Surah: AN-FAL 

Ayah : 45

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا لَقِيتُمۡ فِئَةٗ فَٱثۡبُتُواْ وَٱذۡكُرُواْ ٱللَّهَ كَثِيرٗا لَّعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ

Enyi mlioamini, mkikutana na jeshi (la makafiri), basi kuweni thabiti (kuweni imara na msikimbie), na mtajeni sana Allah (muombeni) ili mpate kufanikiwa



Surah: AN-FAL 

Ayah : 46

وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَلَا تَنَٰزَعُواْ فَتَفۡشَلُواْ وَتَذۡهَبَ رِيحُكُمۡۖ وَٱصۡبِرُوٓاْۚ إِنَّ ٱللَّهَ مَعَ ٱلصَّـٰبِرِينَ

Na mtiini Allah na Mtume wake, wala msizozane mtasambaratika (na woga utakutawaleni) na nguvu zenu zitatoweka. Na vumilieni. Hakika Allah yupo pamoja na wavumilivu



Surah: AN-FAL 

Ayah : 55

إِنَّ شَرَّ ٱلدَّوَآبِّ عِندَ ٱللَّهِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Hakika viumbe waovu mno mbele ya Allah ni wale waliokufuru, kwasababu hawaamini (upekee wa Allah na uweza wake)



Surah: AN-FAL 

Ayah : 56

ٱلَّذِينَ عَٰهَدتَّ مِنۡهُمۡ ثُمَّ يَنقُضُونَ عَهۡدَهُمۡ فِي كُلِّ مَرَّةٖ وَهُمۡ لَا يَتَّقُونَ

Ambao miongoni mwao umeingia[1] nao maafikiano (mikataba) kwamba wasiwasaidie makafiri), kisha wanavunja maafikiano yao kila mara, na hawaogopi (wala hawajali)


1- - Wayahudi wa kabila la Quraidha


Surah: AN-FAL 

Ayah : 57

فَإِمَّا تَثۡقَفَنَّهُمۡ فِي ٱلۡحَرۡبِ فَشَرِّدۡ بِهِم مَّنۡ خَلۡفَهُمۡ لَعَلَّهُمۡ يَذَّكَّرُونَ

Basi ukiwakuta vitani wafurushe (kisawa sawa ili uwaogopeshe (makafiri wengine) walioko nyuma yao ili wapate kukumbuka (wasithubutu tena kukuchezea na kuuchezea Uislamu)



Surah: AN-FAL 

Ayah : 60

وَأَعِدُّواْ لَهُم مَّا ٱسۡتَطَعۡتُم مِّن قُوَّةٖ وَمِن رِّبَاطِ ٱلۡخَيۡلِ تُرۡهِبُونَ بِهِۦ عَدُوَّ ٱللَّهِ وَعَدُوَّكُمۡ وَءَاخَرِينَ مِن دُونِهِمۡ لَا تَعۡلَمُونَهُمُ ٱللَّهُ يَعۡلَمُهُمۡۚ وَمَا تُنفِقُواْ مِن شَيۡءٖ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ يُوَفَّ إِلَيۡكُمۡ وَأَنتُمۡ لَا تُظۡلَمُونَ

Na (Enyi Waislamu) waandalieni (maadui zenu) nguvu yoyote muiwezayo, na kwa farasi walioandaliwa (kwa Jihadi) ili kwa maandalizi hayo muwatishe maadui wa Allah na maadui zenu na (maadui) wengine tofauti na hao ambao nyinyi hamuwajui, (lakini) Allah anawajua. Na chochote mnachokitoa katika njia ya Allah kitalipwa kwa ukamilifu nanyi hamtadhulumiwa



Surah: AN-FAL 

Ayah : 61

۞وَإِن جَنَحُواْ لِلسَّلۡمِ فَٱجۡنَحۡ لَهَا وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Na (makafiri) wakielekea kutaka amani (na suluhu), basi na wewe elekea kwenye amani (na suluhu) hiyo na mtegemee Allah. Hakika, yeye (Allah) ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kujua



Surah: AN-FAL 

Ayah : 62

وَإِن يُرِيدُوٓاْ أَن يَخۡدَعُوكَ فَإِنَّ حَسۡبَكَ ٱللَّهُۚ هُوَ ٱلَّذِيٓ أَيَّدَكَ بِنَصۡرِهِۦ وَبِٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Na (makafiri) wakitaka kukuhadaa (kwenye suluhu na amani) basi Allah anakutosha (dhidi ya hila na khiyana zao). Yeye (Allah) ndiye aliyekupa nguvu kwa nusra yake na kwa waumini



Surah: AN-FAL 

Ayah : 74

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَهَاجَرُواْ وَجَٰهَدُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَٱلَّذِينَ ءَاوَواْ وَّنَصَرُوٓاْ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ حَقّٗاۚ لَّهُم مَّغۡفِرَةٞ وَرِزۡقٞ كَرِيمٞ

Na walioamini na wakahama (kwa ajili ya usalama wa imani zao) na wakapigana Jihadi katika njia ya Allah, na waliotoa mahali pa kuishi (hifadhi) na wakatoa misaada (mbali mbali), hao ndio Waumini wa kweli. Watapata msamaha na riziki nzuri



Surah: AN-FAL 

Ayah : 75

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنۢ بَعۡدُ وَهَاجَرُواْ وَجَٰهَدُواْ مَعَكُمۡ فَأُوْلَـٰٓئِكَ مِنكُمۡۚ وَأُوْلُواْ ٱلۡأَرۡحَامِ بَعۡضُهُمۡ أَوۡلَىٰ بِبَعۡضٖ فِي كِتَٰبِ ٱللَّهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمُۢ

Na walioamini baada ya hapo (baada ya suluhu ya Hudaibiya) na wakahama na wakapigana Jihadi pamoja nanyi, basi hao ni katika nyinyi (kiulinzi na nusra). Na ndugu wa nasaba wanastahikiana zaidi wenyewe kwa wenyewe (katika kurithiana) katika kitabu cha Allah (kuliko kurithiana kwasababu ya Hijira). Hakika, Allah ni Mwenye kukijua kila kitu



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 5

فَإِذَا ٱنسَلَخَ ٱلۡأَشۡهُرُ ٱلۡحُرُمُ فَٱقۡتُلُواْ ٱلۡمُشۡرِكِينَ حَيۡثُ وَجَدتُّمُوهُمۡ وَخُذُوهُمۡ وَٱحۡصُرُوهُمۡ وَٱقۡعُدُواْ لَهُمۡ كُلَّ مَرۡصَدٖۚ فَإِن تَابُواْ وَأَقَامُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتَوُاْ ٱلزَّكَوٰةَ فَخَلُّواْ سَبِيلَهُمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Basi inapokwisha Miezi (minne) Mitukufu (ambayo mliwapa amani makafiri) basi (tengueni ahadi na) waueni washirikina popote mnapowakuta, na washikeni (watieni mbaroni) na wazingireni, na wakalieni (wadhibitini) katika kila njia (kila kona). Basi iwapo watatubu (wataacha ukafiri) nawakasimamisha Swala na wakatoa Zaka, basi waachieni (kwakuwa wameshakuwa ndugu zenu katika imani). Hakika Allah ni Mwenye kusamehe mno, Mwenye kurehemu



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 6

وَإِنۡ أَحَدٞ مِّنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ ٱسۡتَجَارَكَ فَأَجِرۡهُ حَتَّىٰ يَسۡمَعَ كَلَٰمَ ٱللَّهِ ثُمَّ أَبۡلِغۡهُ مَأۡمَنَهُۥۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ قَوۡمٞ لَّا يَعۡلَمُونَ

Na iwapo yeyote katika washirikina (makafiri) wakikuomba ujirani (na ulinzi na amani kwenye himaya yako), basi mpe ujirani (ukae naye) ili apate kuyasikia maneno ya Allah. Kisha mfikishe mahali pake pa amani (sehemu atakayokuwa salama). Hiyo ni kwa kuwa hao ni watu wasiojua (Uislamu)



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 12

وَإِن نَّكَثُوٓاْ أَيۡمَٰنَهُم مِّنۢ بَعۡدِ عَهۡدِهِمۡ وَطَعَنُواْ فِي دِينِكُمۡ فَقَٰتِلُوٓاْ أَئِمَّةَ ٱلۡكُفۡرِ إِنَّهُمۡ لَآ أَيۡمَٰنَ لَهُمۡ لَعَلَّهُمۡ يَنتَهُونَ

Na iwapo Makafiri) watavunja viapo vyao baada ya ahadi zao, na wakaitukana Dini yenu, basi waueni viongozi wa ukafiri. Hakika, hao hawana muamana (hawaheshimu viapo vyao). (Washirikina wakiona wanauawa au wanapigwa) huenda wakaacha[1]


1- - Aya hizi za 11 na 12 zinawahiyarisha washirikishaji mambo mawili; ima watubu au waingie vitani.


Surah: ATTAUBA 

Ayah : 13

أَلَا تُقَٰتِلُونَ قَوۡمٗا نَّكَثُوٓاْ أَيۡمَٰنَهُمۡ وَهَمُّواْ بِإِخۡرَاجِ ٱلرَّسُولِ وَهُم بَدَءُوكُمۡ أَوَّلَ مَرَّةٍۚ أَتَخۡشَوۡنَهُمۡۚ فَٱللَّهُ أَحَقُّ أَن تَخۡشَوۡهُ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

Hivi kwa nini hampigani na watu waliokiuka viapo vyao na kudhamiria kumfukuza Mtume, na hao ndio waliokuanzeni (kukuchozeni) mara ya kwanza?[1] Je, mnawaogopa? Basi Allah anastahiki zaidi kuogopwa, ikiwa nyinyi ni Waumini (wa kweli)


1- - Allah katika Aya hizi tatu 11,12 na13 anawahimiza Waislamu kuingia kwenye mapambano na makafiri kwa sababu kuu tatu. Mosi, Pale dini yao inapotukanwa na kudhalilishwa. Pili, Ahadi zinapokiukwa, na Tatu wanapodhamiria kumfukuza (au kumdhuru) Mtume (au kiongozi yeyote wa dini yao).


Surah: ATTAUBA 

Ayah : 14

قَٰتِلُوهُمۡ يُعَذِّبۡهُمُ ٱللَّهُ بِأَيۡدِيكُمۡ وَيُخۡزِهِمۡ وَيَنصُرۡكُمۡ عَلَيۡهِمۡ وَيَشۡفِ صُدُورَ قَوۡمٖ مُّؤۡمِنِينَ

Piganeni nao, Allah atawaadhibu kwa mikono yenu, na atawafedhehesha na atakunusuruni dhidi yao, na ataviponya vifua vya watu waumini



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 15

وَيُذۡهِبۡ غَيۡظَ قُلُوبِهِمۡۗ وَيَتُوبُ ٱللَّهُ عَلَىٰ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ

Na ataondoa hasira ya nyoyo zao (hao waumini). Na Allah humkubalia toba amtakaye. Na Allah ni Mwenye kujua sana, Mwenye hekima nyingi



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 16

أَمۡ حَسِبۡتُمۡ أَن تُتۡرَكُواْ وَلَمَّا يَعۡلَمِ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ جَٰهَدُواْ مِنكُمۡ وَلَمۡ يَتَّخِذُواْ مِن دُونِ ٱللَّهِ وَلَا رَسُولِهِۦ وَلَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَلِيجَةٗۚ وَٱللَّهُ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ

Hivi mlidhani (enyi waumini) kuwa mtaachwa tu bila ya Allah kuwajua wale waliopigana Jihadi kati yenu, na wala hawakumfanya mwandani wao isipokuwa Allah na Mtume wake na Waumini wenzao? Na Allah ana habari nyingi za yote mnayoyatenda



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 20

ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَهَاجَرُواْ وَجَٰهَدُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡ أَعۡظَمُ دَرَجَةً عِندَ ٱللَّهِۚ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡفَآئِزُونَ

Wale walioamini na wakahama na wakapigana Jihadi katika Njia ya Allah kwa mali zao na nafsi zao, hao wana hadhi kubwa zaidi mbele ya Allah na hao tu ndio wenye kufuzu



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 24

قُلۡ إِن كَانَ ءَابَآؤُكُمۡ وَأَبۡنَآؤُكُمۡ وَإِخۡوَٰنُكُمۡ وَأَزۡوَٰجُكُمۡ وَعَشِيرَتُكُمۡ وَأَمۡوَٰلٌ ٱقۡتَرَفۡتُمُوهَا وَتِجَٰرَةٞ تَخۡشَوۡنَ كَسَادَهَا وَمَسَٰكِنُ تَرۡضَوۡنَهَآ أَحَبَّ إِلَيۡكُم مِّنَ ٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ وَجِهَادٖ فِي سَبِيلِهِۦ فَتَرَبَّصُواْ حَتَّىٰ يَأۡتِيَ ٱللَّهُ بِأَمۡرِهِۦۗ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡفَٰسِقِينَ

Sema: Ikiwa baba zenu na watoto wenu na ndugu zenu na wake zenu na jamaa zenu na mali mlizochuma na biashara mnazoogopa kuharibika kwake (kwa kukosa soko) na majumba mnayoyapenda ni vipendwa zaidi kwenu kuliko Allah na Mtume wake na kupigana Jihadi katika Njia yake, basi ngojeni mpaka Allah alete amri yake (adhabu yake). Na Allah hawaongozi watu waovu



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 29

قَٰتِلُواْ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَلَا بِٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَلَا يُحَرِّمُونَ مَا حَرَّمَ ٱللَّهُ وَرَسُولُهُۥ وَلَا يَدِينُونَ دِينَ ٱلۡحَقِّ مِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ حَتَّىٰ يُعۡطُواْ ٱلۡجِزۡيَةَ عَن يَدٖ وَهُمۡ صَٰغِرُونَ

(Enyi Waislamu) Piganeni na wasiomuamini Allah wala Siku ya Mwisho na hawaharamishi alivyoviharimisha Allah na Mtume wake na hawafuati Dini ya Haki, miongoni mwa waliopewa Kitabu, mpaka watoe kodi[1] kwa hiari yao na wao wakiwa dhalili.[2]


1- - Jizia ni kodi maalumu anayoitoa kafiri mwenye uwezo wa kuitoa katika serikali ya Kiislamu kwa sababu ya huduma anazozipata ikiwemo ulinzi na usalama wa maisha yake, mwili wake, mali yake, dini yake, hadhi na heshima yake.


2- - Maana ya Aya hii ni maelekezo kwa mamlaka ya serikali ya Kiislamu ambayo imeshika hatamu. Sio maelekezo kwa mtu mmoja mmoja au kikundi kisichokuwa na mamlaka ya kisheria.


Surah: ATTAUBA 

Ayah : 36

إِنَّ عِدَّةَ ٱلشُّهُورِ عِندَ ٱللَّهِ ٱثۡنَا عَشَرَ شَهۡرٗا فِي كِتَٰبِ ٱللَّهِ يَوۡمَ خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ مِنۡهَآ أَرۡبَعَةٌ حُرُمٞۚ ذَٰلِكَ ٱلدِّينُ ٱلۡقَيِّمُۚ فَلَا تَظۡلِمُواْ فِيهِنَّ أَنفُسَكُمۡۚ وَقَٰتِلُواْ ٱلۡمُشۡرِكِينَ كَآفَّةٗ كَمَا يُقَٰتِلُونَكُمۡ كَآفَّةٗۚ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ مَعَ ٱلۡمُتَّقِينَ

Hakika, idadi ya miezi kwa Allah ni miezi kumi na miwili katika kitabu cha Allah[1] tangu alipoumba mbingu na ardhi. Katika hiyo ipo (miezi) minne mitukufu[2]. Hiyo ndio Dini iliyo sawa. Basi msidhulumu nafsi zenu humo (ndani ya hiyo miezi minne kwa kufanya mambo yasiyomridhisha Allah). Na piganeni na washirikina (makafiri) wote kama wao wanavyopigana nanyi nyote. Na jueni kuwa Allah yupo pamoja na wenye takwa (uchaMungu)


1- - Hiki ni kitabu kiitwacho Allauhul-Mahfuudh na kinachotunza mambo yote. Kitabu hiki kimetajwa katika Aya ya 22 ya Sura Alburuuj (85).


2- - Miezi hiyo mine mitukufu ni Dhul-qa’adah (Mfungopili), Dhul-hijja (Mfungotatu), Muharram (Mfungonne) na Rajabu (mfungokumi).


Surah: ATTAUBA 

Ayah : 38

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَا لَكُمۡ إِذَا قِيلَ لَكُمُ ٱنفِرُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ ٱثَّاقَلۡتُمۡ إِلَى ٱلۡأَرۡضِۚ أَرَضِيتُم بِٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا مِنَ ٱلۡأٓخِرَةِۚ فَمَا مَتَٰعُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا فِي ٱلۡأٓخِرَةِ إِلَّا قَلِيلٌ

Enyi mlioamini, mna nini wakati mnapoambiwa: Nendeni haraka katika Njia ya Allah (Jihadi), mnajitia uzito katika ardhi (kwa kubaki majumbani na kuwa wazito katika kuitikia wito wa Jihadi)? Je, mmeyaridhia maisha ya dunia kuliko ya Akhera? Basi hazikuwa starehe za maisha ya dunia ukizilinganisha na za Akhera isipokuwa ni chache mno



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 39

إِلَّا تَنفِرُواْ يُعَذِّبۡكُمۡ عَذَابًا أَلِيمٗا وَيَسۡتَبۡدِلۡ قَوۡمًا غَيۡرَكُمۡ وَلَا تَضُرُّوهُ شَيۡـٔٗاۗ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ

Kama hamtatoka (kwenda kupambana kwenye Jihadi basi Allah) atakuadhibuni adhabu inayoumiza mno, na atabadilisha (na kuleta) watu wengine wasiokuwa nyinyi (wenye utayari wa kwenda Jihadi) na nyinyi hamtamdhuru chochote Allah (kwa kuikimbia kwenu Jihadi). Na Allah ni Muweza wa kila kitu



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 40

إِلَّا تَنصُرُوهُ فَقَدۡ نَصَرَهُ ٱللَّهُ إِذۡ أَخۡرَجَهُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ ثَانِيَ ٱثۡنَيۡنِ إِذۡ هُمَا فِي ٱلۡغَارِ إِذۡ يَقُولُ لِصَٰحِبِهِۦ لَا تَحۡزَنۡ إِنَّ ٱللَّهَ مَعَنَاۖ فَأَنزَلَ ٱللَّهُ سَكِينَتَهُۥ عَلَيۡهِ وَأَيَّدَهُۥ بِجُنُودٖ لَّمۡ تَرَوۡهَا وَجَعَلَ كَلِمَةَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ ٱلسُّفۡلَىٰۗ وَكَلِمَةُ ٱللَّهِ هِيَ ٱلۡعُلۡيَاۗ وَٱللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ

Ikiwa nyinyi hamtamnusuru Mtume (Muhammad), basi Allah alikwishamnusuru pale waliokufuru walipomtoa (walipomfukuza) akiwa mmoja kati ya wawili wakati walipokuwa kwenye pango (la mlima Thaur), wakati akimwambia Swahibawake[1]: “Usihuzunike. Hakika, Allah yupo pamoja nasi”. Allah alimteremshia utulivu wake, na akampa nguvu kwa majeshi ambayo hamkuyaona, na akalifanya neno la waliokufuru kuwa chini sana, na Neno la Allah ndilo lililo juu zaidi. Na Allah ndiye Mwenye nguvu mno, Mwenye hekima sana[2]


1- - Alikuwa Swahaba Abubakar, Allah amuwie radhi.


2- - Aya hii inatutajia tukio adhimu la kuhama kwa Nabii Muhammad (Allah amshushie rehema na amani)
kutoka kwenye mji Mtukufu wa Makkah na kwenda kujificha kwenye pango (Ghari Thaur) kwa muda wa
siku tatu, na hatimae kuelekea uhamishoni kwenye Mji wa Madina. Aidha, Allah kupitia Aya hii
ametudhihirishia wazi utukufu wa Nabii wake na utukufu wa Swahaba Abubakar Allah amridhie ambaye
Alifuatana na Nabii kwenye msafara huo.


Surah: ATTAUBA 

Ayah : 41

ٱنفِرُواْ خِفَافٗا وَثِقَالٗا وَجَٰهِدُواْ بِأَمۡوَٰلِكُمۡ وَأَنفُسِكُمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِۚ ذَٰلِكُمۡ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Tokeni haraka (kwenda kwenye Jihadi katika mazingira yoyote) mkiwa wepesi (wa hali, mali, maandalizi n.k.) na wazito (wa hali, mali, maandalizi n.k.) na piganeni Jihadi kwa mali zenu na nafsi zenu katika Njia ya Allah. Hiyo ni heri kwenu iwapo mnajua



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 44

لَا يَسۡتَـٔۡذِنُكَ ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ أَن يُجَٰهِدُواْ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡۗ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلۡمُتَّقِينَ

Hawakuombi ruhusa wale wanaomuamini Allah na Siku ya Mwisho, wasiende kupigana Jihadi kwa mali zao na nafsi zao. Na Allah ni Mwenye kuwajua mno wachaMungu



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 73

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّبِيُّ جَٰهِدِ ٱلۡكُفَّارَ وَٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱغۡلُظۡ عَلَيۡهِمۡۚ وَمَأۡوَىٰهُمۡ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Ewe Nabii, pambana na makafiri na wanafiki (kwa mbinu za aina zote) na uwe mkali kwao. Na makazi yao ni Jahanamu, na huo ni mwisho mbaya sana



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 88

لَٰكِنِ ٱلرَّسُولُ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَعَهُۥ جَٰهَدُواْ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡۚ وَأُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمُ ٱلۡخَيۡرَٰتُۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Lakini Mtume na wale walioamini pamoja naye walipigana Jihadi kwa mali zao na nafsi zao. Na hao ndio watakaopata heri nyingi na hao ndio hasa wenye kufaulu



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 89

أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Allah amewaandalia Pepo zipitazo mito mbele yake wadumu humo. Huko ndiko kufuzu kukubwa hasa



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 111

۞إِنَّ ٱللَّهَ ٱشۡتَرَىٰ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ أَنفُسَهُمۡ وَأَمۡوَٰلَهُم بِأَنَّ لَهُمُ ٱلۡجَنَّةَۚ يُقَٰتِلُونَ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ فَيَقۡتُلُونَ وَيُقۡتَلُونَۖ وَعۡدًا عَلَيۡهِ حَقّٗا فِي ٱلتَّوۡرَىٰةِ وَٱلۡإِنجِيلِ وَٱلۡقُرۡءَانِۚ وَمَنۡ أَوۡفَىٰ بِعَهۡدِهِۦ مِنَ ٱللَّهِۚ فَٱسۡتَبۡشِرُواْ بِبَيۡعِكُمُ ٱلَّذِي بَايَعۡتُم بِهِۦۚ وَذَٰلِكَ هُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Hakika, Allah amenunua kwa Waumini nafsi zao na mali zao kwamba watapata Pepo. Wanapigana katika Njia ya Allah; wanaua na wanauawa. Ni ahadi ya haki juu ya hilo katika Taurati na Injili na Qur’ani. Na ni nani atimizae ahadi zaidi kuliko Allah? Basi furahieni biashara yenu mliyofanya naye. Na huko ndiko hasa kufaulu kukubwa