Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 31

وَمَا جَعَلۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَـٰٓئِكَةٗۖ وَمَا جَعَلۡنَا عِدَّتَهُمۡ إِلَّا فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيَسۡتَيۡقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَيَزۡدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِيمَٰنٗا وَلَا يَرۡتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَمَا يَعۡلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡبَشَرِ

Na Hatukuweka walinzi wa moto isipokuwa ni Malaika, na Hatukufanya idadi yao isipokuwa iwe ni mtihani kwa wale waliokufuru; ili wawe na yakini wale waliopewa Kitabu, na iwazidishie Imani wale walioamini; na wala wasitie shaka wale waliopewa Kitabu na Waumini; na ili wale waliokuwa na maradhi nyoyoni mwao (ya unafiki), na makafiri waseme: Allah Amekusudia nini kwa mfano huu? Hivyo ndivyo Allah Anavyompoteza Amtakaye na Anamuongoa Amtakaye. Na hakuna ajuaye majeshi ya Mola wako isipokuwa Yeye Peke yake, na haya hayakuwa isipokuwa ni ukumbusho tu kwa binadamu



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 32

كَلَّا وَٱلۡقَمَرِ

Sivyo hivyo! Naapa kwa mwezi



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 33

وَٱلَّيۡلِ إِذۡ أَدۡبَرَ

Na Naapa kwa usiku unapoondoka



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 34

وَٱلصُّبۡحِ إِذَآ أَسۡفَرَ

Na Naapa kwa asubuhi inapoangaza (inapo pambazuka)



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 35

إِنَّهَا لَإِحۡدَى ٱلۡكُبَرِ

Hakika huo (Moto) bila shaka ni mojawapo ya majanga makubwa kabisa



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 36

نَذِيرٗا لِّلۡبَشَرِ

Ni onyo kwa binadamu



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 37

لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَتَقَدَّمَ أَوۡ يَتَأَخَّرَ

Kwa atakaye miongoni mwenu atatangulia mbele au atachelewa nyuma



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 38

كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡ رَهِينَةٌ

Kila nafsi iko katika rehani kwa yale iliyoyachuma.[1]


1- - Kila nafsi itashikwa kwa iliyo yatenda.


Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 39

إِلَّآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡيَمِينِ

Isipokuwa watu wa kuliani



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 40

فِي جَنَّـٰتٖ يَتَسَآءَلُونَ

Hao watakuwa katika Mabustani ya Peponi, wanaulizana



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 41

عَنِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ

Kuhusu wakosefu



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 42

مَا سَلَكَكُمۡ فِي سَقَرَ

(Watawauliza): Nini kilicho kuingizeni katika Moto?



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 43

قَالُواْ لَمۡ نَكُ مِنَ ٱلۡمُصَلِّينَ

Watasema: Hatukuwa miongoni mwa wanaosali



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 44

وَلَمۡ نَكُ نُطۡعِمُ ٱلۡمِسۡكِينَ

Na wala hatukuwa tunalisha masikini



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 45

وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلۡخَآئِضِينَ

Na tulikuwa tukipiga porojo pamoja na wanaopiga porojo



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 46

وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na tulikuwa tunaikadhibisha Siku ya malipo



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 47

حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلۡيَقِينُ

Mpaka ikatufikia yakini (mauti)



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 48

فَمَا تَنفَعُهُمۡ شَفَٰعَةُ ٱلشَّـٰفِعِينَ

Basi haitowafaa uombezi wowote wa waombezi



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 49

فَمَا لَهُمۡ عَنِ ٱلتَّذۡكِرَةِ مُعۡرِضِينَ

Basi wana nini hata wanapuuza ukumbusho huu!



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 50

كَأَنَّهُمۡ حُمُرٞ مُّسۡتَنفِرَةٞ

Kama kwamba ni punda milia wenye kutimuliwa, (wenye kushtuka)



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 51

فَرَّتۡ مِن قَسۡوَرَةِۭ

Wamekimbia mbio kutokana na kumkimbia simba



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 52

بَلۡ يُرِيدُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُؤۡتَىٰ صُحُفٗا مُّنَشَّرَةٗ

Bali anataka kila mtu miongoni mwao apewe nyaraka zilizofunuliwa



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 53

كَلَّاۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ

Si hivyo! hasha! Bali hawaiogopi Akhera



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 54

كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذۡكِرَةٞ

Na sihivyo! Hakika hii (Qur’ani) ni mawaidha



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 55

فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ

Basi anayetaka atawaidhika



Surah: ALMUDDATH-THIR 

Ayah : 56

وَمَا يَذۡكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ هُوَ أَهۡلُ ٱلتَّقۡوَىٰ وَأَهۡلُ ٱلۡمَغۡفِرَةِ

Na hawatowaidhika isipokuwa Akitaka Allah; Yeye Ndiye mwenye kustahiki kuogopwa, na mwenye kustahiki kusamehe (madhambi)