Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 8

إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ

Hakika Yeye ana uwezo wa kumrudisha



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 7

إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلۡجَهۡرَ وَمَا يَخۡفَىٰ

Ila akipenda Allah. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana



Surah: ADH-DHUHAA 

Ayah : 11

وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ

Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie



Surah: AL-A’LAQ 

Ayah : 14

أَلَمۡ يَعۡلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ

Hajui ya kwamba Allah anaona?



Surah: AL-BAYYINAH 

Ayah : 5

وَمَآ أُمِرُوٓاْ إِلَّا لِيَعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَ حُنَفَآءَ وَيُقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَيُؤۡتُواْ ٱلزَّكَوٰةَۚ وَذَٰلِكَ دِينُ ٱلۡقَيِّمَةِ

Nao hawakuamrishwa kitu isipokuwa wamuabudu Allah kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu, na washike Sala, na watoe Zaka. Na hiyo ndiyo Dini madhubuti



Surah: ANASRI 

Ayah : 3

فَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ وَٱسۡتَغۡفِرۡهُۚ إِنَّهُۥ كَانَ تَوَّابَۢا

Basi zitakase sifa za Mola wako Mlezi na muombe msamaha. Hakika, Yeye (Allah) amekuwa Mwenye kukubali sana toba. Sura imetoa utabiri wa kifo cha Mtume rehma na amani ziwe juu yake



Surah: AL-IKHLAAS 

Ayah : 1

قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ

Sema: Yeye Allah ni wa pekee



Surah: AL-IKHLAAS 

Ayah : 2

ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ

Allah ndiye tu Mkusudiwa (katika kuabudiwa, kutegemewa na kutatua shida za watu)



Surah: AL-IKHLAAS 

Ayah : 3

لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ

Hakuzaa[1] na hakuzaliwa.[2]


1- - Kwa maana hiyo hana mtoto.


2- - Kwa maana hiyo hana baba wala mama.

---------------

------------------------------------------------------------

---------------

------------------------------------------------------------


Surah: AL-IKHLAAS 

Ayah : 4

وَلَمۡ يَكُن لَّهُۥ كُفُوًا أَحَدُۢ

Na hakuna yeyote anaye fanana naye



Surah: ANNAAS

Ayah : 2

مَلِكِ ٱلنَّاسِ

Mfalme wa watu