Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 21

وَقَاسَمَهُمَآ إِنِّي لَكُمَا لَمِنَ ٱلنَّـٰصِحِينَ

Na (shetani) akawaapia (kwamba): Kwa hakika kabisa, mimi kwenu ni miongoni mwa watoaji nasaha



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 22

فَدَلَّىٰهُمَا بِغُرُورٖۚ فَلَمَّا ذَاقَا ٱلشَّجَرَةَ بَدَتۡ لَهُمَا سَوۡءَٰتُهُمَا وَطَفِقَا يَخۡصِفَانِ عَلَيۡهِمَا مِن وَرَقِ ٱلۡجَنَّةِۖ وَنَادَىٰهُمَا رَبُّهُمَآ أَلَمۡ أَنۡهَكُمَا عَن تِلۡكُمَا ٱلشَّجَرَةِ وَأَقُل لَّكُمَآ إِنَّ ٱلشَّيۡطَٰنَ لَكُمَا عَدُوّٞ مُّبِينٞ

(Shetani) Akawashusha (Kutoka katika daraja la utiifu na kuwaweka katika uovu wa kukaidi amri ya Allah) kwa njia ya hadaa. Basi walipo uonja mti ule, zilidhihiri tupu zao na wakaanza kujibandika majani ya bustanini (ili kujisitiri). Na Mola wao aliwaita: Hivi sikukukatazeni mti ule na kukuambieni ya kwamba, hakika shetani kwenu ni adui aliye dhahiri sana?



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 27

يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ لَا يَفۡتِنَنَّكُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ كَمَآ أَخۡرَجَ أَبَوَيۡكُم مِّنَ ٱلۡجَنَّةِ يَنزِعُ عَنۡهُمَا لِبَاسَهُمَا لِيُرِيَهُمَا سَوۡءَٰتِهِمَآۚ إِنَّهُۥ يَرَىٰكُمۡ هُوَ وَقَبِيلُهُۥ مِنۡ حَيۡثُ لَا تَرَوۡنَهُمۡۗ إِنَّا جَعَلۡنَا ٱلشَّيَٰطِينَ أَوۡلِيَآءَ لِلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ

Enyi Wanadamu, kamwe shetani asikufitinisheni[1] kama alivyowatoa Peponi wazazi wenu, akiwavua nguo zao ili kuwawekea wazi tupu zao. Hakika yeye (shetani) anakuoneni yeye na jeshi lake katika namna ambayo nyinyi hamuwaoni. Hakika, sisi tumewafanya mashetani wandani wa (watu) wasioamini


1- - Shetani asikudanganyeni kwa kukupambieni maasi, kama ambavyo alimhadaa baba yenu Adamu na mkewe kwa kuwashawishi waonje mti. Matokeo yake walitolewa Peponi.


Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 200

وَإِمَّا يَنزَغَنَّكَ مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ نَزۡغٞ فَٱسۡتَعِذۡ بِٱللَّهِۚ إِنَّهُۥ سَمِيعٌ عَلِيمٌ

Na iwapo utahisi ushawishi wowote wa shetani basi omba kinga kwa Allah. Hakika, yeye (Allah) ni Msikivu sana, Mjuzi mno



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 201

إِنَّ ٱلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ إِذَا مَسَّهُمۡ طَـٰٓئِفٞ مِّنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ تَذَكَّرُواْ فَإِذَا هُم مُّبۡصِرُونَ

Hakika, wale wamchao Allah ukiwagusa upepo (wasiwasi, uchochezi na ushawishi) wa shetani wanakumbuka (mafundisho na muongozo wa Allah) na hapo hapo wanaona (haki na kuifuata)



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 202

وَإِخۡوَٰنُهُمۡ يَمُدُّونَهُمۡ فِي ٱلۡغَيِّ ثُمَّ لَا يُقۡصِرُونَ

Na ndugu zao wanawavuta kwenye upotevu kisha hawaachi



Surah: AN-FAL 

Ayah : 48

وَإِذۡ زَيَّنَ لَهُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ أَعۡمَٰلَهُمۡ وَقَالَ لَا غَالِبَ لَكُمُ ٱلۡيَوۡمَ مِنَ ٱلنَّاسِ وَإِنِّي جَارٞ لَّكُمۡۖ فَلَمَّا تَرَآءَتِ ٱلۡفِئَتَانِ نَكَصَ عَلَىٰ عَقِبَيۡهِ وَقَالَ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّنكُمۡ إِنِّيٓ أَرَىٰ مَا لَا تَرَوۡنَ إِنِّيٓ أَخَافُ ٱللَّهَۚ وَٱللَّهُ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ

Na (kumbukeni) wakati Shetani alipowapambia (alipowaaminisha makafiri kwamba) amali zao (ni nzuri) na akawaambia: Leo hii hakuna watu wa kukushindeni, na hakika mimi nipo bega kwa bega na nyinyi (nitakunusuruni). Basi yalipoona na majeshi mawili (na kukabiliana macho kwa macho), (shetani) alirudi nyuma na akasema: Mimi sipo pamoja nanyi. Mimi naona msiyoyaona. Mimi namuogopa Allah, na Allah ni mkali wa kuadhibu



Surah: IBRAHIM 

Ayah : 22

وَقَالَ ٱلشَّيۡطَٰنُ لَمَّا قُضِيَ ٱلۡأَمۡرُ إِنَّ ٱللَّهَ وَعَدَكُمۡ وَعۡدَ ٱلۡحَقِّ وَوَعَدتُّكُمۡ فَأَخۡلَفۡتُكُمۡۖ وَمَا كَانَ لِيَ عَلَيۡكُم مِّن سُلۡطَٰنٍ إِلَّآ أَن دَعَوۡتُكُمۡ فَٱسۡتَجَبۡتُمۡ لِيۖ فَلَا تَلُومُونِي وَلُومُوٓاْ أَنفُسَكُمۖ مَّآ أَنَا۠ بِمُصۡرِخِكُمۡ وَمَآ أَنتُم بِمُصۡرِخِيَّ إِنِّي كَفَرۡتُ بِمَآ أَشۡرَكۡتُمُونِ مِن قَبۡلُۗ إِنَّ ٱلظَّـٰلِمِينَ لَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Na Shetani atawaambia wafuasi (wake huko Akhera) mara itapokatwa hukumu (na watu wa Peponi kuingia Peponi na wa Motoni kuingia Motoni): Hakika Allah alikuahidini ahadi ya kweli. Nami nilikuahidini (uongo); lakini sikukutimizieni. Na sikuwa na mamlaka juu yenu, isipokuwa nilikuiteni (katika ukafiri na maasi), nanyi mkaniitikia. Basi msinilaumu mimi, bali jilaumuni wenyewe. Mimi siwezi kuwa msaidizi wenu, wala nyinyi hamuwezi kuwa wasaidizi wangu. Hakika mimi nilikataa tangu zamani kunishirikisha na Allah. Hakika madhalimu watakuwa na adhabu chungu mno



Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 31

إِلَّآ إِبۡلِيسَ أَبَىٰٓ أَن يَكُونَ مَعَ ٱلسَّـٰجِدِينَ

Isipokuwa Ibilisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na waliosujudu



Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 32

قَالَ يَـٰٓإِبۡلِيسُ مَا لَكَ أَلَّا تَكُونَ مَعَ ٱلسَّـٰجِدِينَ

(Allah) alisema: Ewe Ibilisi! Umepatwa na nini hata hukuwa pamoja na waliosujudu?



Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 33

قَالَ لَمۡ أَكُن لِّأَسۡجُدَ لِبَشَرٍ خَلَقۡتَهُۥ مِن صَلۡصَٰلٖ مِّنۡ حَمَإٖ مَّسۡنُونٖ

(Ibilisi) Alisema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliyemuumba kwa udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope meusi yaliyovunda[1]


1- - Ibilisi aliyasema hayo kwa kiburi na kujiona kuwa, Yeye aliyeumbwa kwa miale ya moto ni bora
zaidi kuliko Yule aliyeumbwa kwa udongo mweusi, unaotoa sauti na uliovunda.


Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 34

قَالَ فَٱخۡرُجۡ مِنۡهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٞ

(Allah) alisema: Basi toka humo (Peponi), kwa hakika wewe ni umelaaniwa



Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 35

وَإِنَّ عَلَيۡكَ ٱللَّعۡنَةَ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na hakika laana itakuwa juu yako mpaka Siku ya Malipo



Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 36

قَالَ رَبِّ فَأَنظِرۡنِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ

(Iblisi) Alisema: (Ewe) Mola wangu Mlezi, Nipe muhula (nibakishe) mpaka siku watakapofufuliwa (watu)



Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 37

قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلۡمُنظَرِينَ

(Allah) alisema: Kwa hakika wewe ni katika waliopewa muhula (wa kutoangamizwa mpaka siku hiyo)



Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 38

إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡوَقۡتِ ٱلۡمَعۡلُومِ

(Wewe utaendelea kuwepo) Mpaka siku ya wakati maalumu



Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 39

قَالَ رَبِّ بِمَآ أَغۡوَيۡتَنِي لَأُزَيِّنَنَّ لَهُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَأُغۡوِيَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ

(Ibilisi) Alisema: (Ewe) Mola wangu Mlezi, kwa ulivyonipotoa, basi ninakuapia nitawapambia (upotovu) hapa duniani na nitawapoteza wote



Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 40

إِلَّا عِبَادَكَ مِنۡهُمُ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipokuwa waja wako walio-safishwa



Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 41

قَالَ هَٰذَا صِرَٰطٌ عَلَيَّ مُسۡتَقِيمٌ

(Allah) Alisema: Hii Njia ya kuja kwangu Iliyo nyooka (kuwalinda waja wangu na upotovu hilo ni jukumu langu)



Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 42

إِنَّ عِبَادِي لَيۡسَ لَكَ عَلَيۡهِمۡ سُلۡطَٰنٌ إِلَّا مَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلۡغَاوِينَ

Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipokuwa (ataathirika nawe) yule mpotofu aliyekufuata



Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 43

وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمَوۡعِدُهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Na bila shaka Jahanamu ndipo mahali pao walipoahidiwa wote (wanaokufuata)



Surah: AL-HIJRI 

Ayah : 44

لَهَا سَبۡعَةُ أَبۡوَٰبٖ لِّكُلِّ بَابٖ مِّنۡهُمۡ جُزۡءٞ مَّقۡسُومٌ

(Moto wa Jahanamu) una milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu waliyotengewa



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 63

تَٱللَّهِ لَقَدۡ أَرۡسَلۡنَآ إِلَىٰٓ أُمَمٖ مِّن قَبۡلِكَ فَزَيَّنَ لَهُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ أَعۡمَٰلَهُمۡ فَهُوَ وَلِيُّهُمُ ٱلۡيَوۡمَ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Naapa kwajina la Allah hakika tulipeleka (Mitume) kwa umma zilizokuwa kabla yako, na shetani akawapambia matendo yao (mabaya wakayaona mazuri), basi yeye (shetani) leo ni rafiki yao, nao watapata adhabu iumizayo mno (Siku ya Kiyama)



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 98

فَإِذَا قَرَأۡتَ ٱلۡقُرۡءَانَ فَٱسۡتَعِذۡ بِٱللَّهِ مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ ٱلرَّجِيمِ

Na pindi unapotaka kusoma Qur’ani, basi jikinge kwa Allah (akulinde) na shetani aliyelaaniwa



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 99

إِنَّهُۥ لَيۡسَ لَهُۥ سُلۡطَٰنٌ عَلَى ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَلَىٰ رَبِّهِمۡ يَتَوَكَّلُونَ

Hakika yeye hana nguvu juu ya wale walioamini na kwa Mola wao mlezi tu wanategemea



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 100

إِنَّمَا سُلۡطَٰنُهُۥ عَلَى ٱلَّذِينَ يَتَوَلَّوۡنَهُۥ وَٱلَّذِينَ هُم بِهِۦ مُشۡرِكُونَ

Hakika nguvu yake ni juu ya wale tu wanaomfanya kuwa rafiki na wale wanaomshirikisha (Allah)



Surah: AL-ISRAA 

Ayah : 27

إِنَّ ٱلۡمُبَذِّرِينَ كَانُوٓاْ إِخۡوَٰنَ ٱلشَّيَٰطِينِۖ وَكَانَ ٱلشَّيۡطَٰنُ لِرَبِّهِۦ كَفُورٗا

Hakika wabadhirifu ni ndugu wa Mashetani. Na Shetani ni mwenye kumkufuru Mola wake Mlezi



Surah: AL-ISRAA 

Ayah : 53

وَقُل لِّعِبَادِي يَقُولُواْ ٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُۚ إِنَّ ٱلشَّيۡطَٰنَ يَنزَغُ بَيۡنَهُمۡۚ إِنَّ ٱلشَّيۡطَٰنَ كَانَ لِلۡإِنسَٰنِ عَدُوّٗا مُّبِينٗا

Waambie waja wangu waseme maneno mazuri, maana Shetani huchochea ugomvi baina yao. Hakika Shetani ni adui aliye dhaahiri kwa mwanaadamu



Surah: AL-ISRAA 

Ayah : 61

وَإِذۡ قُلۡنَا لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ ٱسۡجُدُواْ لِأٓدَمَ فَسَجَدُوٓاْ إِلَّآ إِبۡلِيسَ قَالَ ءَأَسۡجُدُ لِمَنۡ خَلَقۡتَ طِينٗا

Na pale tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam. Wakamsujudia isipo kuwa Iblisi. Akasema: Je! Nimsujudie uliye muumba kwa udongo?



Surah: AL-ISRAA 

Ayah : 62

قَالَ أَرَءَيۡتَكَ هَٰذَا ٱلَّذِي كَرَّمۡتَ عَلَيَّ لَئِنۡ أَخَّرۡتَنِ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ لَأَحۡتَنِكَنَّ ذُرِّيَّتَهُۥٓ إِلَّا قَلِيلٗا

Akasema: Hebu nambie khabari ya huyu uliye mtukuza juu yangu. Ukiniakhirisha mpaka Siku ya Kiyama, hapana shaka nitawaangamiza kizazi chake isipo kuwa wachache tu