Surah: MARYAM 

Ayah : 91

أَن دَعَوۡاْ لِلرَّحۡمَٰنِ وَلَدٗا

Kwa kudai kwao kuwa (Allah) Mwingi wa Rehema ana mtoto



Surah: MARYAM 

Ayah : 92

وَمَا يَنۢبَغِي لِلرَّحۡمَٰنِ أَن يَتَّخِذَ وَلَدًا

Na haitakiwi kwa (Allah) Mwingi wa Rehema kuwa na mtoto.[1]


1- - Aya hizi tano 88, 89, 90, 91 na 92 zinakataa kwa ukali itikadi kwamba Mungu ana mtoto. Muislamu hatakiwi kabisa kuikumbatia itikadi hii au kuishabikia. Ni itikadi mbaya mno kiasi kwamba mbingu, ardhi na milima haziivumilii kuisikia.


Surah: MARYAM 

Ayah : 93

إِن كُلُّ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ إِلَّآ ءَاتِي ٱلرَّحۡمَٰنِ عَبۡدٗا

Hapana yeyote aliyomo mbinguni na ardhini ila atafika kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa ni mtumwa wake



Surah: MARYAM 

Ayah : 94

لَّقَدۡ أَحۡصَىٰهُمۡ وَعَدَّهُمۡ عَدّٗا

Yeye hakika amewadhibiti na amewahesabu sawa sawa



Surah: MARYAM 

Ayah : 95

وَكُلُّهُمۡ ءَاتِيهِ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ فَرۡدًا

Na kila mmoja katika wao atamfikia Siku ya Kiyama peke yake



Surah: MARYAM 

Ayah : 96

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ سَيَجۡعَلُ لَهُمُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وُدّٗا

Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi



Surah: MARYAM 

Ayah : 97

فَإِنَّمَا يَسَّرۡنَٰهُ بِلِسَانِكَ لِتُبَشِّرَ بِهِ ٱلۡمُتَّقِينَ وَتُنذِرَ بِهِۦ قَوۡمٗا لُّدّٗا

Na hakika tumeifanya nyepesi (Qur’ani) kwa ulimi wako, ili uwabashirie kwayo wacha Mungu, na uwaonye kwayo watu wabishi



Surah: MARYAM 

Ayah : 98

وَكَمۡ أَهۡلَكۡنَا قَبۡلَهُم مِّن قَرۡنٍ هَلۡ تُحِسُّ مِنۡهُم مِّنۡ أَحَدٍ أَوۡ تَسۡمَعُ لَهُمۡ رِكۡزَۢا

Na kaumu ngapi tuziangamiza kabla yao. Je! Unawaona hata mmoja katika wao au unasikia hata mchakato wao