Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 31

لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ

Hakiwafuniki, na wala hakiwa-kingi na muwako wa moto



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 32

إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ

Hakika Moto huo hurusha macheche Kama majumba!



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 33

كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ

Kana kwamba ni ngamia waku-bwa wa rangi ya manjano!



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 34

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 35

هَٰذَا يَوۡمُ لَا يَنطِقُونَ

Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 36

وَلَا يُؤۡذَنُ لَهُمۡ فَيَعۡتَذِرُونَ

Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 37

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 38

هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِۖ جَمَعۡنَٰكُمۡ وَٱلۡأَوَّلِينَ

Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 39

فَإِن كَانَ لَكُمۡ كَيۡدٞ فَكِيدُونِ

Ikiwa mnayo hila yoyote ile basi Nifanyieni mimi



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 40

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 41

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ

Hakika wacha Mungu watakuwa katika vivuli na chemchem



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 42

وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ

Na matunda katika yale wanayoyatamani



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 43

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

(Wataabiwa): Kuleni na kunyweni kwa furaha kwasababu ya yale mliyokuwa mkiyatenda



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 44

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakika sisi ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 45

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 46

كُلُواْ وَتَمَتَّعُواْ قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجۡرِمُونَ

Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 47

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 48

وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱرۡكَعُواْ لَا يَرۡكَعُونَ

Na walipokuwa wakiambiwa Rukuuni (mswali), hawakuwa wakirukuu



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 49

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 50

فَبِأَيِّ حَدِيثِۭ بَعۡدَهُۥ يُؤۡمِنُونَ

Basi maneno gani baada ya hii (Qurani) watayaamini?