Surah: IBRAHIM 

Ayah : 1

الٓرۚ كِتَٰبٌ أَنزَلۡنَٰهُ إِلَيۡكَ لِتُخۡرِجَ ٱلنَّاسَ مِنَ ٱلظُّلُمَٰتِ إِلَى ٱلنُّورِ بِإِذۡنِ رَبِّهِمۡ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ

Alif Lam Raa[1]. Hiki ni Kitabu tulichokiteremsha kwako ili kwacho uwatowe watu kwenye giza uwapeleke kwenye muangaza, kwa idhini ya Mola wao Mlezi, uwafikishe kwenye Njia ya Mwenye nguvu, Msifiwa


1- - Allah ndiye ajuaye maana halisi ya herufi hizi.


Surah: IBRAHIM 

Ayah : 2

ٱللَّهِ ٱلَّذِي لَهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۗ وَوَيۡلٞ لِّلۡكَٰفِرِينَ مِنۡ عَذَابٖ شَدِيدٍ

Allah ambaye ni vyake yeye tu vyote vilivyomo mbinguni na ardhini. Na ole wao makafiri kwa adhabu kali mno



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 3

ٱلَّذِينَ يَسۡتَحِبُّونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا عَلَى ٱلۡأٓخِرَةِ وَيَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ وَيَبۡغُونَهَا عِوَجًاۚ أُوْلَـٰٓئِكَ فِي ضَلَٰلِۭ بَعِيدٖ

Ambao wanafadhilisha maisha ya dunia kuliko Akhera, na wanazuia (watu wasifuate) Njia ya Allah, na wanataka kuipotosha. Hao wapo kwenye upotevu wa mbali



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 4

وَمَآ أَرۡسَلۡنَا مِن رَّسُولٍ إِلَّا بِلِسَانِ قَوۡمِهِۦ لِيُبَيِّنَ لَهُمۡۖ فَيُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Na hatukumtuma Mtume yoyote ila kwa lugha ya kaumu yake ili apate kuwabainishia. Basi Allah humuacha akapotea amtakaye, na akamuongoa amtakaye. Naye ni Mtukufu Mwenye nguvu na Mwenye hekima



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 5

وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا مُوسَىٰ بِـَٔايَٰتِنَآ أَنۡ أَخۡرِجۡ قَوۡمَكَ مِنَ ٱلظُّلُمَٰتِ إِلَى ٱلنُّورِ وَذَكِّرۡهُم بِأَيَّىٰمِ ٱللَّهِۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّكُلِّ صَبَّارٖ شَكُورٖ

Na kwa hakika kabisa tulimtuma Mussa pamoja na miujiza yetu, (na tulimwambia): Watoe watu wako kwenye giza uwapeleke kwenye mwangaza. Na uwakumbushe siku za Allah. Hakika katika hayo zipo ishara kwa kila mwenye kusubiri (na) kushukuru



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 6

وَإِذۡ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوۡمِهِ ٱذۡكُرُواْ نِعۡمَةَ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡ إِذۡ أَنجَىٰكُم مِّنۡ ءَالِ فِرۡعَوۡنَ يَسُومُونَكُمۡ سُوٓءَ ٱلۡعَذَابِ وَيُذَبِّحُونَ أَبۡنَآءَكُمۡ وَيَسۡتَحۡيُونَ نِسَآءَكُمۡۚ وَفِي ذَٰلِكُم بَلَآءٞ مِّن رَّبِّكُمۡ عَظِيمٞ

Na (kumbuka) Mussa alipo-waambia watu wake: Kumbukeni neema ya Allah aliyokujaalieni, pale alipokuokoeni kutokana na watu wa Firauni waliokupeni adhabu mbaya kabisa, wakiwachinja watoto wenu wanaume, na wakiwaacha hai wanawake. Na katika hayo ulikuwa mtihani mkubwa unaotoka kwa Mola wenu Mlezi



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 7

وَإِذۡ تَأَذَّنَ رَبُّكُمۡ لَئِن شَكَرۡتُمۡ لَأَزِيدَنَّكُمۡۖ وَلَئِن كَفَرۡتُمۡ إِنَّ عَذَابِي لَشَدِيدٞ

Na alipotangaza Mola wenu Mlezi (kwamba): iwapo mtani-shukuru nitakuzidishieni; na iwapo mtanikufuru, basi adhabu yangu ni kali mno



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 8

وَقَالَ مُوسَىٰٓ إِن تَكۡفُرُوٓاْ أَنتُمۡ وَمَن فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا فَإِنَّ ٱللَّهَ لَغَنِيٌّ حَمِيدٌ

Na Mussa alisema: Iwapo nyinyi mtakufuru na wote waliomo duniani, hakika Allah ni Mkwasi mno, Msifiwa



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 9

أَلَمۡ يَأۡتِكُمۡ نَبَؤُاْ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِكُمۡ قَوۡمِ نُوحٖ وَعَادٖ وَثَمُودَ وَٱلَّذِينَ مِنۢ بَعۡدِهِمۡ لَا يَعۡلَمُهُمۡ إِلَّا ٱللَّهُۚ جَآءَتۡهُمۡ رُسُلُهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِ فَرَدُّوٓاْ أَيۡدِيَهُمۡ فِيٓ أَفۡوَٰهِهِمۡ وَقَالُوٓاْ إِنَّا كَفَرۡنَا بِمَآ أُرۡسِلۡتُم بِهِۦ وَإِنَّا لَفِي شَكّٖ مِّمَّا تَدۡعُونَنَآ إِلَيۡهِ مُرِيبٖ

Je, hazikukufikieni habari za baadhi ya waliokuwa kabla yenu? Kaumu ya Nuhu, na A’adi, na Thamud, na waliofuata baada yao, ambao hapana awajuaye ila Allah? Mitume wao waliwajia kwa hoja zilizo wazi, na wao wakarudisha mikono yao kwenye vinywa vyao, wakasema: Hakika sisi hatuyataki hayo mliyotumwa kwayo, na hakika sisi tuna shaka kubwa na mnayotuitia



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 10

۞قَالَتۡ رُسُلُهُمۡ أَفِي ٱللَّهِ شَكّٞ فَاطِرِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ يَدۡعُوكُمۡ لِيَغۡفِرَ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمۡ وَيُؤَخِّرَكُمۡ إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمّٗىۚ قَالُوٓاْ إِنۡ أَنتُمۡ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا تُرِيدُونَ أَن تَصُدُّونَا عَمَّا كَانَ يَعۡبُدُ ءَابَآؤُنَا فَأۡتُونَا بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٖ

Mitume wao walisema: Je, kuna shaka na Allah, Muumba mbingu na ardhi? Yeye anakuiteni ili apate kukufutieni madhambi yenu, na akupeni muhula (wa adhabu angamizi) mpaka muda uliowekwa (ufike). Walisema: Nyinyi si chochote ila ni wanadamu tu kama sisi. Mnataka kutuzuia na waliyokuwa wanayaabudu Baba zetu. Basi tuleteeni hoja ilio wazi



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 11

قَالَتۡ لَهُمۡ رُسُلُهُمۡ إِن نَّحۡنُ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُكُمۡ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ يَمُنُّ عَلَىٰ مَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦۖ وَمَا كَانَ لَنَآ أَن نَّأۡتِيَكُم بِسُلۡطَٰنٍ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۚ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ

Mitume wao waliwaambia: Sisi kweli si chochote (kimaumbo) ila ni wanadamu kama nyinyi. Lakini Allah humfanyia hisani amtakaye katika waja wake. Wala sisi hatuwezi kuleta uthibitisho ila kwa idhini ya Allah. Na kwa Allah tu ndio wategemee Waumini



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 12

وَمَا لَنَآ أَلَّا نَتَوَكَّلَ عَلَى ٱللَّهِ وَقَدۡ هَدَىٰنَا سُبُلَنَاۚ وَلَنَصۡبِرَنَّ عَلَىٰ مَآ ءَاذَيۡتُمُونَاۚ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُتَوَكِّلُونَ

Na wala hatuna udhuru (wa kwa) nini tusimtegemee Allah, na hali Yeye ametuongoa kwenye Njia zetu. Na hapana shaka sisi tutavumilia hizo kero mlizotuudhi kwazo. Na kwa Allah tu wategemee wanaotegemea



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 13

وَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لِرُسُلِهِمۡ لَنُخۡرِجَنَّكُم مِّنۡ أَرۡضِنَآ أَوۡ لَتَعُودُنَّ فِي مِلَّتِنَاۖ فَأَوۡحَىٰٓ إِلَيۡهِمۡ رَبُّهُمۡ لَنُهۡلِكَنَّ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na walisema waliokufuru (kuwaambia) Mitume wao: Tutakutoeni mkuku katika nchi yetu, au mrudi katika dini yetu. Basi Mola wao Mlezi aliwaletea wahyi: Hakika tutawaangamiza madhalimu



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 14

وَلَنُسۡكِنَنَّكُمُ ٱلۡأَرۡضَ مِنۢ بَعۡدِهِمۡۚ ذَٰلِكَ لِمَنۡ خَافَ مَقَامِي وَخَافَ وَعِيدِ

Na tutakuwekeni katika ardhi baada yao. Haya ni kwa anayeogopa kusimamishwa mbele yangu, na akaogopa maonyo yangu (ya adhabu)



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 15

وَٱسۡتَفۡتَحُواْ وَخَابَ كُلُّ جَبَّارٍ عَنِيدٖ

Na (Mitume) waliomba nusra (kwa Allah dhidi ya mahasimu wao), na alishindwa kila jabari mkaidi



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 16

مِّن وَرَآئِهِۦ جَهَنَّمُ وَيُسۡقَىٰ مِن مَّآءٖ صَدِيدٖ

(Kila mkaidi ajue) Usoni (mbele) yake ipo Jahanamu (inamngoja), na atanyweshwa maji ya usaha (na damu itiririkayo kutoka kwenye mili ya watu wa Motoni)



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 17

يَتَجَرَّعُهُۥ وَلَا يَكَادُ يُسِيغُهُۥ وَيَأۡتِيهِ ٱلۡمَوۡتُ مِن كُلِّ مَكَانٖ وَمَا هُوَ بِمَيِّتٖۖ وَمِن وَرَآئِهِۦ عَذَابٌ غَلِيظٞ

Ataugugumia usaha (na damu ili akate kiu), wala hawezi kuumeza (kutokana na kinyaa na kuunguza kwake). Na (sababu za) mauti zitamjia kutoka kila upande (wa kiungo, lakini), wala hafi. Na zaidi ya hayo ipo adhabu nyingine kali zaidi



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 18

مَّثَلُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِرَبِّهِمۡۖ أَعۡمَٰلُهُمۡ كَرَمَادٍ ٱشۡتَدَّتۡ بِهِ ٱلرِّيحُ فِي يَوۡمٍ عَاصِفٖۖ لَّا يَقۡدِرُونَ مِمَّا كَسَبُواْ عَلَىٰ شَيۡءٖۚ ذَٰلِكَ هُوَ ٱلضَّلَٰلُ ٱلۡبَعِيدُ

Mfano (wa kutisha wa) waliomkufuru Mola wao Mlezi, vitendo vyao (vyema ikiwemo kuunga udugu n.k Siku ya Kiyama havitawafaa) ni kama jivu linalopeperushwa kwa nguvu za upepo katika siku ya dhoruba. Hawawezi kupata chochote katika waliyoyachuma. Huo ndio upotevu wa mbali



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 19

أَلَمۡ تَرَ أَنَّ ٱللَّهَ خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّۚ إِن يَشَأۡ يُذۡهِبۡكُمۡ وَيَأۡتِ بِخَلۡقٖ جَدِيدٖ

(Ewe unaeambiwa habari hii) Hivi uoni kuwa Allah ameziumba mbingu na ardhi kwa Haki? Akitaka atakuondoeni na ataleta viumbe wapya kabisa (watiifu zaidi kuliko nyinyi)



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 20

وَمَا ذَٰلِكَ عَلَى ٱللَّهِ بِعَزِيزٖ

Na hilo (la kuwaondoeni na kuleta viumbe wapya) kwa Allah si jambo gumu



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 21

وَبَرَزُواْ لِلَّهِ جَمِيعٗا فَقَالَ ٱلضُّعَفَـٰٓؤُاْ لِلَّذِينَ ٱسۡتَكۡبَرُوٓاْ إِنَّا كُنَّا لَكُمۡ تَبَعٗا فَهَلۡ أَنتُم مُّغۡنُونَ عَنَّا مِنۡ عَذَابِ ٱللَّهِ مِن شَيۡءٖۚ قَالُواْ لَوۡ هَدَىٰنَا ٱللَّهُ لَهَدَيۡنَٰكُمۡۖ سَوَآءٌ عَلَيۡنَآ أَجَزِعۡنَآ أَمۡ صَبَرۡنَا مَا لَنَا مِن مَّحِيصٖ

Na (viumbe) wote watatoka (makaburini na) kuhudhuria mbele ya Allah. Basi (wale wafuasi waliokuwa wanafuata mkumbo) wanyonge watawaambia (wakubwa wao) waliotakabari: Sisi tulikuwa wafuasi wenu; basi hamuwezi kutuondolea adhabu ya Allah japo kidogo? Watasema: Lau Allah angelituongoa (tukawa waumini) basi hapana shaka nasi tungelikuongoeni. Ni mamoja kwetu (kama) tutapapatika au tutasubiri; hatuna pa kukimbilia



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 22

وَقَالَ ٱلشَّيۡطَٰنُ لَمَّا قُضِيَ ٱلۡأَمۡرُ إِنَّ ٱللَّهَ وَعَدَكُمۡ وَعۡدَ ٱلۡحَقِّ وَوَعَدتُّكُمۡ فَأَخۡلَفۡتُكُمۡۖ وَمَا كَانَ لِيَ عَلَيۡكُم مِّن سُلۡطَٰنٍ إِلَّآ أَن دَعَوۡتُكُمۡ فَٱسۡتَجَبۡتُمۡ لِيۖ فَلَا تَلُومُونِي وَلُومُوٓاْ أَنفُسَكُمۖ مَّآ أَنَا۠ بِمُصۡرِخِكُمۡ وَمَآ أَنتُم بِمُصۡرِخِيَّ إِنِّي كَفَرۡتُ بِمَآ أَشۡرَكۡتُمُونِ مِن قَبۡلُۗ إِنَّ ٱلظَّـٰلِمِينَ لَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Na Shetani atawaambia wafuasi (wake huko Akhera) mara itapokatwa hukumu (na watu wa Peponi kuingia Peponi na wa Motoni kuingia Motoni): Hakika Allah alikuahidini ahadi ya kweli. Nami nilikuahidini (uongo); lakini sikukutimizieni. Na sikuwa na mamlaka juu yenu, isipokuwa nilikuiteni (katika ukafiri na maasi), nanyi mkaniitikia. Basi msinilaumu mimi, bali jilaumuni wenyewe. Mimi siwezi kuwa msaidizi wenu, wala nyinyi hamuwezi kuwa wasaidizi wangu. Hakika mimi nilikataa tangu zamani kunishirikisha na Allah. Hakika madhalimu watakuwa na adhabu chungu mno



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 23

وَأُدۡخِلَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَا بِإِذۡنِ رَبِّهِمۡۖ تَحِيَّتُهُمۡ فِيهَا سَلَٰمٌ

Na (Allah) atawaingiza walioamini na waliotenda mema katika Pepo ipitayo mito mbele yake, watadumu humo kwa idhini ya Mola wao Mlezi. Maamkizi yao humo (kutoka kwa Allah na Malaika) yatakuwa: Salaam[1]


1- - Rejea Sura ArRa’d 13: 24 “Amani iwe kwenu, kwa sababu mlisubiri, basi ni mema yaliyoje matokeo ya
nyumba ya Akhera


Surah: IBRAHIM 

Ayah : 24

أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ ضَرَبَ ٱللَّهُ مَثَلٗا كَلِمَةٗ طَيِّبَةٗ كَشَجَرَةٖ طَيِّبَةٍ أَصۡلُهَا ثَابِتٞ وَفَرۡعُهَا فِي ٱلسَّمَآءِ

(Ewe unayeambiwa) Kwani hukuona vipi Allah alivyopiga mfano wa neno zuri (ambapo amelilinganisha neno Lailaha illa LLah)? Ni kama mti mzuri, mizizi yake ni imara, na matawi yake (yamechanua) kuelekea mbinguni



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 25

تُؤۡتِيٓ أُكُلَهَا كُلَّ حِينِۭ بِإِذۡنِ رَبِّهَاۗ وَيَضۡرِبُ ٱللَّهُ ٱلۡأَمۡثَالَ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمۡ يَتَذَكَّرُونَ

Hutoa matunda yake kila wakati kwa idhini ya Mola wake Mlezi. Na Allah huwapigia watu mifano ili wapate kukumbuka



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 26

وَمَثَلُ كَلِمَةٍ خَبِيثَةٖ كَشَجَرَةٍ خَبِيثَةٍ ٱجۡتُثَّتۡ مِن فَوۡقِ ٱلۡأَرۡضِ مَا لَهَا مِن قَرَارٖ

Na mfano wa neno ovu (neno la ukafiri) ni kama mti muovu, uliong’olewa juu ya ardhi. Hauna uimara



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 27

يُثَبِّتُ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ بِٱلۡقَوۡلِ ٱلثَّابِتِ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَفِي ٱلۡأٓخِرَةِۖ وَيُضِلُّ ٱللَّهُ ٱلظَّـٰلِمِينَۚ وَيَفۡعَلُ ٱللَّهُ مَا يَشَآءُ

Allah anawathibitisha wale walioamini kwa kauli thabiti[1] katika maisha ya dunia (kaburini)[2] na katika Akhera. Na Allah huwapoteza madhalimu. Na Allah anafanya analolitaka


1- - Neno madhubuti na imara ni Lailaha illa llah na kila neno la haki na kweli


2- - Wakati watakapokuwa wanaulizwa na Malaika wawili kuhusu Mola wao, Dini yao na Mtume wao?


Surah: IBRAHIM 

Ayah : 28

۞أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِينَ بَدَّلُواْ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ كُفۡرٗا وَأَحَلُّواْ قَوۡمَهُمۡ دَارَ ٱلۡبَوَارِ

Kwani hukuwaona wale (maka-firi) waliobadilisha neema za Allah kuwa kufuru, na wakawafikisha watu wao kwenye nyumba ya maangamivu?



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 29

جَهَنَّمَ يَصۡلَوۡنَهَاۖ وَبِئۡسَ ٱلۡقَرَارُ

(Nao wataingia) Jahanamu, maovu yaliyoje makazi hayo!?



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 30

وَجَعَلُواْ لِلَّهِ أَندَادٗا لِّيُضِلُّواْ عَن سَبِيلِهِۦۗ قُلۡ تَمَتَّعُواْ فَإِنَّ مَصِيرَكُمۡ إِلَى ٱلنَّارِ

Na walimfanyia Allah washirika ili wapoteze watu kwenye Njia yake. Sema: Stareheni, kwani marejeo yenu ni Motoni