Surah: QAAF 

Ayah : 1

قٓۚ وَٱلۡقُرۡءَانِ ٱلۡمَجِيدِ

Qaaf. Nina apa kwa Qur’ani Tukufu



Surah: QAAF 

Ayah : 2

بَلۡ عَجِبُوٓاْ أَن جَآءَهُم مُّنذِرٞ مِّنۡهُمۡ فَقَالَ ٱلۡكَٰفِرُونَ هَٰذَا شَيۡءٌ عَجِيبٌ

Bali wamestaajabu kwamba amewajia muonyaji miongoni mwao, na kwa sababu hiyo makafiri wakasema: “Hili ni jambo la ajabu sana!



Surah: QAAF 

Ayah : 3

أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗاۖ ذَٰلِكَ رَجۡعُۢ بَعِيدٞ

Je, hivi tukifa na tukawa udongo (tutafufuliwa)? Kurejea huko kuko mbali sana”



Surah: QAAF 

Ayah : 4

قَدۡ عَلِمۡنَا مَا تَنقُصُ ٱلۡأَرۡضُ مِنۡهُمۡۖ وَعِندَنَا كِتَٰبٌ حَفِيظُۢ

Hakika, sisi tumejua kila ambacho ardhi inakipunguza kwao[1] na tunacho Kitabu kinachohifadhi barabara


1- - Kinachokusudiwa hap ani kwamba, kwa Allah hakipotei kitu. Pamoja na kwamba, makafifiri katika Aya iliyopita kabla ya hii wanaona kwamba wakifa na kuzikwa miili yao inaoza ardhini na kwamba si jambo linalowezekana kurejea tena kwenye hali yao ya zamani, Allah anasema hilo kwake ni jepesi na hakuna kitakachopotea.


Surah: QAAF 

Ayah : 5

بَلۡ كَذَّبُواْ بِٱلۡحَقِّ لَمَّا جَآءَهُمۡ فَهُمۡ فِيٓ أَمۡرٖ مَّرِيجٍ

Bali wameikadhibisha (wamei-pinga) haki ilipowajia. Basi wao wamo katika jambo la mkorogeko



Surah: QAAF 

Ayah : 6

أَفَلَمۡ يَنظُرُوٓاْ إِلَى ٱلسَّمَآءِ فَوۡقَهُمۡ كَيۡفَ بَنَيۡنَٰهَا وَزَيَّنَّـٰهَا وَمَا لَهَا مِن فُرُوجٖ

Je, hawatazami mbingu juu yao, vipi Tumezijenga na Tumezipamba, na wala hazina mipasuko yoyote



Surah: QAAF 

Ayah : 7

وَٱلۡأَرۡضَ مَدَدۡنَٰهَا وَأَلۡقَيۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ وَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوۡجِۭ بَهِيجٖ

Na ardhi Tumeitandaza na Tukaiwekea milima thabiti, na Tukaotesha humo kila aina ya mimea ya kupendeza



Surah: QAAF 

Ayah : 8

تَبۡصِرَةٗ وَذِكۡرَىٰ لِكُلِّ عَبۡدٖ مُّنِيبٖ

Ni ufumbuzi wa macho na ukumbusho kwa kila mja mwenye kuelekea kwa Allah



Surah: QAAF 

Ayah : 9

وَنَزَّلۡنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ مُّبَٰرَكٗا فَأَنۢبَتۡنَا بِهِۦ جَنَّـٰتٖ وَحَبَّ ٱلۡحَصِيدِ

Na Tukateremsha kutoka mbinguni maji yaliyobarikiwa, kisha Tukaotesha kwayo mabustani na nafaka za kuvunwa



Surah: QAAF 

Ayah : 10

وَٱلنَّخۡلَ بَاسِقَٰتٖ لَّهَا طَلۡعٞ نَّضِيدٞ

Na mitende mirefu yenye mashada (makole) ya matunda yenye kuzaa kwa wingi



Surah: QAAF 

Ayah : 11

رِّزۡقٗا لِّلۡعِبَادِۖ وَأَحۡيَيۡنَا بِهِۦ بَلۡدَةٗ مَّيۡتٗاۚ كَذَٰلِكَ ٱلۡخُرُوجُ

Ili iwe ni riziki kwa waja wangu. Na Tukahuisha kwayo nchi iliyokufa, kama hivyo ndivyo utakavyokuwa ufufuaji



Surah: QAAF 

Ayah : 12

كَذَّبَتۡ قَبۡلَهُمۡ قَوۡمُ نُوحٖ وَأَصۡحَٰبُ ٱلرَّسِّ وَثَمُودُ

Walikadhibisha kabla yao watu wa Nuhu na wakazi wa Ar-Rass na kina Thamud



Surah: QAAF 

Ayah : 13

وَعَادٞ وَفِرۡعَوۡنُ وَإِخۡوَٰنُ لُوطٖ

Na kina Aad na Firaun na ndugu wa Lutwi



Surah: QAAF 

Ayah : 14

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡأَيۡكَةِ وَقَوۡمُ تُبَّعٖۚ كُلّٞ كَذَّبَ ٱلرُّسُلَ فَحَقَّ وَعِيدِ

Na wakaazi wa Machakani na watu wa Tubbaa, wote walikadhibisha Mitume. Basi onyo likathibitika juu yao



Surah: QAAF 

Ayah : 15

أَفَعَيِينَا بِٱلۡخَلۡقِ ٱلۡأَوَّلِۚ بَلۡ هُمۡ فِي لَبۡسٖ مِّنۡ خَلۡقٖ جَدِيدٖ

Je, kwani Tulichoka kwa uumbaji wa kwanza? Bali wao wamo katika shaka juu ya uumbaji upya (kufufuliwa)



Surah: QAAF 

Ayah : 16

وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ وَنَعۡلَمُ مَا تُوَسۡوِسُ بِهِۦ نَفۡسُهُۥۖ وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنۡ حَبۡلِ ٱلۡوَرِيدِ

Na kwa yakini Tumemuumba Mtu na Tunajua yale inayowaza nafsi yake, na Sisi Tuko karibu naye kuliko mshipa wa shingoni mwake



Surah: QAAF 

Ayah : 17

إِذۡ يَتَلَقَّى ٱلۡمُتَلَقِّيَانِ عَنِ ٱلۡيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ قَعِيدٞ

Pale wanapopokea wapokeaji wawili (Malaika) wanaokaa kuliani na kushotoni



Surah: QAAF 

Ayah : 18

مَّا يَلۡفِظُ مِن قَوۡلٍ إِلَّا لَدَيۡهِ رَقِيبٌ عَتِيدٞ

Hatamki kauli yoyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi)



Surah: QAAF 

Ayah : 19

وَجَآءَتۡ سَكۡرَةُ ٱلۡمَوۡتِ بِٱلۡحَقِّۖ ذَٰلِكَ مَا كُنتَ مِنۡهُ تَحِيدُ

Na uchungu wa mauti (wa kutoka roho) utakapomjia kwa haki. (Itasemwa): Hayo ndiyo yale uliyokuwa ukiyakimbia



Surah: QAAF 

Ayah : 20

وَنُفِخَ فِي ٱلصُّورِۚ ذَٰلِكَ يَوۡمُ ٱلۡوَعِيدِ

Na litapulizwa baragumu. Hiyo ndio Siku ya miadi. (makamiano)



Surah: QAAF 

Ayah : 21

وَجَآءَتۡ كُلُّ نَفۡسٖ مَّعَهَا سَآئِقٞ وَشَهِيدٞ

Na kila nafsi itakuja pamoja nayo mcungaji na shahidi



Surah: QAAF 

Ayah : 22

لَّقَدۡ كُنتَ فِي غَفۡلَةٖ مِّنۡ هَٰذَا فَكَشَفۡنَا عَنكَ غِطَآءَكَ فَبَصَرُكَ ٱلۡيَوۡمَ حَدِيدٞ

(Aambiwe): Kwa yakini ulikuwa umeghafilika na haya! Basi Tumekuondoshea kifuniko chako (pazia lako), basi kuona kwako leo ni kukali



Surah: QAAF 

Ayah : 23

وَقَالَ قَرِينُهُۥ هَٰذَا مَا لَدَيَّ عَتِيدٌ

Na Malaika wake aliyepewa jukumu atasema: Hii (rekodi) iliyoko kwangu imeshatayarishwa



Surah: QAAF 

Ayah : 24

أَلۡقِيَا فِي جَهَنَّمَ كُلَّ كَفَّارٍ عَنِيدٖ

(Allaah Atasema): Mtupeni katika Jahannam kila kafiri, mkaidi!



Surah: QAAF 

Ayah : 25

مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٖ مُّرِيبٍ

Mzuiaji wa kheri, mwenye kuruka mipaka, mwenye kutia shaka



Surah: QAAF 

Ayah : 26

ٱلَّذِي جَعَلَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَأَلۡقِيَاهُ فِي ٱلۡعَذَابِ ٱلشَّدِيدِ

Ambaye amefanya mwabudiwa mwengine pamoja na Allah, basi mtupeni katika adhabu kali



Surah: QAAF 

Ayah : 27

۞قَالَ قَرِينُهُۥ رَبَّنَا مَآ أَطۡغَيۡتُهُۥ وَلَٰكِن كَانَ فِي ضَلَٰلِۭ بَعِيدٖ

Shatani mwenzake atasema: Ee Mola wetu mlezi! Sikumpoteza mimi, bali yeye mwenyewe alikuwa katika upotofu wa mbali. (na haki)



Surah: QAAF 

Ayah : 28

قَالَ لَا تَخۡتَصِمُواْ لَدَيَّ وَقَدۡ قَدَّمۡتُ إِلَيۡكُم بِٱلۡوَعِيدِ

(Allah) Atasema: Msigombane mbele yangu, na hali Nilikuleteeni onyo Langu!



Surah: QAAF 

Ayah : 29

مَا يُبَدَّلُ ٱلۡقَوۡلُ لَدَيَّ وَمَآ أَنَا۠ بِظَلَّـٰمٖ لِّلۡعَبِيدِ

Haibadilishwi kauli Kwangu, Nami si mwenye kudhulumu waja wangu



Surah: QAAF 

Ayah : 30

يَوۡمَ نَقُولُ لِجَهَنَّمَ هَلِ ٱمۡتَلَأۡتِ وَتَقُولُ هَلۡ مِن مَّزِيدٖ

Siku Tutakapoiambia Jahannam: Je, umeshajaa? Nayo itasema: Je, kuna ziada yoyote?