Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 31

سَنَفۡرُغُ لَكُمۡ أَيُّهَ ٱلثَّقَلَانِ

Tutakukusudieni kukuhesabuni enyi aina mbili ya viumbe; majini na wanaadamu



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 32

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 33

يَٰمَعۡشَرَ ٱلۡجِنِّ وَٱلۡإِنسِ إِنِ ٱسۡتَطَعۡتُمۡ أَن تَنفُذُواْ مِنۡ أَقۡطَارِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ فَٱنفُذُواْۚ لَا تَنفُذُونَ إِلَّا بِسُلۡطَٰنٖ

Enyi jamii ya Majini na Watu kama mtaweza kupenya kutoka pande za mbinguni na ardhini, basi penyeni hamtoweza kupenya ila kwa nguvu na uwezo. (mamlaka)



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 34

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 35

يُرۡسَلُ عَلَيۡكُمَا شُوَاظٞ مِّن نَّارٖ وَنُحَاسٞ فَلَا تَنتَصِرَانِ

Mtapelekewa muwako wa moto juu yenu na shaba iliyoyeyushwa, basi hamtoweza kujinusuru



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 36

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 37

فَإِذَا ٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ وَرۡدَةٗ كَٱلدِّهَانِ

Zitakapo pasuka mbingu zikawa nyekundu kama mafuta



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 38

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 39

فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُسۡـَٔلُ عَن ذَنۢبِهِۦٓ إِنسٞ وَلَا جَآنّٞ

Basi Siku hiyo hatoulizwa kuhusu dhambi yake Binadamu na wala Jini



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 40

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 41

يُعۡرَفُ ٱلۡمُجۡرِمُونَ بِسِيمَٰهُمۡ فَيُؤۡخَذُ بِٱلنَّوَٰصِي وَٱلۡأَقۡدَامِ

Watatambulikana wahalifu kwa alama zao, basi watachukuliwa kwa nywele za utosi na nyayo



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 42

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 43

هَٰذِهِۦ جَهَنَّمُ ٱلَّتِي يُكَذِّبُ بِهَا ٱلۡمُجۡرِمُونَ

Huu hapa moto wa jahannamu ambao wanaukadhibisha Watu waovu



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 44

يَطُوفُونَ بَيۡنَهَا وَبَيۡنَ حَمِيمٍ ءَانٖ

Wataizunguka baina yake na baina ya maji yachemkayo yaliyo-fikia ukomo wa kutokota



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 45

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 46

وَلِمَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ جَنَّتَانِ

Na kwa mwenye kukhofu kusi-mamishwa mbele ya Mola wake atapata bustani mbili



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 47

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 48

ذَوَاتَآ أَفۡنَانٖ

Zenye miti yenye matawi



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 49

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 50

فِيهِمَا عَيۡنَانِ تَجۡرِيَانِ

Mna humo chemchemu mbili zinazopita



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 51

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 52

فِيهِمَا مِن كُلِّ فَٰكِهَةٖ زَوۡجَانِ

Mna humo kila matunda ya aina mbili mbili



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 53

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 54

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ فُرُشِۭ بَطَآئِنُهَا مِنۡ إِسۡتَبۡرَقٖۚ وَجَنَى ٱلۡجَنَّتَيۡنِ دَانٖ

Hali yakuwa wakiegemea kwenye matandiko mazito yaliyotengenezwa ndani yake kwa hariri nyepesi na matunda ya bustani hizo yapo karibu



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 55

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 56

فِيهِنَّ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ لَمۡ يَطۡمِثۡهُنَّ إِنسٞ قَبۡلَهُمۡ وَلَا جَآنّٞ

Mna humo wanawake wenye staha wanaoinamisha macho, hawajaguswa na Mtu kabla yao wala Jini



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 57

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 58

كَأَنَّهُنَّ ٱلۡيَاقُوتُ وَٱلۡمَرۡجَانُ

Kana kwamba hao wanawake ni yakuti na marijani



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 59

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 60

هَلۡ جَزَآءُ ٱلۡإِحۡسَٰنِ إِلَّا ٱلۡإِحۡسَٰنُ

Haikua malipo ya wema ispokua wema