Surah: AL-QAMAR

Ayah : 1

ٱقۡتَرَبَتِ ٱلسَّاعَةُ وَٱنشَقَّ ٱلۡقَمَرُ

Kimekaribia Kiyama na mwezi umepasuka



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 2

وَإِن يَرَوۡاْ ءَايَةٗ يُعۡرِضُواْ وَيَقُولُواْ سِحۡرٞ مُّسۡتَمِرّٞ

Na (Makafiri kila) wanapoona Aya yoyote (ishara/muujiza) wanakengeuka na kusema: (Huu) Ni uchawi endelevu



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 3

وَكَذَّبُواْ وَٱتَّبَعُوٓاْ أَهۡوَآءَهُمۡۚ وَكُلُّ أَمۡرٖ مُّسۡتَقِرّٞ

Na wamekadhibisha (haki) na wamefuata utashi wa nafsi zao. Na kila jambo (la kheri au la shari) litatulia (mahali pake. Watu wema watalipwa wema na watu wabaya watalipwa ubaya)



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 4

وَلَقَدۡ جَآءَهُم مِّنَ ٱلۡأَنۢبَآءِ مَا فِيهِ مُزۡدَجَرٌ

Na kwa yakini kabisa, katika habari muhimu, imekwishawajia habari ambayo ndani yake mna makemeo makali



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 5

حِكۡمَةُۢ بَٰلِغَةٞۖ فَمَا تُغۡنِ ٱلنُّذُرُ

Ni hekima ya kiwango cha juu kabisa, lakini maonyo (wanayopewa) hayasaidii kitu



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 6

فَتَوَلَّ عَنۡهُمۡۘ يَوۡمَ يَدۡعُ ٱلدَّاعِ إِلَىٰ شَيۡءٖ نُّكُرٍ

Basi wapuuze (na waache waingoje) siku (ya Kiyama ambapo) mnadi (mtangazaji) atanadi (atatangaza ili watu waende) kwenye jambo la kutisha sana



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 7

خُشَّعًا أَبۡصَٰرُهُمۡ يَخۡرُجُونَ مِنَ ٱلۡأَجۡدَاثِ كَأَنَّهُمۡ جَرَادٞ مُّنتَشِرٞ

Macho yao yakiwa dhalili, watatoka katika makaburi kama kwamba wao ni nzige waliosambaa



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 8

مُّهۡطِعِينَ إِلَى ٱلدَّاعِۖ يَقُولُ ٱلۡكَٰفِرُونَ هَٰذَا يَوۡمٌ عَسِرٞ

Wenye kukimbia mbio huku wakibinua shingo zao wakielekea kwa muitaji; makafiri watasema: Hii ni siku ngumu!



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 9

۞كَذَّبَتۡ قَبۡلَهُمۡ قَوۡمُ نُوحٖ فَكَذَّبُواْ عَبۡدَنَا وَقَالُواْ مَجۡنُونٞ وَٱزۡدُجِرَ

Walikadhibisha kabla yao watu wa nuhu na wakamkadhibisha mja wetu wakasema mwendawazimu na akafanyiwa maudhi



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 10

فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنِّي مَغۡلُوبٞ فَٱنتَصِرۡ

Basi akamwita Mola wake mlezi kwamba: Hakika mimi nimeshindwa (nimezidiwa nguvu) basi ni Nusuru



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 11

فَفَتَحۡنَآ أَبۡوَٰبَ ٱلسَّمَآءِ بِمَآءٖ مُّنۡهَمِرٖ

Tukafungua milango ya mbingu kwa maji yanayofoka na kumiminika kwa nguvu



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 12

وَفَجَّرۡنَا ٱلۡأَرۡضَ عُيُونٗا فَٱلۡتَقَى ٱلۡمَآءُ عَلَىٰٓ أَمۡرٖ قَدۡ قُدِرَ

Na tukaipasua ardhi yote kwa chemchem, na yakakutana maji kwa pamoja kwa jambo lililokadiriwa



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 13

وَحَمَلۡنَٰهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلۡوَٰحٖ وَدُسُرٖ

Na Tukambeba kwenye ile (jahazi) yenye mbao na misumari



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 14

تَجۡرِي بِأَعۡيُنِنَا جَزَآءٗ لِّمَن كَانَ كُفِرَ

Kikienda haraka tukikitazama kwa macho yetu ikiwa ni malipo kwa ambaye alikuwa amekufuru



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 15

وَلَقَد تَّرَكۡنَٰهَآ ءَايَةٗ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na kwa yakini Tumeiacha iwe ni mazingatio, Je, basi yuko yeyote mwenye kuwaidhika?



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 16

فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi vipi ilikuwa adhabu Yangu na maonyo Yangu?



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 17

وَلَقَدۡ يَسَّرۡنَا ٱلۡقُرۡءَانَ لِلذِّكۡرِ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na Hakika Tumeirahisisha Qur’an Kwa Ajili Ya Ukumbusho Je Kuna Mwenye kukumbuka?



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 18

كَذَّبَتۡ عَادٞ فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Kina ‘Aad walikadhibisha, basi vipi ilikuwa adhabu Yangu na maonyo Yangu?



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 19

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ رِيحٗا صَرۡصَرٗا فِي يَوۡمِ نَحۡسٖ مُّسۡتَمِرّٖ

Hakika Sisi Tumewapelekea upepo wa kimbunga wenye sauti kali na baridi kali katika siku korofi yenye kuendelea mfululizo



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 20

تَنزِعُ ٱلنَّاسَ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٖ مُّنقَعِرٖ

Unawang’oa watu kana kwamba vigogo vya mtende vilong’olewa



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 21

فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi vipi ilikuwa adhabu Yangu na maonyo Yangu?



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 22

وَلَقَدۡ يَسَّرۡنَا ٱلۡقُرۡءَانَ لِلذِّكۡرِ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na Hakika Tumeirahisisha Qur’an Kwa Ajili Ya Ukumbusho Je Kuna Mwenye kukumbuka?



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 23

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِٱلنُّذُرِ

Kina Thamuwd waliwakadhibisha Waonyaji



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 24

فَقَالُوٓاْ أَبَشَرٗا مِّنَّا وَٰحِدٗا نَّتَّبِعُهُۥٓ إِنَّآ إِذٗا لَّفِي ضَلَٰلٖ وَسُعُرٍ

Wakasema: Ah! Tumfuate binaadamu miongoni mwetu? Hakika hapo sisi tutakuwa katika upotofu na wazimu



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 25

أَءُلۡقِيَ ٱلذِّكۡرُ عَلَيۡهِ مِنۢ بَيۡنِنَا بَلۡ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٞ

Ah! Ameteremshiwa ukumbusho (Wahyi) baina yetu? Bali yeye ni muongo mkubwa mwenye kiburi mno



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 26

سَيَعۡلَمُونَ غَدٗا مَّنِ ٱلۡكَذَّابُ ٱلۡأَشِرُ

Watakuja kujua kesho nani muongo mkubwa mwenye kiburi mno



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 27

إِنَّا مُرۡسِلُواْ ٱلنَّاقَةِ فِتۡنَةٗ لَّهُمۡ فَٱرۡتَقِبۡهُمۡ وَٱصۡطَبِرۡ

Hakika Sisi Tutawapelekea ngamia jike awe jaribio kwao, basi (Ee Nabiy Swaalih) watazame na vuta subira



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 28

وَنَبِّئۡهُمۡ أَنَّ ٱلۡمَآءَ قِسۡمَةُۢ بَيۡنَهُمۡۖ كُلُّ شِرۡبٖ مُّحۡتَضَرٞ

Na wajulishe kwamba maji ni mgawanyo baina yao (ngamia na wao), kila sehemu ya maji itahudhuriwa (kwa zamu)



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 29

فَنَادَوۡاْ صَاحِبَهُمۡ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ

Wakamuita Mtu Wao Akajipa Ushujaa Na Kumchinja



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 30

فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi Vipi Ilikua Adhabu Yangu Na Maonyo yangu?