Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 31

ثُمَّ ٱلۡجَحِيمَ صَلُّوهُ

Kisha kwenye moto uwakao vikali mtupeni humo!



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 32

ثُمَّ فِي سِلۡسِلَةٖ ذَرۡعُهَا سَبۡعُونَ ذِرَاعٗا فَٱسۡلُكُوهُ

Mkamateni Na Mtieni Minyororo Shingoni Mwake,



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 33

إِنَّهُۥ كَانَ لَا يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ ٱلۡعَظِيمِ

Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Allah Mtukufu



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 34

وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ

Wala Hakuhimiza Juu Ya Kulisha Maskini



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 35

فَلَيۡسَ لَهُ ٱلۡيَوۡمَ هَٰهُنَا حَمِيمٞ

Basi Leo Hapa Hana Rafiki Mpenzi ( wa kumwonea uchungu)



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 36

وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنۡ غِسۡلِينٖ

Na wala hana chakula isipokuwa maji ya usaha ya vidonda vilivyooshwa (vya watu wa motoni)



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 37

لَّا يَأۡكُلُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡخَٰطِـُٔونَ

Hawakili chakula hicho isipokuwa wakosefu



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 38

فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَا تُبۡصِرُونَ

Basi Naapa kwa yale mnayoyaona



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 39

وَمَا لَا تُبۡصِرُونَ

Na Naapa kwa yale msiyoyaona



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 40

إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ

Kwa hakika hii (Qur’ani) ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye heshima



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 41

وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَاعِرٖۚ قَلِيلٗا مَّا تُؤۡمِنُونَ

Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayoyaamini



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 42

وَلَا بِقَوۡلِ كَاهِنٖۚ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ

Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 43

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni Uteremsho Kutoka Kwa Mola Wa Viumbe Vyote



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 44

وَلَوۡ تَقَوَّلَ عَلَيۡنَا بَعۡضَ ٱلۡأَقَاوِيلِ

Na Kama (Mtume) Angelizua Juu Yetu Baadhi Ya Maneno tu,



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 45

لَأَخَذۡنَا مِنۡهُ بِٱلۡيَمِينِ

Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 46

ثُمَّ لَقَطَعۡنَا مِنۡهُ ٱلۡوَتِينَ

Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa (wa moyo!)



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 47

فَمَا مِنكُم مِّنۡ أَحَدٍ عَنۡهُ حَٰجِزِينَ

Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 48

وَإِنَّهُۥ لَتَذۡكِرَةٞ لِّلۡمُتَّقِينَ

Kwa hakika hii (Qur’ani) ni ukumbusho kwa wachamungu



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 49

وَإِنَّا لَنَعۡلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ

Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 50

وَإِنَّهُۥ لَحَسۡرَةٌ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na hakika hii (Qur’ani) bila shaka itakuwa ni majuto makubwa juu ya makafiri



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 51

وَإِنَّهُۥ لَحَقُّ ٱلۡيَقِينِ

Na hakika hii (Qur’an) ni haki ya yakini



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 52

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litukuze jina la Mola Wako aliye Mkuu