Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 70

إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَا تَعۡبُدُونَ

Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 71

قَالُواْ نَعۡبُدُ أَصۡنَامٗا فَنَظَلُّ لَهَا عَٰكِفِينَ

Wakasema: Tunaabudu masa-namu, daima tunayanyenyekea



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 72

قَالَ هَلۡ يَسۡمَعُونَكُمۡ إِذۡ تَدۡعُونَ

Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 73

أَوۡ يَنفَعُونَكُمۡ أَوۡ يَضُرُّونَ

Au yanakufaeni, au yanaku-dhuruni?



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 74

قَالُواْ بَلۡ وَجَدۡنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفۡعَلُونَ

Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 75

قَالَ أَفَرَءَيۡتُم مَّا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ

Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 76

أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلۡأَقۡدَمُونَ

Nyinyi na baba zenu wa zamani?



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 77

فَإِنَّهُمۡ عَدُوّٞ لِّيٓ إِلَّا رَبَّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Kwani hakika hao ni adui zangu, isipokuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 78

ٱلَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهۡدِينِ

Ambaye ndiye aliyeniumba, na Yeye ndiye ananiongoa



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 79

وَٱلَّذِي هُوَ يُطۡعِمُنِي وَيَسۡقِينِ

Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 80

وَإِذَا مَرِضۡتُ فَهُوَ يَشۡفِينِ

Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 81

وَٱلَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحۡيِينِ

Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 82

وَٱلَّذِيٓ أَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لِي خَطِيٓـَٔتِي يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 83

رَبِّ هَبۡ لِي حُكۡمٗا وَأَلۡحِقۡنِي بِٱلصَّـٰلِحِينَ

Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 84

وَٱجۡعَل لِّي لِسَانَ صِدۡقٖ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 85

وَٱجۡعَلۡنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ

Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 86

وَٱغۡفِرۡ لِأَبِيٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ

Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 87

وَلَا تُخۡزِنِي يَوۡمَ يُبۡعَثُونَ

Wala usinihizi (usinifedheheshe) Siku watapo fufuliwa



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 88

يَوۡمَ لَا يَنفَعُ مَالٞ وَلَا بَنُونَ

Siku ambayo kwamba mali hayatofaa kitu wala watoto



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 89

إِلَّا مَنۡ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلۡبٖ سَلِيمٖ

Isipokuwa mwenye kumjia Allah na moyo safi



Surah: AL-ANKABUUT 

Ayah : 16

وَإِبۡرَٰهِيمَ إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ وَٱتَّقُوهُۖ ذَٰلِكُمۡ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Na Ibrahim pale alipo waambia watu wake: Muabuduni Allah, na mcheni Yeye. Hiyo ndiyo kheri yenu, ikiwa nyinyi mnajua



Surah: AL-ANKABUUT 

Ayah : 17

إِنَّمَا تَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ أَوۡثَٰنٗا وَتَخۡلُقُونَ إِفۡكًاۚ إِنَّ ٱلَّذِينَ تَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ لَا يَمۡلِكُونَ لَكُمۡ رِزۡقٗا فَٱبۡتَغُواْ عِندَ ٱللَّهِ ٱلرِّزۡقَ وَٱعۡبُدُوهُ وَٱشۡكُرُواْ لَهُۥٓۖ إِلَيۡهِ تُرۡجَعُونَ

Hakika nyinyi mnaabudu masanamu badala ya Allah, na mnazua uzushi. Hakika hao mnao waabudu badala ya Allah hawakumilikiini riziki yoyote. Takeni riziki kwa Allah, na mumuabudu Yeye, na mumshukuru Yeye. Kwake Yeye ndio mtarudishwa



Surah: AL-ANKABUUT 

Ayah : 18

وَإِن تُكَذِّبُواْ فَقَدۡ كَذَّبَ أُمَمٞ مِّن قَبۡلِكُمۡۖ وَمَا عَلَى ٱلرَّسُولِ إِلَّا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Na mkikadhibisha, basi kaumu kadhaa wa kadhaa za kabla yenu zilikwisha kadhibisha. Na si juu ya Mtume ila kufikisha Ujumbe waziwazi



Surah: AL-ANKABUUT 

Ayah : 24

فَمَا كَانَ جَوَابَ قَوۡمِهِۦٓ إِلَّآ أَن قَالُواْ ٱقۡتُلُوهُ أَوۡ حَرِّقُوهُ فَأَنجَىٰهُ ٱللَّهُ مِنَ ٱلنَّارِۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ

Basi haikuwa jawabu ya watu wake ila ni kusema: Muuweni au mchomeni moto! Allah akamwokoa na moto. Hakika katika hayo zipo Ishara kwa watu wanaoamini



Surah: AL-ANKABUUT 

Ayah : 25

وَقَالَ إِنَّمَا ٱتَّخَذۡتُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ أَوۡثَٰنٗا مَّوَدَّةَ بَيۡنِكُمۡ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ ثُمَّ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ يَكۡفُرُ بَعۡضُكُم بِبَعۡضٖ وَيَلۡعَنُ بَعۡضُكُم بَعۡضٗا وَمَأۡوَىٰكُمُ ٱلنَّارُ وَمَا لَكُم مِّن نَّـٰصِرِينَ

Na alisema: Hakika nyinyi mmeyashika masanamu badala ya Allah kwa mapenzi yaliyo baina yenu katika uhai wa duniani. Kisha Siku ya Kiyama mtakataana nyinyi kwa nyinyi, na mtalaaniana nyinyi kwa nyinyi. Na makaazi yenu ni Motoni. Wala hamtapata wa kukunusuruni



Surah: AL-ANKABUUT 

Ayah : 26

۞فَـَٔامَنَ لَهُۥ لُوطٞۘ وَقَالَ إِنِّي مُهَاجِرٌ إِلَىٰ رَبِّيٓۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Lutwi akamuamini, na akasema: Mimi nahamia kwa Mola wangu Mlezi. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hekima



Surah: AL-ANKABUUT 

Ayah : 27

وَوَهَبۡنَا لَهُۥٓ إِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ وَجَعَلۡنَا فِي ذُرِّيَّتِهِ ٱلنُّبُوَّةَ وَٱلۡكِتَٰبَ وَءَاتَيۡنَٰهُ أَجۡرَهُۥ فِي ٱلدُّنۡيَاۖ وَإِنَّهُۥ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ لَمِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Na tulimtunukia (Ibrahim) Is-haq na Yaa’qub. Na tukajaalia katika dhuriya zake Unabii na Kitabu, na tukampa ujira wake katika dunia; naye hakika katika Akhera bila ya shaka ni katika watu wema



Surah: AL-ANKABUUT 

Ayah : 31

وَلَمَّا جَآءَتۡ رُسُلُنَآ إِبۡرَٰهِيمَ بِٱلۡبُشۡرَىٰ قَالُوٓاْ إِنَّا مُهۡلِكُوٓاْ أَهۡلِ هَٰذِهِ ٱلۡقَرۡيَةِۖ إِنَّ أَهۡلَهَا كَانُواْ ظَٰلِمِينَ

Na wajumbe wetu walipo mjia Ibrahim na bishara, walisema: Hakika sisi hapana shaka tutawaangamiza watu wa mji huu, kwani watu wake hakika wamekuwa madhaalimu



Surah: AL-ANKABUUT 

Ayah : 32

قَالَ إِنَّ فِيهَا لُوطٗاۚ قَالُواْ نَحۡنُ أَعۡلَمُ بِمَن فِيهَاۖ لَنُنَجِّيَنَّهُۥ وَأَهۡلَهُۥٓ إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ كَانَتۡ مِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ

Akasema: Hakika humo yumo Lutwi. Wao wakasema: Sisi tunajua zaidi nani yumo humo. Hapana shaka tutamwokoa yeye na ahali zake, isipokuwa mkewe aliye miongoni mwa wataokaa nyuma



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 83

۞وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبۡرَٰهِيمَ

Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,