Surah: A’BASA

Ayah : 1

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ

Alikunja paji lake la uso na akageuka



Surah: A’BASA

Ayah : 2

أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ

Kwasababu alimjia kipofu



Surah: A’BASA

Ayah : 3

وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ

Na nini kitakachokujulisha; huwenda akatakasika?



Surah: A’BASA

Ayah : 4

أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ

Au akawaidhika na yakamnufaisha mawaidha?



Surah: A’BASA

Ayah : 5

أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ

Ama yule ajionaye amejitosheleza (hana haja na mawaidha)



Surah: A’BASA

Ayah : 6

فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ

Basi wewe ndio unamgeukia na kushughulika naye?



Surah: A’BASA

Ayah : 7

وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ

Na si juu yako wewe asipotakasika



Surah: A’BASA

Ayah : 8

وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ

Na ama yule aliyekujia kwa kukukimbilia



Surah: A’BASA

Ayah : 9

وَهُوَ يَخۡشَىٰ

Na huku akiogopa (adhabu ya Allah)



Surah: A’BASA

Ayah : 10

فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ

Basi ndio wewe unampuuza?



Surah: A’BASA

Ayah : 11

كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ

Sivyo hivyo! Hakika, hii [Qurani] ni mawaidha



Surah: A’BASA

Ayah : 12

فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ

Basi anayetaka, akumbushike kwayo



Surah: A’BASA

Ayah : 13

فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ

Nayo hii Qur’ani imo katika kurasa zilizo tukuzwa



Surah: A’BASA

Ayah : 14

مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ

Zilizo inuliwa, zilizo takaswa



Surah: A’BASA

Ayah : 15

بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ

Katika mikono ya Malaika waandishi



Surah: A’BASA

Ayah : 16

كِرَامِۭ بَرَرَةٖ

Walio watukufu, walio wema



Surah: A’BASA

Ayah : 17

قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ

Amelaaniwa na Kuangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha? [Au ukafiri ulioje alionao?]



Surah: A’BASA

Ayah : 18

مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ

Hivi hakumbuki! Kwa kitu gani amemuumba?



Surah: A’BASA

Ayah : 19

مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ

Kutokana na tone la manii, Amemuumba, Akamkadiria, [Akamuwezesha]



Surah: A’BASA

Ayah : 20

ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ

Kisha akamsahilishia njia



Surah: A’BASA

Ayah : 21

ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ

Kisha akamfisha, akamtia kaburini



Surah: A’BASA

Ayah : 22

ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ

Kisha Atakapotaka, Atamfufua



Surah: A’BASA

Ayah : 23

كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ

Si hivyo! Hakutimiza Aliyomuamuru (Allah)



Surah: A’BASA

Ayah : 24

فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ

Basi atazame mwanaadam chakula chake



Surah: A’BASA

Ayah : 25

أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا

Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu



Surah: A’BASA

Ayah : 26

ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا

Kisha Tukaipasua ardhi mipasuko



Surah: A’BASA

Ayah : 27

فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا

Kisha tukaotesha humo nafaka mbali mbali



Surah: A’BASA

Ayah : 28

وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا

Na mizabibu na mimea ya mboga (ikatwayo ikamea tena)



Surah: A’BASA

Ayah : 29

وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا

Na mizaituni na mitende



Surah: A’BASA

Ayah : 30

وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا

Na mabustani yaliyositawi na kusongamana miti yake