Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 1

ٱلۡحَآقَّةُ

Tukio la haki



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 2

مَا ٱلۡحَآقَّةُ

Ni nini tukio la haki?



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 3

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحَآقَّةُ

Na ni nini kitakachokujuulisha; ni nini hilo tukio la haki?



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 4

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ وَعَادُۢ بِٱلۡقَارِعَةِ

Kina Thamudi na Adi walikadhibisha tukio (Kiyama) lenye kugonga (na kutia kiwewe)



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 5

فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهۡلِكُواْ بِٱلطَّاغِيَةِ

Ama kina Thamudi, waliangamizwa kwa ukelele mkali sana



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 6

وَأَمَّا عَادٞ فَأُهۡلِكُواْ بِرِيحٖ صَرۡصَرٍ عَاتِيَةٖ

Na ama kina Adi, waliangamizwa kwa upepo wenye baridi kali, uvumao kwa nguvu



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 7

سَخَّرَهَا عَلَيۡهِمۡ سَبۡعَ لَيَالٖ وَثَمَٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومٗاۖ فَتَرَى ٱلۡقَوۡمَ فِيهَا صَرۡعَىٰ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٍ خَاوِيَةٖ

(Allah) Aliwapelekea mausiku saba na michana minane mfululizo (bila kupumzika). Basi utaona watu wameanguka kifudifudi kana kwamba ni magogo ya mitende yaliyo wazi ndani



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 8

فَهَلۡ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٖ

Basi je, unamuona yeyote aliyebaki?



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 9

وَجَآءَ فِرۡعَوۡنُ وَمَن قَبۡلَهُۥ وَٱلۡمُؤۡتَفِكَٰتُ بِٱلۡخَاطِئَةِ

Na Firauni na wale waliokuwepo kabla yake na (watu wa) miji iliyopinduliwa (chini juu kwa sababu ya madhambi yao) walikuja kufanya makosa pia



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 10

فَعَصَوۡاْ رَسُولَ رَبِّهِمۡ فَأَخَذَهُمۡ أَخۡذَةٗ رَّابِيَةً

Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye (Allah) akawakamata (na kuwaadhibu) kwa mkamato wa nguvu sana



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 11

إِنَّا لَمَّا طَغَا ٱلۡمَآءُ حَمَلۡنَٰكُمۡ فِي ٱلۡجَارِيَةِ

Maji Yalipofurika Hakika Sisi Tuliwapandisheni Katika Merikebu



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 12

لِنَجۡعَلَهَا لَكُمۡ تَذۡكِرَةٗ وَتَعِيَهَآ أُذُنٞ وَٰعِيَةٞ

Ili tuifanye kuwa ni ukumbusho kwenu, na ibakie kumbukumbu katika sikio linalobakisha kumbukumbu



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 13

فَإِذَا نُفِخَ فِي ٱلصُّورِ نَفۡخَةٞ وَٰحِدَةٞ

Na litakapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 14

وَحُمِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَٱلۡجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةٗ وَٰحِدَةٗ

Na ardhi na majabali ikaondolewa kisha ika pondwa pondwa mpondo mmoja



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 15

فَيَوۡمَئِذٖ وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ

Basi siku hiyo ndio litatokea tukio la kutokea



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 16

وَٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَهِيَ يَوۡمَئِذٖ وَاهِيَةٞ

Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 17

وَٱلۡمَلَكُ عَلَىٰٓ أَرۡجَآئِهَاۚ وَيَحۡمِلُ عَرۡشَ رَبِّكَ فَوۡقَهُمۡ يَوۡمَئِذٖ ثَمَٰنِيَةٞ

Na Malaika Watakuwa Wame-simama Kandoni Mwake, Na Siku Hiyo Juu Yao Malaika Wanane Watakibeba Kiti Cha Enzi Cha Mola Wako



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 18

يَوۡمَئِذٖ تُعۡرَضُونَ لَا تَخۡفَىٰ مِنكُمۡ خَافِيَةٞ

Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika kwenu siri yoyote yenu



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 19

فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَيَقُولُ هَآؤُمُ ٱقۡرَءُواْ كِتَٰبِيَهۡ

Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 20

إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَٰقٍ حِسَابِيَهۡ

Hakika mimi niliyakinisha kuwa hakiki mimi ni mwenye kukutana na hesabu yangu!



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 21

فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ

Basi Yeye Atakuwa Katika Maisha Ya Raha



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 22

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ

Katika Bustani (Pepo) Iliyo Juu,



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 23

قُطُوفُهَا دَانِيَةٞ

Vishada Vyake (vya matunda) Vitakuwa Karibu:



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 24

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَآ أَسۡلَفۡتُمۡ فِي ٱلۡأَيَّامِ ٱلۡخَالِيَةِ

(Wataambiwa): Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyoyatanguliza katika siku nyingi zilizopita



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 25

وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِشِمَالِهِۦ فَيَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي لَمۡ أُوتَ كِتَٰبِيَهۡ

Na ama yule atakayepewa kitabu chake kushotoni mwake; atasema: Ee! Laiti nisingelipewa kitabu changu!



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 26

وَلَمۡ أَدۡرِ مَا حِسَابِيَهۡ

Wala nisingeli jua nini hesabu yangu



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 27

يَٰلَيۡتَهَا كَانَتِ ٱلۡقَاضِيَةَ

Ee! Laiti yangelikuwa (mauti) ndio kumalizika kwangu



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 28

مَآ أَغۡنَىٰ عَنِّي مَالِيَهۡۜ

Haikunifaa mali yangu



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 29

هَلَكَ عَنِّي سُلۡطَٰنِيَهۡ

Madaraka yangu yamenitoweka



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 30

خُذُوهُ فَغُلُّوهُ

(Ataambiwa): Mchukueni, na mfungeni pingu