Surah: SWAAD 

Ayah : 31

إِذۡ عُرِضَ عَلَيۡهِ بِٱلۡعَشِيِّ ٱلصَّـٰفِنَٰتُ ٱلۡجِيَادُ

Alipopelekewa jioni farasi wasimamao kidete, tayari kutoka shoti;



Surah: SWAAD 

Ayah : 32

فَقَالَ إِنِّيٓ أَحۡبَبۡتُ حُبَّ ٱلۡخَيۡرِ عَن ذِكۡرِ رَبِّي حَتَّىٰ تَوَارَتۡ بِٱلۡحِجَابِ

Basi akasema: Navipenda vitu vizuri kwa kumkumbuka Mola wangu Mlezi. Kisha wakafichikana nyuma ya boma



Surah: SWAAD 

Ayah : 33

رُدُّوهَا عَلَيَّۖ فَطَفِقَ مَسۡحَۢا بِٱلسُّوقِ وَٱلۡأَعۡنَاقِ

Nirudishieni! Akaanza kuwa-papasa miguu na shingo



Surah: SWAAD 

Ayah : 34

وَلَقَدۡ فَتَنَّا سُلَيۡمَٰنَ وَأَلۡقَيۡنَا عَلَىٰ كُرۡسِيِّهِۦ جَسَدٗا ثُمَّ أَنَابَ

Na tulimtia mtihanini Suleiman, na tukauweka mwili juu ya kiti chake, kisha akarejea kwa kutubu



Surah: SWAAD 

Ayah : 35

قَالَ رَبِّ ٱغۡفِرۡ لِي وَهَبۡ لِي مُلۡكٗا لَّا يَنۢبَغِي لِأَحَدٖ مِّنۢ بَعۡدِيٓۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡوَهَّابُ

Akasema: Mola wangu Mlezi! Nisamehe na unipe ufalme usio mwelekea (asiupate) yeyote baada yangu. Hakika Wewe ndiye Mpaji



Surah: SWAAD 

Ayah : 36

فَسَخَّرۡنَا لَهُ ٱلرِّيحَ تَجۡرِي بِأَمۡرِهِۦ رُخَآءً حَيۡثُ أَصَابَ

Basi tukaufanya upepo umtumikie, ukaenda kwa amri yake, popote alipo taka kufika



Surah: SWAAD 

Ayah : 37

وَٱلشَّيَٰطِينَ كُلَّ بَنَّآءٖ وَغَوَّاصٖ

Na tukayafanya mashetani yamtumikie, wote wajenzi na wapiga mbizi



Surah: SWAAD 

Ayah : 38

وَءَاخَرِينَ مُقَرَّنِينَ فِي ٱلۡأَصۡفَادِ

Na wengine wafungwao kwa minyororo



Surah: SWAAD 

Ayah : 39

هَٰذَا عَطَآؤُنَا فَٱمۡنُنۡ أَوۡ أَمۡسِكۡ بِغَيۡرِ حِسَابٖ

Hichi ndicho kipawa chetu. Basi toa au zuia, bila ya hesabu



Surah: SWAAD 

Ayah : 40

وَإِنَّ لَهُۥ عِندَنَا لَزُلۡفَىٰ وَحُسۡنَ مَـَٔابٖ

Na hakika yeye kwetu Sisi ana cheo cha kukaribishwa kwetu, na pahala pazuri pa kurejea



Surah: SWAAD 

Ayah : 41

وَٱذۡكُرۡ عَبۡدَنَآ أَيُّوبَ إِذۡ نَادَىٰ رَبَّهُۥٓ أَنِّي مَسَّنِيَ ٱلشَّيۡطَٰنُ بِنُصۡبٖ وَعَذَابٍ

Na mkumbuke mja wetu Ayubu alipo mwita Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika Shetani amenifikishia udhia na adhabu



Surah: SWAAD 

Ayah : 42

ٱرۡكُضۡ بِرِجۡلِكَۖ هَٰذَا مُغۡتَسَلُۢ بَارِدٞ وَشَرَابٞ

(Akaambiwa:) Piga-piga ardhi kwa mguu wako! Basi haya maji baridi ya kuogea na ya kunywa



Surah: SWAAD 

Ayah : 43

وَوَهَبۡنَا لَهُۥٓ أَهۡلَهُۥ وَمِثۡلَهُم مَّعَهُمۡ رَحۡمَةٗ مِّنَّا وَذِكۡرَىٰ لِأُوْلِي ٱلۡأَلۡبَٰبِ

Na tukampa ahali zake na wengine kama wao pamoja nao, kuwa ni rehema itokayo kwetu, na iweukumbusho kwa watu wenye akili



Surah: SWAAD 

Ayah : 44

وَخُذۡ بِيَدِكَ ضِغۡثٗا فَٱضۡرِب بِّهِۦ وَلَا تَحۡنَثۡۗ إِنَّا وَجَدۡنَٰهُ صَابِرٗاۚ نِّعۡمَ ٱلۡعَبۡدُ إِنَّهُۥٓ أَوَّابٞ

Na shika kicha cha vijiti tu mkononi mwako, kisha ndio upigie nacho, wala usivunje kiapo. Hakika tulimkuta ni mwenye subira, mbora wa waja, kwa hakika alikuwa mwingi wa kutubu



Surah: SWAAD 

Ayah : 45

وَٱذۡكُرۡ عِبَٰدَنَآ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ أُوْلِي ٱلۡأَيۡدِي وَٱلۡأَبۡصَٰرِ

Na wakumbuke waja wetu, Ibrahim na Is-haqa na Yaa’qubu waliokuwa na nguvu na busara



Surah: SWAAD 

Ayah : 46

إِنَّآ أَخۡلَصۡنَٰهُم بِخَالِصَةٖ ذِكۡرَى ٱلدَّارِ

Sisi tumewahusisha wao kwa sifa ya ukumbusho wa Akhera



Surah: SWAAD 

Ayah : 47

وَإِنَّهُمۡ عِندَنَا لَمِنَ ٱلۡمُصۡطَفَيۡنَ ٱلۡأَخۡيَارِ

Na hakika wao kwetu sisi ni wateuliwa walio bora



Surah: SWAAD 

Ayah : 48

وَٱذۡكُرۡ إِسۡمَٰعِيلَ وَٱلۡيَسَعَ وَذَا ٱلۡكِفۡلِۖ وَكُلّٞ مِّنَ ٱلۡأَخۡيَارِ

Na mkumbuke Ismail na Alyasaa na Dhulkifli, na wote hao ni katika walio bora



Surah: SWAAD 

Ayah : 49

هَٰذَا ذِكۡرٞۚ وَإِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ لَحُسۡنَ مَـَٔابٖ

Huu ni ukumbusho. Na hakika wacha Mungu wana marejeo mazuri



Surah: SWAAD 

Ayah : 50

جَنَّـٰتِ عَدۡنٖ مُّفَتَّحَةٗ لَّهُمُ ٱلۡأَبۡوَٰبُ

Bustani za milele zitakazo funguliwa milango kwa ajili yao



Surah: SWAAD 

Ayah : 51

مُتَّكِـِٔينَ فِيهَا يَدۡعُونَ فِيهَا بِفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ وَشَرَابٖ

Humo wataegemea masofa mazuri, wawe wanaagiza humo matunda mengi na vinywaji



Surah: SWAAD 

Ayah : 52

۞وَعِندَهُمۡ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ أَتۡرَابٌ

Na pamoja nao wake zao wenye kutuliza macho, hirimu zao



Surah: SWAAD 

Ayah : 53

هَٰذَا مَا تُوعَدُونَ لِيَوۡمِ ٱلۡحِسَابِ

Haya ndiyo mliyo ahidiwa kwa Siku ya Hesabu



Surah: SWAAD 

Ayah : 54

إِنَّ هَٰذَا لَرِزۡقُنَا مَا لَهُۥ مِن نَّفَادٍ

Hakika hii ndiyo riziki yetu isiyo malizika



Surah: SWAAD 

Ayah : 55

هَٰذَاۚ وَإِنَّ لِلطَّـٰغِينَ لَشَرَّ مَـَٔابٖ

Ndiyo hivi! Na hakika wenye kuasi bila ya shaka watapata marejeo mabaya kabisa;



Surah: SWAAD 

Ayah : 56

جَهَنَّمَ يَصۡلَوۡنَهَا فَبِئۡسَ ٱلۡمِهَادُ

Nayo ni Jahannamu! Wataingia humo. Nacho hicho ni kitanda kiovu mno cha kulalia



Surah: SWAAD 

Ayah : 57

هَٰذَا فَلۡيَذُوقُوهُ حَمِيمٞ وَغَسَّاقٞ

Ndio hivi! Basi na wayaonje maji ya moto na ya usaha!



Surah: SWAAD 

Ayah : 58

وَءَاخَرُ مِن شَكۡلِهِۦٓ أَزۡوَٰجٌ

Na adhabu nyenginezo za namna hii



Surah: SWAAD 

Ayah : 59

هَٰذَا فَوۡجٞ مُّقۡتَحِمٞ مَّعَكُمۡ لَا مَرۡحَبَۢا بِهِمۡۚ إِنَّهُمۡ صَالُواْ ٱلنَّارِ

Hili ndilo kundi litakalo ingia pamoja nanyi. Hapana makaribisho mema kwao. Hakika hao wanaingia Motoni



Surah: SWAAD 

Ayah : 60

قَالُواْ بَلۡ أَنتُمۡ لَا مَرۡحَبَۢا بِكُمۡۖ أَنتُمۡ قَدَّمۡتُمُوهُ لَنَاۖ فَبِئۡسَ ٱلۡقَرَارُ

Waseme: Lakini nyinyi! Hamna mapokezi mazuri! Nyinyi ndio mlio tusababishia haya, napo ni pahala pabaya kabisa!