Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 84

إِذۡ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلۡبٖ سَلِيمٍ

Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo ulio salama



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 85

إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَاذَا تَعۡبُدُونَ

Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 86

أَئِفۡكًا ءَالِهَةٗ دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ

Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Allah?



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 87

فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 88

فَنَظَرَ نَظۡرَةٗ فِي ٱلنُّجُومِ

Kisha akapiga jicho kutazama nyota



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 89

فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٞ

Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 90

فَتَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ مُدۡبِرِينَ

Nao wakamwacha, wakampa kisogo



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 91

فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمۡ فَقَالَ أَلَا تَأۡكُلُونَ

Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 92

مَا لَكُمۡ لَا تَنطِقُونَ

Mna nini hata hamsemi?



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 93

فَرَاغَ عَلَيۡهِمۡ ضَرۡبَۢا بِٱلۡيَمِينِ

Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 94

فَأَقۡبَلُوٓاْ إِلَيۡهِ يَزِفُّونَ

Basi wakamjia upesi upesi



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 95

قَالَ أَتَعۡبُدُونَ مَا تَنۡحِتُونَ

Akasema: Hivyomnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 96

وَٱللَّهُ خَلَقَكُمۡ وَمَا تَعۡمَلُونَ

Na hali Allah ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 97

قَالُواْ ٱبۡنُواْ لَهُۥ بُنۡيَٰنٗا فَأَلۡقُوهُ فِي ٱلۡجَحِيمِ

Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 98

فَأَرَادُواْ بِهِۦ كَيۡدٗا فَجَعَلۡنَٰهُمُ ٱلۡأَسۡفَلِينَ

Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 99

وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهۡدِينِ

Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 100

رَبِّ هَبۡ لِي مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa wema



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 101

فَبَشَّرۡنَٰهُ بِغُلَٰمٍ حَلِيمٖ

Basi tukambashiria mtoto aliye mpole



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 102

فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعۡيَ قَالَ يَٰبُنَيَّ إِنِّيٓ أَرَىٰ فِي ٱلۡمَنَامِ أَنِّيٓ أَذۡبَحُكَ فَٱنظُرۡ مَاذَا تَرَىٰۚ قَالَ يَـٰٓأَبَتِ ٱفۡعَلۡ مَا تُؤۡمَرُۖ سَتَجِدُنِيٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّـٰبِرِينَ

Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 103

فَلَمَّآ أَسۡلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلۡجَبِينِ

Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji (kifudifudi ili amchinje)



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 104

وَنَٰدَيۡنَٰهُ أَن يَـٰٓإِبۡرَٰهِيمُ

Tulimwita: Ewe Ibrahim!



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 105

قَدۡ صَدَّقۡتَ ٱلرُّءۡيَآۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 106

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡبَلَـٰٓؤُاْ ٱلۡمُبِينُ

Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 107

وَفَدَيۡنَٰهُ بِذِبۡحٍ عَظِيمٖ

Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu (mnyama wa kuchinja) mtukufu



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 108

وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 109

سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِبۡرَٰهِيمَ

Iwe salama kwa Ibrahim!



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 110

كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 111

إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 112

وَبَشَّرۡنَٰهُ بِإِسۡحَٰقَ نَبِيّٗا مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 113

وَبَٰرَكۡنَا عَلَيۡهِ وَعَلَىٰٓ إِسۡحَٰقَۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحۡسِنٞ وَظَالِمٞ لِّنَفۡسِهِۦ مُبِينٞ

Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa vizazi vyao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi