi



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 9

فَذَكِّرۡ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكۡرَىٰ

Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 10

سَيَذَّكَّرُ مَن يَخۡشَىٰ

Atakumbuka mwenye kuogopa



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 11

وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلۡأَشۡقَى

Na atajitenga mbali nayo mpotovu,



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 12

ٱلَّذِي يَصۡلَى ٱلنَّارَ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Ambaye atauingia Moto mkubwa



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 13

ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحۡيَىٰ

Tena humo hatakufa wala hawi hai



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 14

قَدۡ أَفۡلَحَ مَن تَزَكَّىٰ

Hakika amekwisha fanikiwa aliyejitakasa



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 15

وَذَكَرَ ٱسۡمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ

Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 16

بَلۡ تُؤۡثِرُونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Lakini nyinyi mnakhiari (mnapenda sana) maisha ya dunia!



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 17

وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ وَأَبۡقَىٰٓ

Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 18

إِنَّ هَٰذَا لَفِي ٱلصُّحُفِ ٱلۡأُولَىٰ

Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 19

صُحُفِ إِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ

Vitabu vya Ibrahimu na Mussa