Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 211

سَلۡ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ كَمۡ ءَاتَيۡنَٰهُم مِّنۡ ءَايَةِۭ بَيِّنَةٖۗ وَمَن يُبَدِّلۡ نِعۡمَةَ ٱللَّهِ مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَتۡهُ فَإِنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ

Waulize Wana wa Israili: Ni Aya ngapi zilizo wazi tumewapa? Na yeyote atakayebadili neema za Allah baada ya kumfikia, kwa hakika Allah ni Mkali wa kuadhibu



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 285

ءَامَنَ ٱلرَّسُولُ بِمَآ أُنزِلَ إِلَيۡهِ مِن رَّبِّهِۦ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَۚ كُلٌّ ءَامَنَ بِٱللَّهِ وَمَلَـٰٓئِكَتِهِۦ وَكُتُبِهِۦ وَرُسُلِهِۦ لَا نُفَرِّقُ بَيۡنَ أَحَدٖ مِّن رُّسُلِهِۦۚ وَقَالُواْ سَمِعۡنَا وَأَطَعۡنَاۖ غُفۡرَانَكَ رَبَّنَا وَإِلَيۡكَ ٱلۡمَصِيرُ

Mtume ameamini yote yaliyoteremshwa kwake kutoka kwa Mola wake Mlezi na Waumini (pia wameamini hivyo). Kila mmoja amemwamini Allah na Malaika wake na Vitabu vyake na Mitume wake. (Waumini na Mtume wao husema), “Hatutafautishi baina ya yoyote katika Mitume yake (wote tunawaamini). Na husema: “Tumesikia na tumetii tunakuomba msamaha ewe Mola wetu Mlezi, na marejeo ni kwako tu



Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 3

حُرِّمَتۡ عَلَيۡكُمُ ٱلۡمَيۡتَةُ وَٱلدَّمُ وَلَحۡمُ ٱلۡخِنزِيرِ وَمَآ أُهِلَّ لِغَيۡرِ ٱللَّهِ بِهِۦ وَٱلۡمُنۡخَنِقَةُ وَٱلۡمَوۡقُوذَةُ وَٱلۡمُتَرَدِّيَةُ وَٱلنَّطِيحَةُ وَمَآ أَكَلَ ٱلسَّبُعُ إِلَّا مَا ذَكَّيۡتُمۡ وَمَا ذُبِحَ عَلَى ٱلنُّصُبِ وَأَن تَسۡتَقۡسِمُواْ بِٱلۡأَزۡلَٰمِۚ ذَٰلِكُمۡ فِسۡقٌۗ ٱلۡيَوۡمَ يَئِسَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن دِينِكُمۡ فَلَا تَخۡشَوۡهُمۡ وَٱخۡشَوۡنِۚ ٱلۡيَوۡمَ أَكۡمَلۡتُ لَكُمۡ دِينَكُمۡ وَأَتۡمَمۡتُ عَلَيۡكُمۡ نِعۡمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ ٱلۡإِسۡلَٰمَ دِينٗاۚ فَمَنِ ٱضۡطُرَّ فِي مَخۡمَصَةٍ غَيۡرَ مُتَجَانِفٖ لِّإِثۡمٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Mmeharamishiwa (kula) mzoga[1] na damu na nyama ya nguruwe na (mnyama) aliyechinjwa pasina (kutajwa jina la) Allah na (mnyama) aliyekufa kwa kusongeka koo (kujinyonga) na aliyekufa kwa kupigwa na aliyekufa kwa kuporomoka na aliyekufa kwa kupigwa pembe (na mwenzake) na aliyeliwa (kwa kushambuliwa) na mnyama mkali ila (mliyemuwahi akiwa hai) mkamchinja. Na (pia mmeharamishiwa kula nyama ya mnyama) aliyechinjwa katika (sehem yalipo) masanamu.[2] Na (mmeharamishiwa) kutaka kujua mambo yaliyopangwa (na Allah ikiwemo kupiga ramli na mfano wa hilo) kwa kutumia mbao. Ilivyo ni kwamba hayo (yote) ni uovu. Leo waliokufuru wameikatia tamaa dini yenu, basi msiwaogope (isipokuwa) niogopeni Mimi. Leo nimekukamilishieni dini yenu na kukutimizieni neema yangu na nimeuchagua Uislamu uwe dini yenu. Na mwenye kushikwa na dhiki ya njaa kali pasipo na kukusudia dhambi (anaruhusiwa kula hivyo vilivyoharamishwa kwa sababu) hakika, Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa huruma


1- - Mzoga ni mnyama aliyekufa mwenyewe au amechinjwa bila ya kufuata taratibu za sheria ya Kiislamu; kibudu, nyamafu.


2- - Mnyama aliyechinjwa katika sehemu za masanamu, mizimu, makaburini nk. Ni haramu kula nyama yake.


Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 70

وَذَرِ ٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ دِينَهُمۡ لَعِبٗا وَلَهۡوٗا وَغَرَّتۡهُمُ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَاۚ وَذَكِّرۡ بِهِۦٓ أَن تُبۡسَلَ نَفۡسُۢ بِمَا كَسَبَتۡ لَيۡسَ لَهَا مِن دُونِ ٱللَّهِ وَلِيّٞ وَلَا شَفِيعٞ وَإِن تَعۡدِلۡ كُلَّ عَدۡلٖ لَّا يُؤۡخَذۡ مِنۡهَآۗ أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ أُبۡسِلُواْ بِمَا كَسَبُواْۖ لَهُمۡ شَرَابٞ مِّنۡ حَمِيمٖ وَعَذَابٌ أَلِيمُۢ بِمَا كَانُواْ يَكۡفُرُونَ

Na waache wale walioifanya dini yao mchezo na pumbao, na yamewahadaa maisha ya dunia. Na kumbusha kwayo (Qur’ani ili), isije nafsi ikaangamizwa kwasababu ya (madhambi) waliyoyachuma, haina mlinzi yeyote wala muombezi yeyote. Na hata kama (nafsi hiyo) itatoa fidia ya aina yoyote (ili isiadhibiwe) haitachukuliwa. Hao ndio wale walioangamizwa kwa (sababu ya madhambi) waliyoyachuma. Watapata kinywaji cha maji ya moto na adhabu iumizayo sana kwa (sababu) ya walivyokuwa wanakufuru



Surah: AL-ANBIYAA 

Ayah : 92

إِنَّ هَٰذِهِۦٓ أُمَّتُكُمۡ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ وَأَنَا۠ رَبُّكُمۡ فَٱعۡبُدُونِ

Kwa hakika huu umma wenu ni umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi. Kwa hivyo niabuduni Mimi



Surah: ALMUUMINUUN 

Ayah : 52

وَإِنَّ هَٰذِهِۦٓ أُمَّتُكُمۡ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ وَأَنَا۠ رَبُّكُمۡ فَٱتَّقُونِ

Na kwa yakini huu Umma wenu ni Umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi, basi nicheni Mimi



Surah: AL-QASWAS 

Ayah : 61

أَفَمَن وَعَدۡنَٰهُ وَعۡدًا حَسَنٗا فَهُوَ لَٰقِيهِ كَمَن مَّتَّعۡنَٰهُ مَتَٰعَ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا ثُمَّ هُوَ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ مِنَ ٱلۡمُحۡضَرِينَ

Je! Yule tuliye muahidi ahadi nzuri, tena naye akayapata, ni kama tuliye mstarehesha kwa starehe za maisha ya duniani, na kisha Siku ya Kiyama akawa miongoni mwa wanao hudhurishwa?



Surah: ASSAJDAH 

Ayah : 18

أَفَمَن كَانَ مُؤۡمِنٗا كَمَن كَانَ فَاسِقٗاۚ لَّا يَسۡتَوُۥنَ

Ati aliye Muumini atakuwa sawa na aliye mpotovu? Hawawi sawa



Surah: AZZUMAR 

Ayah : 11

قُلۡ إِنِّيٓ أُمِرۡتُ أَنۡ أَعۡبُدَ ٱللَّهَ مُخۡلِصٗا لَّهُ ٱلدِّينَ

Sema: Hakika mimi nimeamrishwa nimuabudu Allah kwa kumsafishia Dini Yeye tu



Surah: AZZUMAR 

Ayah : 12

وَأُمِرۡتُ لِأَنۡ أَكُونَ أَوَّلَ ٱلۡمُسۡلِمِينَ

Na nimeamrishwa niwe wa mwanzo wa Waislamu (wanao jisa-limisha)



Surah: AZZUMAR 

Ayah : 13

قُلۡ إِنِّيٓ أَخَافُ إِنۡ عَصَيۡتُ رَبِّي عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ

Sema: Hakika mimi ninaogopa adhabu ya Siku Kubwa nikimuasi Mola wangu Mlezi



Surah: AZZUMAR 

Ayah : 14

قُلِ ٱللَّهَ أَعۡبُدُ مُخۡلِصٗا لَّهُۥ دِينِي

Sema: Allah tu namuabudu kwa kumsafishia Yeye tu Dini yangu



Surah: AL-AALAA 

Ayah : 14

قَدۡ أَفۡلَحَ مَن تَزَكَّىٰ

Hakika amekwisha fanikiwa aliyejitakasa



Surah: AL-BAYYINAH 

Ayah : 5

وَمَآ أُمِرُوٓاْ إِلَّا لِيَعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَ حُنَفَآءَ وَيُقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَيُؤۡتُواْ ٱلزَّكَوٰةَۚ وَذَٰلِكَ دِينُ ٱلۡقَيِّمَةِ

Nao hawakuamrishwa kitu isipokuwa wamuabudu Allah kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu, na washike Sala, na watoe Zaka. Na hiyo ndiyo Dini madhubuti