Surah: ANNAJMI 

Ayah : 1

وَٱلنَّجۡمِ إِذَا هَوَىٰ

Nina apa kwa nyota zinapozama



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 2

مَا ضَلَّ صَاحِبُكُمۡ وَمَا غَوَىٰ

Hakupotoka swahibu wenu na wala hakupotoka



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 3

وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلۡهَوَىٰٓ

Na hasemi (neno lolote lile) kwa utashi wa nafsi (yake)



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 4

إِنۡ هُوَ إِلَّا وَحۡيٞ يُوحَىٰ

Hayakuwa hayo (anayaoyasema) isipokuwa tu ni Wahy unaofunuliwa



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 5

عَلَّمَهُۥ شَدِيدُ ٱلۡقُوَىٰ

Amemfundisha (Malaika Jibrili) Mwenye nguvu kubwa



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 6

ذُو مِرَّةٖ فَٱسۡتَوَىٰ

Mwenye nguvu na hekima na akakaa katika umbile lake halisi



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 7

وَهُوَ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Naye yuko juu kabisa katika upeo wa macho



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 8

ثُمَّ دَنَا فَتَدَلَّىٰ

Kisha akakurubia na akashuka



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 9

فَكَانَ قَابَ قَوۡسَيۡنِ أَوۡ أَدۡنَىٰ

Kisha akawa kiasi cha umbali wa mipinde miwili au karibu zaidi



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 10

فَأَوۡحَىٰٓ إِلَىٰ عَبۡدِهِۦ مَآ أَوۡحَىٰ

(Allah) Akamfunulia Wahy mja Wake yale Aliyomfunulia Wahy



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 11

مَا كَذَبَ ٱلۡفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ

Moyo (wake) haukukadhibisha yale aliyoyaona



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 12

أَفَتُمَٰرُونَهُۥ عَلَىٰ مَا يَرَىٰ

Je, mnambishia kuhusu yale aliyoyaona?



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 13

وَلَقَدۡ رَءَاهُ نَزۡلَةً أُخۡرَىٰ

Na hakika alimuona (Jibriyl) kwa mara nyingine



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 14

عِندَ سِدۡرَةِ ٱلۡمُنتَهَىٰ

Kwenye mkunazi wa mpaka wa mwisho kabisa



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 15

عِندَهَا جَنَّةُ ٱلۡمَأۡوَىٰٓ

Karibu yake kuna Jannatu Al-Ma-waa



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 16

إِذۡ يَغۡشَى ٱلسِّدۡرَةَ مَا يَغۡشَىٰ

Ulipoufunika mkunazi huo hicho kilicho ufinika



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 17

مَا زَاغَ ٱلۡبَصَرُ وَمَا طَغَىٰ

Jicho lake halikukengeuka wala halikupindukia mipaka



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 18

لَقَدۡ رَأَىٰ مِنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ

Kwa yakini aliona miongoni mwa Aayaat (ishara, dalili) za Bwana wake kubwa kabisa



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 19

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱللَّـٰتَ وَٱلۡعُزَّىٰ

Je, mmeona (masanamu) Laata na ‘Uzzaa?



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 20

وَمَنَوٰةَ ٱلثَّالِثَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰٓ

Na Manaata mwengine wa tatu?



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 21

أَلَكُمُ ٱلذَّكَرُ وَلَهُ ٱلۡأُنثَىٰ

Je, nyinyi mna wana wa kiume Naye Ana wana wa kike?



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 22

تِلۡكَ إِذٗا قِسۡمَةٞ ضِيزَىٰٓ

Huo basi ni mgao wa dhulma!



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 23

إِنۡ هِيَ إِلَّآ أَسۡمَآءٞ سَمَّيۡتُمُوهَآ أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُم مَّآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بِهَا مِن سُلۡطَٰنٍۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَمَا تَهۡوَى ٱلۡأَنفُسُۖ وَلَقَدۡ جَآءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ ٱلۡهُدَىٰٓ

Hayo si chochote isipokuwa ni majina mmeyaita nyinyi na baba zenu, wala Allah Hakuyateremshia dalili yoyote. Hawafuati isipokuwa dhana na yale yanayotamani nafsi (zao), na hali imekwishawajia kutoka kwa Bwana wao mwongozo



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 24

أَمۡ لِلۡإِنسَٰنِ مَا تَمَنَّىٰ

Kwani kila Mtu anapata kila anayoyatamani?



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 25

فَلِلَّهِ ٱلۡأٓخِرَةُ وَٱلۡأُولَىٰ

Na Allah ndiye mmiliki wa Akhera na Dunia



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 26

۞وَكَم مِّن مَّلَكٖ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ لَا تُغۡنِي شَفَٰعَتُهُمۡ شَيۡـًٔا إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ أَن يَأۡذَنَ ٱللَّهُ لِمَن يَشَآءُ وَيَرۡضَىٰٓ

Na kuna malaika wengi mbinguni hainufaishi chochote uombezi wao ila baada ya kupewa idhini na Allah kwa amtakaye na amridhie



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 27

إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ لَيُسَمُّونَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ تَسۡمِيَةَ ٱلۡأُنثَىٰ

Hakika wale wasioamini Aakhirah bila shaka wanawaita Malaika kwa majina ya kike



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 28

وَمَا لَهُم بِهِۦ مِنۡ عِلۡمٍۖ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّۖ وَإِنَّ ٱلظَّنَّ لَا يُغۡنِي مِنَ ٱلۡحَقِّ شَيۡـٔٗا

Na wala hawana ujuzi wowote ule wa hayo; hawafuati isipokuwa dhana, na hakika dhana haifai kitu chochote mbele ya haki



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 29

فَأَعۡرِضۡ عَن مَّن تَوَلَّىٰ عَن ذِكۡرِنَا وَلَمۡ يُرِدۡ إِلَّا ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Basi achana naye ambaye ameupa mgongo ukumbusho Wetu na wala hataki isipokuwa maisha ya dunia



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 30

ذَٰلِكَ مَبۡلَغُهُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱهۡتَدَىٰ

Huo ndio upeo wao wa elimu. Hakika Bwana wako ni Mjuzi zaidi wa ambaye amepotoka njia Yake, Naye Mjuzi zaidi wa ambaye ameongoka