Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 1

ٱلرَّحۡمَٰنُ

(Allah) Mwingi wa rehma



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 2

عَلَّمَ ٱلۡقُرۡءَانَ

Amefundisha Qur’ani



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 3

خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ

Amemumba mwanadamu



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 4

عَلَّمَهُ ٱلۡبَيَانَ

Amemfundisha kusema (yaliyomo moyoni)



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 5

ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ بِحُسۡبَانٖ

Jua na mwezi (vinatembea) kwa hesabu (na mpangilio maalum)



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 6

وَٱلنَّجۡمُ وَٱلشَّجَرُ يَسۡجُدَانِ

Na nyota na miti vinasujudu



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 7

وَٱلسَّمَآءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ ٱلۡمِيزَانَ

Na mbingu ameinyanyua na ameweka mizani (kuthibitisha uadilifu na usawa)



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 8

أَلَّا تَطۡغَوۡاْ فِي ٱلۡمِيزَانِ

(Ameweka mizani) Ili msifanye dhulma katika upimaji



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 9

وَأَقِيمُواْ ٱلۡوَزۡنَ بِٱلۡقِسۡطِ وَلَا تُخۡسِرُواْ ٱلۡمِيزَانَ

Na simamisheni mzani kwa uadilifu na msipunguze mizani



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 10

وَٱلۡأَرۡضَ وَضَعَهَا لِلۡأَنَامِ

Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 11

فِيهَا فَٰكِهَةٞ وَٱلنَّخۡلُ ذَاتُ ٱلۡأَكۡمَامِ

Humo mna matunda na mitende yenye makole



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 12

وَٱلۡحَبُّ ذُو ٱلۡعَصۡفِ وَٱلرَّيۡحَانُ

Na punje (nafaka ) zenye majani (makapi) na harufu nzuri



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 13

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 14

خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِن صَلۡصَٰلٖ كَٱلۡفَخَّارِ

Amemuumba mwanadamu kutokana na udongo utowao sauti kama vyombo vya udongo vilivyochomwa



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 15

وَخَلَقَ ٱلۡجَآنَّ مِن مَّارِجٖ مِّن نَّارٖ

Na Akaumba majini kutokana na ulimi wa moto



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 16

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Molawenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 17

رَبُّ ٱلۡمَشۡرِقَيۡنِ وَرَبُّ ٱلۡمَغۡرِبَيۡنِ

Mola wa Mashariki mbili na Mola wa Magharibi mbili



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 18

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 19

مَرَجَ ٱلۡبَحۡرَيۡنِ يَلۡتَقِيَانِ

Ameziachilia bahari mbili zina-kutana



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 20

بَيۡنَهُمَا بَرۡزَخٞ لَّا يَبۡغِيَانِ

Baina yake kuna kizuizi; hazivu-kiani mipaka



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 21

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 22

يَخۡرُجُ مِنۡهُمَا ٱللُّؤۡلُؤُ وَٱلۡمَرۡجَانُ

Zinatoka humo lulu na marijani



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 23

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 24

وَلَهُ ٱلۡجَوَارِ ٱلۡمُنشَـَٔاتُ فِي ٱلۡبَحۡرِ كَٱلۡأَعۡلَٰمِ

Na ana yeye jahazi zilizoten-genezwa baharini kama milima



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 25

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 26

كُلُّ مَنۡ عَلَيۡهَا فَانٖ

Kila aliyekuwa juu yake (ardhini) ni mwenye kutoweka



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 27

وَيَبۡقَىٰ وَجۡهُ رَبِّكَ ذُو ٱلۡجَلَٰلِ وَٱلۡإِكۡرَامِ

Na atabakia Mwenyewe Mola wako mlezi mwenye utukufu na ukarimu



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 28

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 29

يَسۡـَٔلُهُۥ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ كُلَّ يَوۡمٍ هُوَ فِي شَأۡنٖ

Wanamuomba Yeye kila aliyeku-wepo mbinguni na ardhini, kila siku Yeye Yumo katika kujaalia mambo



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 30

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?