ٱهۡدِنَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ
Tuongoze kwenye njia ilio nyooka
صِرَٰطَ ٱلَّذِينَ أَنۡعَمۡتَ عَلَيۡهِمۡ غَيۡرِ ٱلۡمَغۡضُوبِ عَلَيۡهِمۡ وَلَا ٱلضَّآلِّينَ
Njia ya ambao umewaneemesha, na sio yawalio kasirikiwa na sio ya waliopotea[1]
1- - Walioneemeshwa wametajwa katika Sura AnNisaa (4), Aya ya 69. Hapa Aya inaashiria utukufu wa Swahaba wa kiongozwana Abubakar, Umar, Uthman na Ali (Allah awawieradhi) kwasababu wao ni miongoni mwa walioneemeshwa na ambao tunatakiwa kufuata njia yao. Waliokasirikiwa wametajwa kuanzia Aya ya 75 mpaka Aya ya 90 ya Sura Albaqara, na waliopotea wametajwa katika Aya ya 77 ya Sura Almaida (5).
بَلَىٰۚ مَنۡ أَسۡلَمَ وَجۡهَهُۥ لِلَّهِ وَهُوَ مُحۡسِنٞ فَلَهُۥٓ أَجۡرُهُۥ عِندَ رَبِّهِۦ وَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ
Naam, wenye kujisalimisha kwa Allah na ilhali wanatenda yaliyo mazuri, basi watapata malipo yao kwa Mola wao, na hawatakuwa na hofu na hawatahuzunika
إِذۡ قَالَ لَهُۥ رَبُّهُۥٓ أَسۡلِمۡۖ قَالَ أَسۡلَمۡتُ لِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na (kumbuka) Mola wake alipomwambia: Jisalimishe. Akasema: Nimejisalimisha kwa Mola wa walimwengu wote
وَوَصَّىٰ بِهَآ إِبۡرَٰهِـۧمُ بَنِيهِ وَيَعۡقُوبُ يَٰبَنِيَّ إِنَّ ٱللَّهَ ٱصۡطَفَىٰ لَكُمُ ٱلدِّينَ فَلَا تَمُوتُنَّ إِلَّا وَأَنتُم مُّسۡلِمُونَ
Na Ibrahimu aliwausia hayo watoto wake na Yakubu (kwa kuwaambia): “Enyi watoto wangu, hakika Allah amekuteulieni dini, basi msife isipokuwa mkiwa Waisilamu
وَقَالُواْ كُونُواْ هُودًا أَوۡ نَصَٰرَىٰ تَهۡتَدُواْۗ قُلۡ بَلۡ مِلَّةَ إِبۡرَٰهِـۧمَ حَنِيفٗاۖ وَمَا كَانَ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ
Na wamesema: Kuweni Wayahudi au Wanaswara mtaon-goka. Sema: Bali (tunafuata) dini ya Ibrahimu aliyeacha dini zote potevu na kufuata Uislamu, na hakuwa miongoni mwa washirikina
ٱلَّذِينَ ءَاتَيۡنَٰهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ يَعۡرِفُونَهُۥ كَمَا يَعۡرِفُونَ أَبۡنَآءَهُمۡۖ وَإِنَّ فَرِيقٗا مِّنۡهُمۡ لَيَكۡتُمُونَ ٱلۡحَقَّ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ
Na wale tuliowapa kitabu wanayajua hayo[1], kama wana-vyowajua watoto wao. Lakini kundi katika wao wanaificha haki ilhali wanajua
1- - Ya kuwa Muhammad ni Mtume wa kweli na Kaaba ndio kibla sahihi cha Waislamu
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱدۡخُلُواْ فِي ٱلسِّلۡمِ كَآفَّةٗ وَلَا تَتَّبِعُواْ خُطُوَٰتِ ٱلشَّيۡطَٰنِۚ إِنَّهُۥ لَكُمۡ عَدُوّٞ مُّبِينٞ
Enyi mlioamini, ingieni kwenye Uislamu wote (wazima wazima), na msifuate nyayo za shetani, hakika yeye kwenu ni adui aliye wazi
إِنَّ ٱلدِّينَ عِندَ ٱللَّهِ ٱلۡإِسۡلَٰمُۗ وَمَا ٱخۡتَلَفَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَهُمُ ٱلۡعِلۡمُ بَغۡيَۢا بَيۡنَهُمۡۗ وَمَن يَكۡفُرۡ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ فَإِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ
Hakika, dini (inayokubalika) kwa Allah ni Uislamu tu. Na wale waliopewa Kitabu hawakutofautiana isipokuwa tu baada ya kuwa elimu imewafikia kwa sababu ya uovu uliokuwepo kati yao. Na yeyote anayezikataa Aya za Allah, basi hakika Allah ni Mwepesi mno wa kuhesabu
فَإِنۡ حَآجُّوكَ فَقُلۡ أَسۡلَمۡتُ وَجۡهِيَ لِلَّهِ وَمَنِ ٱتَّبَعَنِۗ وَقُل لِّلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡأُمِّيِّـۧنَ ءَأَسۡلَمۡتُمۡۚ فَإِنۡ أَسۡلَمُواْ فَقَدِ ٱهۡتَدَواْۖ وَّإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّمَا عَلَيۡكَ ٱلۡبَلَٰغُۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِٱلۡعِبَادِ
Na kama watakuletea hoja (yoyote), basi sema: Nimeukabidhi uso wangu (nimejisalimisha) kwa Allah; mimi na wale walionifuata. Na waambie waliopewa kitabu na wasio na elimu kwamba: Je, mmesilimu (Mmejisalimisha kwa Allah)? Kama wamesilimu basi hakika wameongoka, na kama wakikataa, basi wajibu wako ni kufikisha tu. Na Allah anawaona mno waja
إِنَّ ٱللَّهَ رَبِّي وَرَبُّكُمۡ فَٱعۡبُدُوهُۚ هَٰذَا صِرَٰطٞ مُّسۡتَقِيمٞ
Hakika Allah ndiye Mola wangu na Mola wenu, basi muabuduni. Hii ndiyo njia iliyonyooka
مَا كَانَ إِبۡرَٰهِيمُ يَهُودِيّٗا وَلَا نَصۡرَانِيّٗا وَلَٰكِن كَانَ حَنِيفٗا مُّسۡلِمٗا وَمَا كَانَ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ
Ibrahimu hakuwa Myahudi na wala (hakuwa) Mnaswara, lakini alikuwa Muongofu, Muislamu na hakuwa miongoni mwa Washirikina
وَمَن يَبۡتَغِ غَيۡرَ ٱلۡإِسۡلَٰمِ دِينٗا فَلَن يُقۡبَلَ مِنۡهُ وَهُوَ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ
Na yeyote atakayetaka dini isiyokuwa Uislamu, hatakubaliwa na Akhera atakuwa miongoni mwa wenye hasara
وَكَيۡفَ تَكۡفُرُونَ وَأَنتُمۡ تُتۡلَىٰ عَلَيۡكُمۡ ءَايَٰتُ ٱللَّهِ وَفِيكُمۡ رَسُولُهُۥۗ وَمَن يَعۡتَصِم بِٱللَّهِ فَقَدۡ هُدِيَ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ
Na vipi mnakufuru na ilhali mnasomewa Aya za Allah na mnaye Mjumbe wake? Na yeyote atakayeshikamana na Allah, basi hakika ameongozwa katika njia iliyonyooka
وَمَنۡ أَحۡسَنُ دِينٗا مِّمَّنۡ أَسۡلَمَ وَجۡهَهُۥ لِلَّهِ وَهُوَ مُحۡسِنٞ وَٱتَّبَعَ مِلَّةَ إِبۡرَٰهِيمَ حَنِيفٗاۗ وَٱتَّخَذَ ٱللَّهُ إِبۡرَٰهِيمَ خَلِيلٗا
Na hakuna aliye na dini iliyo nzuri (sahihi) sana kuliko yule aliyeusalimisha uso wake kwa Allah (kwa kumtii), naye akawa mwenye kufanya mazuri na akafuata dini ya Ibrahimu akijitenga na Shirki. Na Allah amemfanya Ibrahimu kipenzi (chake)
يَهۡدِي بِهِ ٱللَّهُ مَنِ ٱتَّبَعَ رِضۡوَٰنَهُۥ سُبُلَ ٱلسَّلَٰمِ وَيُخۡرِجُهُم مِّنَ ٱلظُّلُمَٰتِ إِلَى ٱلنُّورِ بِإِذۡنِهِۦ وَيَهۡدِيهِمۡ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ
Kwa (Kitabu) hicho Allah anamuongoza anayefuata radhi zake katika njia za amani na anawatoa katika viza (na) kuwapeleka kwenye nuru kwa idhini yake, na anawaongoza kwenye njia iliyonyooka
وَجَعَلُواْ لِلَّهِ مِمَّا ذَرَأَ مِنَ ٱلۡحَرۡثِ وَٱلۡأَنۡعَٰمِ نَصِيبٗا فَقَالُواْ هَٰذَا لِلَّهِ بِزَعۡمِهِمۡ وَهَٰذَا لِشُرَكَآئِنَاۖ فَمَا كَانَ لِشُرَكَآئِهِمۡ فَلَا يَصِلُ إِلَى ٱللَّهِۖ وَمَا كَانَ لِلَّهِ فَهُوَ يَصِلُ إِلَىٰ شُرَكَآئِهِمۡۗ سَآءَ مَا يَحۡكُمُونَ
Na wamemfanyia Allah fungu katika mimea na wanyama aliowaumba, na kusema: Hiki ni kwa ajili ya Allah, kwa madai yao tu, na hiki ni kwa ajili ya washirika wetu. Basi kilichokuwa cha washirika wao hakifiki kwa Allah na kilichokuwa cha Allah kinafika kwa washirika wao. Ni mabaya mno (haya) wanayoyahukumu
وَأَنَّ هَٰذَا صِرَٰطِي مُسۡتَقِيمٗا فَٱتَّبِعُوهُۖ وَلَا تَتَّبِعُواْ ٱلسُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمۡ عَن سَبِيلِهِۦۚ ذَٰلِكُمۡ وَصَّىٰكُم بِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ
Na kwa hakika, hii ni njia yangu iliyonyooka, basi ifuateni. Na msifuate njia nyingine zikaku-farakanisheni muiache njia yake. Hayo amekuusieni (Allah) ili muwe wachaMungu
قُلۡ إِنَّنِي هَدَىٰنِي رَبِّيٓ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ دِينٗا قِيَمٗا مِّلَّةَ إِبۡرَٰهِيمَ حَنِيفٗاۚ وَمَا كَانَ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ
Sema: Kwa hakika, mimi ameniongoza Mola wangu Mlezi kwenye njia iliyo nyooka; dini iliyo sawa kabisa, mila ya Ibrahimu aliyeacha itikadi zote potofu na hakuwa miongoni mwa washirikina
قُلۡ أَمَرَ رَبِّي بِٱلۡقِسۡطِۖ وَأَقِيمُواْ وُجُوهَكُمۡ عِندَ كُلِّ مَسۡجِدٖ وَٱدۡعُوهُ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَۚ كَمَا بَدَأَكُمۡ تَعُودُونَ
Sema: Mola wangu Mlezi ameamrisha (kufanya) uadilifu. Na elekezeni nyuso zenu kila mnaposwali (mkusudieni Allah kila mfanyapo ibada) na muabuduni yeye tu mkimtakasia dini. Kama (Allah) ambavyo amekuumbeni mwanzo ndivyo mtakavyorudi
هُوَ ٱلَّذِيٓ أَرۡسَلَ رَسُولَهُۥ بِٱلۡهُدَىٰ وَدِينِ ٱلۡحَقِّ لِيُظۡهِرَهُۥ عَلَى ٱلدِّينِ كُلِّهِۦ وَلَوۡ كَرِهَ ٱلۡمُشۡرِكُونَ
Yeye (Allah) ndiye aliyemtuma Mtume wake kwa uwongofu (Qur’an) na Dini ya Haki ili ipate kuzishinda dini zote, na hata kama washirikina watachukia
وَٱللَّهُ يَدۡعُوٓاْ إِلَىٰ دَارِ ٱلسَّلَٰمِ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ
Na Allah anaita (watu) kwenye nyumba ya amani na anamuongoza amtakaye kwenye njia iliyonyooka
إِنِّي تَوَكَّلۡتُ عَلَى ٱللَّهِ رَبِّي وَرَبِّكُمۚ مَّا مِن دَآبَّةٍ إِلَّا هُوَ ءَاخِذُۢ بِنَاصِيَتِهَآۚ إِنَّ رَبِّي عَلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ
Hakika mimi nimemtegemea Allah, Mola wangu mlezi na Mola wenu mlezi. Hakuna mnyama (kiumbe) yeyote ispokuwa yeye (Allah) amezishika nywele zake za utosi. Bila shaka Mola wangu mlezi yupo katika njia iliyonyooka
رَبِّ ٱجۡعَلۡنِي مُقِيمَ ٱلصَّلَوٰةِ وَمِن ذُرِّيَّتِيۚ رَبَّنَا وَتَقَبَّلۡ دُعَآءِ
(Ewe) Mola wangu Mlezi, nijaalie niwe mwenye kusimamisha Swala, na katika watoto dhuriya zangu pia. Ewe Mola wetu Mlezi, na ipokee dua yangu
وَضَرَبَ ٱللَّهُ مَثَلٗا رَّجُلَيۡنِ أَحَدُهُمَآ أَبۡكَمُ لَا يَقۡدِرُ عَلَىٰ شَيۡءٖ وَهُوَ كَلٌّ عَلَىٰ مَوۡلَىٰهُ أَيۡنَمَا يُوَجِّههُّ لَا يَأۡتِ بِخَيۡرٍ هَلۡ يَسۡتَوِي هُوَ وَمَن يَأۡمُرُ بِٱلۡعَدۡلِ وَهُوَ عَلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ
Na Allah anapiga mfano wa watu wawili: Mmoja wao bubu, hawezi chochote, naye ni mzigo juu ya bwana wake, popote amtumapo haleti heri. Hivi, huyu anaweza kuwa sawa na yule anayeamuru kwa uadilifu naye yupo katika njia iliyonyoka?[1]
1- - Aya inaelezea ubora wa aliye na elimu na asiye na elimu kuwa asiye na elimu ni sawa na bubu hana kheri yeyote itakayo mnufaisha Allah. Lakini pia mwenye elimu akaacha kuifanyia kazi katika daawa elimu yake sawa na kutokuwa nayo hana tofauti na bubu.
وَإِنَّ ٱللَّهَ رَبِّي وَرَبُّكُمۡ فَٱعۡبُدُوهُۚ هَٰذَا صِرَٰطٞ مُّسۡتَقِيمٞ
Na hakika Allah ni Mola wangu Mlezi, na Mola wenu Mlezi. Basi muabuduni Yeye. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka
لَوۡ كَانَ فِيهِمَآ ءَالِهَةٌ إِلَّا ٱللَّهُ لَفَسَدَتَاۚ فَسُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ رَبِّ ٱلۡعَرۡشِ عَمَّا يَصِفُونَ
Lau wangeli kuwamo humo miungu wengine isipokuwa Allah basi bila ya shaka hizo mbingu na ardhi zingeli fisidika. Subhana ‘Llah Ametakasika Allah, Bwana wa A’rshi (Kiti cha Enzi), na hayo wanayo yazua
إِنَّ هَٰذِهِۦٓ أُمَّتُكُمۡ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ وَأَنَا۠ رَبُّكُمۡ فَٱعۡبُدُونِ
Kwa hakika huu umma wenu ni umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi. Kwa hivyo niabuduni Mimi
وَلِيَعۡلَمَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡعِلۡمَ أَنَّهُ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّكَ فَيُؤۡمِنُواْ بِهِۦ فَتُخۡبِتَ لَهُۥ قُلُوبُهُمۡۗ وَإِنَّ ٱللَّهَ لَهَادِ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ
Na ili walio pewa elimu wajue kuwa hayo ni Haki itokayo kwa Mola wako Mlezi na waamini, na zipate kutua nyoyo zao. Na hakika Allah ndiye anaye waongoa wenye kuamini kwenye Njia Iliyo Nyooka
وَجَٰهِدُواْ فِي ٱللَّهِ حَقَّ جِهَادِهِۦۚ هُوَ ٱجۡتَبَىٰكُمۡ وَمَا جَعَلَ عَلَيۡكُمۡ فِي ٱلدِّينِ مِنۡ حَرَجٖۚ مِّلَّةَ أَبِيكُمۡ إِبۡرَٰهِيمَۚ هُوَ سَمَّىٰكُمُ ٱلۡمُسۡلِمِينَ مِن قَبۡلُ وَفِي هَٰذَا لِيَكُونَ ٱلرَّسُولُ شَهِيدًا عَلَيۡكُمۡ وَتَكُونُواْ شُهَدَآءَ عَلَى ٱلنَّاسِۚ فَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُواْ ٱلزَّكَوٰةَ وَٱعۡتَصِمُواْ بِٱللَّهِ هُوَ مَوۡلَىٰكُمۡۖ فَنِعۡمَ ٱلۡمَوۡلَىٰ وَنِعۡمَ ٱلنَّصِيرُ
Na piganeni jihadi katika njia ya Allah kama inavyo stahiki jihadi yake. Yeye amekuteueni. Wala hakuweka juu yenu mambo mazito katika Dini. Nayo ni mila ya Baba yenu Ibrahim. Yeye (Allah) alikuiteni Waislamu tangu zamani, na katika hii (Qur’ani) pia, ili Mtume awe shahidi juu yenu, na nyinyi muwe mashahidi kwa watu. Basi shikeni Sala na toeni Zaka na shikamaneni na Allah. Yeye ndiye Mlinzi wenu, Mlinzi bora kabisa, na Msaidizi bora kabisa