Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 31

مِن فِرۡعَوۡنَۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَالِيٗا مِّنَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 32

وَلَقَدِ ٱخۡتَرۡنَٰهُمۡ عَلَىٰ عِلۡمٍ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 33

وَءَاتَيۡنَٰهُم مِّنَ ٱلۡأٓيَٰتِ مَا فِيهِ بَلَـٰٓؤٞاْ مُّبِينٌ

Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 34

إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَيَقُولُونَ

Hakika hawa wanasema:



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 35

إِنۡ هِيَ إِلَّا مَوۡتَتُنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُنشَرِينَ

Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 36

فَأۡتُواْ بِـَٔابَآئِنَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 37

أَهُمۡ خَيۡرٌ أَمۡ قَوۡمُ تُبَّعٖ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ أَهۡلَكۡنَٰهُمۡۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ مُجۡرِمِينَ

Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa’ na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 38

وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَا لَٰعِبِينَ

Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 39

مَا خَلَقۡنَٰهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 40

إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ مِيقَٰتُهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 41

يَوۡمَ لَا يُغۡنِي مَوۡلًى عَن مَّوۡلٗى شَيۡـٔٗا وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ

Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 42

إِلَّا مَن رَّحِمَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Isipo kuwa atakaye mrehemu Allah. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 43

إِنَّ شَجَرَتَ ٱلزَّقُّومِ

Hakika Mti wa Zaqqum



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 44

طَعَامُ ٱلۡأَثِيمِ

Ni chakula cha mwenye dhambi



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 45

كَٱلۡمُهۡلِ يَغۡلِي فِي ٱلۡبُطُونِ

Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 46

كَغَلۡيِ ٱلۡحَمِيمِ

Kama kutokota kwa maji ya moto



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 47

خُذُوهُ فَٱعۡتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ

(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 48

ثُمَّ صُبُّواْ فَوۡقَ رَأۡسِهِۦ مِنۡ عَذَابِ ٱلۡحَمِيمِ

Kisha mwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 49

ذُقۡ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡكَرِيمُ

Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 50

إِنَّ هَٰذَا مَا كُنتُم بِهِۦ تَمۡتَرُونَ

Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 51

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٖ

Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 52

فِي جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Katika mabustani na chemchem



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 53

يَلۡبَسُونَ مِن سُندُسٖ وَإِسۡتَبۡرَقٖ مُّتَقَٰبِلِينَ

Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 54

كَذَٰلِكَ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ

Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurulaini



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 55

يَدۡعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَٰكِهَةٍ ءَامِنِينَ

Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 56

لَا يَذُوقُونَ فِيهَا ٱلۡمَوۡتَ إِلَّا ٱلۡمَوۡتَةَ ٱلۡأُولَىٰۖ وَوَقَىٰهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ

Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Allah) atawalinda na adhabu ya Jahannamu



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 57

فَضۡلٗا مِّن رَّبِّكَۚ ذَٰلِكَ هُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 58

فَإِنَّمَا يَسَّرۡنَٰهُ بِلِسَانِكَ لَعَلَّهُمۡ يَتَذَكَّرُونَ

Basi tumeifanya nyepesi hii Qur’ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 59

فَٱرۡتَقِبۡ إِنَّهُم مُّرۡتَقِبُونَ

Ngoja tu, na wao wangoje pia