Surah: ADH-DHAARIYAAT 

Ayah : 44

فَعَتَوۡاْ عَنۡ أَمۡرِ رَبِّهِمۡ فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّـٰعِقَةُ وَهُمۡ يَنظُرُونَ

Wakaasi amri ya bwana wao, basi ikawachukua adhabu ya moto hali yakuwa wao wakiangalia



Surah: ADH-DHAARIYAAT 

Ayah : 45

فَمَا ٱسۡتَطَٰعُواْ مِن قِيَامٖ وَمَا كَانُواْ مُنتَصِرِينَ

Basi hawakuweza kusimama na hawakua wao wenye kushinda



Surah: ANNAJMI 

Ayah : 51

وَثَمُودَاْ فَمَآ أَبۡقَىٰ

Na Watu wa Thamuwd kisha Hakuwabakisha



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 23

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِٱلنُّذُرِ

Kina Thamuwd waliwakadhibisha Waonyaji



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 24

فَقَالُوٓاْ أَبَشَرٗا مِّنَّا وَٰحِدٗا نَّتَّبِعُهُۥٓ إِنَّآ إِذٗا لَّفِي ضَلَٰلٖ وَسُعُرٍ

Wakasema: Ah! Tumfuate binaadamu miongoni mwetu? Hakika hapo sisi tutakuwa katika upotofu na wazimu



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 25

أَءُلۡقِيَ ٱلذِّكۡرُ عَلَيۡهِ مِنۢ بَيۡنِنَا بَلۡ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٞ

Ah! Ameteremshiwa ukumbusho (Wahyi) baina yetu? Bali yeye ni muongo mkubwa mwenye kiburi mno



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 26

سَيَعۡلَمُونَ غَدٗا مَّنِ ٱلۡكَذَّابُ ٱلۡأَشِرُ

Watakuja kujua kesho nani muongo mkubwa mwenye kiburi mno



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 27

إِنَّا مُرۡسِلُواْ ٱلنَّاقَةِ فِتۡنَةٗ لَّهُمۡ فَٱرۡتَقِبۡهُمۡ وَٱصۡطَبِرۡ

Hakika Sisi Tutawapelekea ngamia jike awe jaribio kwao, basi (Ee Nabiy Swaalih) watazame na vuta subira



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 28

وَنَبِّئۡهُمۡ أَنَّ ٱلۡمَآءَ قِسۡمَةُۢ بَيۡنَهُمۡۖ كُلُّ شِرۡبٖ مُّحۡتَضَرٞ

Na wajulishe kwamba maji ni mgawanyo baina yao (ngamia na wao), kila sehemu ya maji itahudhuriwa (kwa zamu)



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 29

فَنَادَوۡاْ صَاحِبَهُمۡ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ

Wakamuita Mtu Wao Akajipa Ushujaa Na Kumchinja



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 30

فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi Vipi Ilikua Adhabu Yangu Na Maonyo yangu?



Surah: AL-QAMAR

Ayah : 31

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ صَيۡحَةٗ وَٰحِدَةٗ فَكَانُواْ كَهَشِيمِ ٱلۡمُحۡتَظِرِ

Hakika Sisi Tulipeleka Kwao Ukelele Moja tu, wakawa kama mabuwa yaliyokatika-katika ya mtengenezaji zizi



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 4

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ وَعَادُۢ بِٱلۡقَارِعَةِ

Kina Thamudi na Adi walikadhibisha tukio (Kiyama) lenye kugonga (na kutia kiwewe)



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 5

فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهۡلِكُواْ بِٱلطَّاغِيَةِ

Ama kina Thamudi, waliangamizwa kwa ukelele mkali sana



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 6

وَأَمَّا عَادٞ فَأُهۡلِكُواْ بِرِيحٖ صَرۡصَرٍ عَاتِيَةٖ

Na ama kina Adi, waliangamizwa kwa upepo wenye baridi kali, uvumao kwa nguvu



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 7

سَخَّرَهَا عَلَيۡهِمۡ سَبۡعَ لَيَالٖ وَثَمَٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومٗاۖ فَتَرَى ٱلۡقَوۡمَ فِيهَا صَرۡعَىٰ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٍ خَاوِيَةٖ

(Allah) Aliwapelekea mausiku saba na michana minane mfululizo (bila kupumzika). Basi utaona watu wameanguka kifudifudi kana kwamba ni magogo ya mitende yaliyo wazi ndani



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 8

فَهَلۡ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٖ

Basi je, unamuona yeyote aliyebaki?



Surah: AL-FAJRI 

Ayah : 9

وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُواْ ٱلصَّخۡرَ بِٱلۡوَادِ

Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?



Surah: AL-SHAMS 

Ayah : 11

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ

Kina Thamudi walikadhibisha kwasababu ya upotofu wao,



Surah: AL-SHAMS 

Ayah : 12

إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا

Alipo simama mwovu wao mkubwa



Surah: AL-SHAMS 

Ayah : 13

فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا

Hapo Mtume wa Allah alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Allah, mwacheni anywe maji fungu lake



Surah: AL-SHAMS 

Ayah : 14

فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا

Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwahivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwasababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa



Surah: AL-SHAMS 

Ayah : 15

وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا

Wala Yeye haogopi matokeo yake