Surah: AL-QALAM 

Ayah : 31

قَالُواْ يَٰوَيۡلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ

Wakasema: Ole wetu! Hakika sisi tumekuwa warukao mipaka



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 32

عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبۡدِلَنَا خَيۡرٗا مِّنۡهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ

Asaa Mola wetu akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 33

كَذَٰلِكَ ٱلۡعَذَابُۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ

Kama hivyo ndivyo inakuwa adhabu (ya hapa duniani), bila shaka adhabu ya akhera ni kubwa zaidi, laiti wangalijua!



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 34

إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Hakika wachamungu watapata Kwa Mola wao Bustani za neema



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 35

أَفَنَجۡعَلُ ٱلۡمُسۡلِمِينَ كَٱلۡمُجۡرِمِينَ

Je, Tuwafanye Waislamu (watiifu) sawa Kama wahalifu?



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 36

مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ

Mmekuwaaje Nyinyi, Vipi mnahukumu?



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 37

أَمۡ لَكُمۡ كِتَٰبٞ فِيهِ تَدۡرُسُونَ

Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 38

إِنَّ لَكُمۡ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ

Kwamba hakika Yatakuwamo Kwa ajili yenu mnayo yachagua (mnachopendelea)?



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 39

أَمۡ لَكُمۡ أَيۡمَٰنٌ عَلَيۡنَا بَٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ إِنَّ لَكُمۡ لَمَا تَحۡكُمُونَ

Au je, mnavyo viapo juu yetu vinavyofika mpaka siku ya Kiyama ya kuwa ninyi mtapata mnayo yahukumu?



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 40

سَلۡهُمۡ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ

Waulize Hao: Ni nani miongoni mwao mdhamini wa hayo?



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 41

أَمۡ لَهُمۡ شُرَكَآءُ فَلۡيَأۡتُواْ بِشُرَكَآئِهِمۡ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ

Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 42

يَوۡمَ يُكۡشَفُ عَن سَاقٖ وَيُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ

Siku ambayo yatakapokuwa mateso makali, na wataitwa kusujudu lakini hawataweza



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 43

خَٰشِعَةً أَبۡصَٰرُهُمۡ تَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۖ وَقَدۡ كَانُواْ يُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمۡ سَٰلِمُونَ

Macho Yao yatainama chini, udhalilifu utawafunika. Na hali walikuwa wakiitwa wasujudu (kuswali duniani) walipokuwa wazima wa afya



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 44

فَذَرۡنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِۖ سَنَسۡتَدۡرِجُهُم مِّنۡ حَيۡثُ لَا يَعۡلَمُونَ

Basi Niache na anayekadhibisha Maneno haya (Qurani hii) Tutawavuta pole pole adhabuni kwa namna wasiyoijua



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 45

وَأُمۡلِي لَهُمۡۚ إِنَّ كَيۡدِي مَتِينٌ

Na Ninawapa muda, hakika mpango Wangu ni Madhubuti



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 46

أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ

Au unawaomba ujira, na wao wanaelemewa na gharama hiyo?



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 47

أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ

Au wanayo (elimu) ya ghaibu, basi wao wanaandika?



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 48

فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلۡحُوتِ إِذۡ نَادَىٰ وَهُوَ مَكۡظُومٞ

Basi subiri hukumu ya mola wako, wala usiwe kama sahibu wa nyangumi, alipomwita (Mola wake) na hali yeye alikuwa mwenye huzuni nyingi (Amebanwa na Dhiki)



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 49

لَّوۡلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعۡمَةٞ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ مَذۡمُومٞ

Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 50

فَٱجۡتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Lakini mola wake alimchagua na akamfanya kuwa ni miongoni mwa watu wema



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 51

وَإِن يَكَادُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَيُزۡلِقُونَكَ بِأَبۡصَٰرِهِمۡ لَمَّا سَمِعُواْ ٱلذِّكۡرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُۥ لَمَجۡنُونٞ

Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 52

وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ

Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote