Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 1

قَدۡ سَمِعَ ٱللَّهُ قَوۡلَ ٱلَّتِي تُجَٰدِلُكَ فِي زَوۡجِهَا وَتَشۡتَكِيٓ إِلَى ٱللَّهِ وَٱللَّهُ يَسۡمَعُ تَحَاوُرَكُمَآۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَمِيعُۢ بَصِيرٌ

Hakika, Allah amekwishasikia kauli ya yule mwanamke anayejadiliana nawe (ewe Muhammad) kuhusu mumewe, na anamshitakia Allah, na Allah anayasikia majibizano yenu. Hakika, Allah ni Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 2

ٱلَّذِينَ يُظَٰهِرُونَ مِنكُم مِّن نِّسَآئِهِم مَّا هُنَّ أُمَّهَٰتِهِمۡۖ إِنۡ أُمَّهَٰتُهُمۡ إِلَّا ٱلَّـٰٓـِٔي وَلَدۡنَهُمۡۚ وَإِنَّهُمۡ لَيَقُولُونَ مُنكَرٗا مِّنَ ٱلۡقَوۡلِ وَزُورٗاۚ وَإِنَّ ٱللَّهَ لَعَفُوٌّ غَفُورٞ

Wale miongoni mwenu ambao wanawatamkia wake zao Dhwihari[1], (Nyinyi kwetu kama migongo ya mama zetu). Hao wake zao si mama zao. Hawakuwa mama zao isipokuwa wale waliowazaa. Na hakika wao bila shaka wanasema kauli ya kuchukiza na uongo. Na hakika Allah bila shaka ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa Maghfira


1- - Dhwihari ni mume kumfananisha mkewe na mwanamke mwengine ambae kwake ni haramu kumuoa.


Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 3

وَٱلَّذِينَ يُظَٰهِرُونَ مِن نِّسَآئِهِمۡ ثُمَّ يَعُودُونَ لِمَا قَالُواْ فَتَحۡرِيرُ رَقَبَةٖ مِّن قَبۡلِ أَن يَتَمَآسَّاۚ ذَٰلِكُمۡ تُوعَظُونَ بِهِۦۚ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ

Na wale ambao wanaowatamkia wake zao dhwihaar, kisha wakarudi katika waliyoyasema (kuitengua dhwihaar), basi ni kuacha huru mtumwa kabla ya kugusana. Hayo mnawaidhiwa kwayo. Na Allah kwa yale myatendayo ni Mwenye khabari kwa yale mnayo yatenda



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 4

فَمَن لَّمۡ يَجِدۡ فَصِيَامُ شَهۡرَيۡنِ مُتَتَابِعَيۡنِ مِن قَبۡلِ أَن يَتَمَآسَّاۖ فَمَن لَّمۡ يَسۡتَطِعۡ فَإِطۡعَامُ سِتِّينَ مِسۡكِينٗاۚ ذَٰلِكَ لِتُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦۚ وَتِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِۗ وَلِلۡكَٰفِرِينَ عَذَابٌ أَلِيمٌ

Na yule asiyepata uwezo, basi afunge Swiyaam miezi miwili mfululuzo kabla ya kugusana. Na yule asiyeweza, basi alishe chakula masikini sitini. Hivyo ili mumuamini Allah na Rasuli Wake. Na hiyo ni mipaka ya Allah. Na makafiri watapata adhabu iumizayo



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 5

إِنَّ ٱلَّذِينَ يُحَآدُّونَ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ كُبِتُواْ كَمَا كُبِتَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۚ وَقَدۡ أَنزَلۡنَآ ءَايَٰتِۭ بَيِّنَٰتٖۚ وَلِلۡكَٰفِرِينَ عَذَابٞ مُّهِينٞ

Hakika wale wanao pinzana na Allah na Mtume Wake watadhalilishwa kama walivyo dhalilishwa wale wa kabla yao. Na Tumekwishateremsha Ishara zilizo wazi na makafiri watapata adhabu ya kudhalilisha



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 6

يَوۡمَ يَبۡعَثُهُمُ ٱللَّهُ جَمِيعٗا فَيُنَبِّئُهُم بِمَا عَمِلُوٓاْۚ أَحۡصَىٰهُ ٱللَّهُ وَنَسُوهُۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٌ

Siku Atakayowafufua Allah wote, Awajulishe yale waliyoyatenda, Allah Ameyadhibiti na wao wameyasahau; na Allah ni Shahidi juu ya kila kitu



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 7

أَلَمۡ تَرَ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۖ مَا يَكُونُ مِن نَّجۡوَىٰ ثَلَٰثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمۡ وَلَا خَمۡسَةٍ إِلَّا هُوَ سَادِسُهُمۡ وَلَآ أَدۡنَىٰ مِن ذَٰلِكَ وَلَآ أَكۡثَرَ إِلَّا هُوَ مَعَهُمۡ أَيۡنَ مَا كَانُواْۖ ثُمَّ يُنَبِّئُهُم بِمَا عَمِلُواْ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۚ إِنَّ ٱللَّهَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٌ

Je, huoni kwamba Allah Anajua yaliyomo mbinguni na yaliyomo ardhini? Hauwi mnong’ono wa watatu isipokuwa Yeye ni wa nne wao (kwa ujuzi Wake), na wala watano isipokuwa Yeye ni wa sita wao (kwa ujuzi Wake), na wala chini kuliko ya hivyo, na wala wengi zaidi isipokuwa Yeye Yu pamoja nao (kwa ujuzi Wake) popote watakapokuwa; kisha Siku ya Kiyama Atawajulisha yale waliyoyatenda. Hakika Allah kwa kila kitu ni mjuzi



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 8

أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِينَ نُهُواْ عَنِ ٱلنَّجۡوَىٰ ثُمَّ يَعُودُونَ لِمَا نُهُواْ عَنۡهُ وَيَتَنَٰجَوۡنَ بِٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡعُدۡوَٰنِ وَمَعۡصِيَتِ ٱلرَّسُولِۖ وَإِذَا جَآءُوكَ حَيَّوۡكَ بِمَا لَمۡ يُحَيِّكَ بِهِ ٱللَّهُ وَيَقُولُونَ فِيٓ أَنفُسِهِمۡ لَوۡلَا يُعَذِّبُنَا ٱللَّهُ بِمَا نَقُولُۚ حَسۡبُهُمۡ جَهَنَّمُ يَصۡلَوۡنَهَاۖ فَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Je, huwaoni wale waliokatazwa kunong’ona, kisha wanarudia yale waliyokatazwa nayo, na wananong’onezana kuhusu dhambi na uadui na kumuasi Mtume. Na wanapokujia wanakuamkia kwa maamkizi Asiyokuamkia kwayo Allah; na wanasema katika nafsi zao: Mbona Allah Hatuadhibu kwa yale tunayoyasema? Jahannam inawatosheleza, wataingia waungue, basi ubaya ulioje mahali pa kuishia



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 9

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا تَنَٰجَيۡتُمۡ فَلَا تَتَنَٰجَوۡاْ بِٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡعُدۡوَٰنِ وَمَعۡصِيَتِ ٱلرَّسُولِ وَتَنَٰجَوۡاْ بِٱلۡبِرِّ وَٱلتَّقۡوَىٰۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ ٱلَّذِيٓ إِلَيۡهِ تُحۡشَرُونَ

Enyi walioamini! Mna-ponong’onezana, basi msinon-g’onezane kuhusu dhambi na uadui na kumuasi Mtume, bali nong’onezaneni kuhusu wema na taqwa; na mcheni Allah Ambaye Kwake Pekee mtakusanywa



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 10

إِنَّمَا ٱلنَّجۡوَىٰ مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ لِيَحۡزُنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَلَيۡسَ بِضَآرِّهِمۡ شَيۡـًٔا إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۚ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ

Hakika mnong’ono unatokana na shaytwaan ili awahuzunishe wale walioamini, na wala hawezi kuwadhuru chochote isipokuwa kwa idhini ya Allah. Na kwa Allah wategemee wenye kuaumini



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 11

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا قِيلَ لَكُمۡ تَفَسَّحُواْ فِي ٱلۡمَجَٰلِسِ فَٱفۡسَحُواْ يَفۡسَحِ ٱللَّهُ لَكُمۡۖ وَإِذَا قِيلَ ٱنشُزُواْ فَٱنشُزُواْ يَرۡفَعِ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنكُمۡ وَٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡعِلۡمَ دَرَجَٰتٖۚ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ

Enyi walioamini! Mnapoambiwa: Fanyeni nafasi katika mabaraza, basi fanyeni nafasi; Allah Atakufanyieni nafasi. Na mnapoambiwa: Inukeni, basi inukeni; Allah Atawainua wale walioamini miongoni mwenu na waliopewa elimu daraja za juu. Na Allah kwa yale myatendayo ni Mwenye khabari nayo



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 12

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا نَٰجَيۡتُمُ ٱلرَّسُولَ فَقَدِّمُواْ بَيۡنَ يَدَيۡ نَجۡوَىٰكُمۡ صَدَقَةٗۚ ذَٰلِكَ خَيۡرٞ لَّكُمۡ وَأَطۡهَرُۚ فَإِن لَّمۡ تَجِدُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٌ

Enyi walioamini! Mnapotaka kushauriana siri na Mtume basi tangulizeni kwanza swadaka kabla ya kusemezana kwenu na Mtume. Hivyo ni kheri kwenu na utakaso zaidi. Na msipopata, basi hakika Allah ni Mwingi wa msamaha na Mwenye kurehemu



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 13

ءَأَشۡفَقۡتُمۡ أَن تُقَدِّمُواْ بَيۡنَ يَدَيۡ نَجۡوَىٰكُمۡ صَدَقَٰتٖۚ فَإِذۡ لَمۡ تَفۡعَلُواْ وَتَابَ ٱللَّهُ عَلَيۡكُمۡ فَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُواْ ٱلزَّكَوٰةَ وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥۚ وَٱللَّهُ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ

Je, mnakhofu kutanguliza hiyo swadaka kabla ya kusemezana kwenu? Ikiwa hamjafanya hayo, na Allah Akapokea toba yenu; basi simamisheni Sala, na toeni Zaka, na mtiini Allah na Mtume Wake; na Allah ni Mwenye khabari kwa yale myatendayo



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 14

۞أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِينَ تَوَلَّوۡاْ قَوۡمًا غَضِبَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِم مَّا هُم مِّنكُمۡ وَلَا مِنۡهُمۡ وَيَحۡلِفُونَ عَلَى ٱلۡكَذِبِ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ

Je, hukuona wale waliofanya urafiki na watu ambao Allah Amewakasirikia?, wao si katika nyinyi, na wala si katika wao, na wanaapia uongo hali yakuwa wanajua



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 15

أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُمۡ عَذَابٗا شَدِيدًاۖ إِنَّهُمۡ سَآءَ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Allah Amewaandalia adhabu kali, hakika ni uovu ulioje waliokuwa wakiutenda



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 16

ٱتَّخَذُوٓاْ أَيۡمَٰنَهُمۡ جُنَّةٗ فَصَدُّواْ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ فَلَهُمۡ عَذَابٞ مُّهِينٞ

Wamefanya viapo vyao kuwa ni kinga hivyo wakazuia njia ya Allah, basi hao watapata adhabu idhalilishayo



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 17

لَّن تُغۡنِيَ عَنۡهُمۡ أَمۡوَٰلُهُمۡ وَلَآ أَوۡلَٰدُهُم مِّنَ ٱللَّهِ شَيۡـًٔاۚ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Hazitowafaa kitu chochote mali zao na wala watoto wao mbele ya Allah, hao ni watu wa motoni, wao humo ni wenye kudumu milele



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 18

يَوۡمَ يَبۡعَثُهُمُ ٱللَّهُ جَمِيعٗا فَيَحۡلِفُونَ لَهُۥ كَمَا يَحۡلِفُونَ لَكُمۡ وَيَحۡسَبُونَ أَنَّهُمۡ عَلَىٰ شَيۡءٍۚ أَلَآ إِنَّهُمۡ هُمُ ٱلۡكَٰذِبُونَ

Siku Atakayowafufua Allah wote, watamwapia kama wanavyokuapieni nyinyi, na wanadhania kwamba wamepata kitu, Tanabahi! Hakika wao ni waongo



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 19

ٱسۡتَحۡوَذَ عَلَيۡهِمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ فَأَنسَىٰهُمۡ ذِكۡرَ ٱللَّهِۚ أُوْلَـٰٓئِكَ حِزۡبُ ٱلشَّيۡطَٰنِۚ أَلَآ إِنَّ حِزۡبَ ٱلشَّيۡطَٰنِ هُمُ ٱلۡخَٰسِرُونَ

Shetani amewatawala, akawasahaulisha kumkumbuka Allah, hao ndio kundi la shetani. Zindukeni! Hakika kundi la shetani ndio lenye kukhasirika. (lenye kupata khasara)



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 20

إِنَّ ٱلَّذِينَ يُحَآدُّونَ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥٓ أُوْلَـٰٓئِكَ فِي ٱلۡأَذَلِّينَ

Hakika wale wanaompinga Allah na Mtume Wake hao ndio miongoni mwa madhalili



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 21

كَتَبَ ٱللَّهُ لَأَغۡلِبَنَّ أَنَا۠ وَرُسُلِيٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ قَوِيٌّ عَزِيزٞ

Allah Amekwishaandika kwamba: Bila shaka Nitashinda Mimi na Mitume Wangu. Hakika Allah ni Mwenye nguvu zote, Mwenye kushinda



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 22

لَّا تَجِدُ قَوۡمٗا يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ يُوَآدُّونَ مَنۡ حَآدَّ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَلَوۡ كَانُوٓاْ ءَابَآءَهُمۡ أَوۡ أَبۡنَآءَهُمۡ أَوۡ إِخۡوَٰنَهُمۡ أَوۡ عَشِيرَتَهُمۡۚ أُوْلَـٰٓئِكَ كَتَبَ فِي قُلُوبِهِمُ ٱلۡإِيمَٰنَ وَأَيَّدَهُم بِرُوحٖ مِّنۡهُۖ وَيُدۡخِلُهُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ رَضِيَ ٱللَّهُ عَنۡهُمۡ وَرَضُواْ عَنۡهُۚ أُوْلَـٰٓئِكَ حِزۡبُ ٱللَّهِۚ أَلَآ إِنَّ حِزۡبَ ٱللَّهِ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Hutokuta watu wanaomuamini Allah na Siku ya Mwisho kuwa wanafanya urafiki na kuwapenda wanaompinga Allah na Mtume Wake, japo wakiwa ni baba zao, au watoto wao, au ndugu zao, au jamaa zao. Hao (Allah) Ameandika katika nyoyo zao Imani, na Akawatia nguvu kwa Roho (Wahyi) kutoka Kwake, na Atawaingiza kwenye Mabustani yapitayo chini yake mito humo watakaa milele. Allah Ameridhika nao, nao wameridhika Naye. Hao ndio kundi la Allah. Zindukeni! Hakika kundi la Allah ndio lenye kufaulu