Surah: AL-IMRAN 

Ayah : 181

لَّقَدۡ سَمِعَ ٱللَّهُ قَوۡلَ ٱلَّذِينَ قَالُوٓاْ إِنَّ ٱللَّهَ فَقِيرٞ وَنَحۡنُ أَغۡنِيَآءُۘ سَنَكۡتُبُ مَا قَالُواْ وَقَتۡلَهُمُ ٱلۡأَنۢبِيَآءَ بِغَيۡرِ حَقّٖ وَنَقُولُ ذُوقُواْ عَذَابَ ٱلۡحَرِيقِ

Hakika Allah amesikia kauli ya wale waliosema: Hakika Allah ni fukara na sisi ndio matajiri, tutakisajili walichokisema, na kuwaua kwao manabii bila ya haki, na siku ya Kiama tutawaambia: onjeni adhabu ya Moto wenye kuunguza



Surah: ANNISAI 

Ayah : 81

وَيَقُولُونَ طَاعَةٞ فَإِذَا بَرَزُواْ مِنۡ عِندِكَ بَيَّتَ طَآئِفَةٞ مِّنۡهُمۡ غَيۡرَ ٱلَّذِي تَقُولُۖ وَٱللَّهُ يَكۡتُبُ مَا يُبَيِّتُونَۖ فَأَعۡرِضۡ عَنۡهُمۡ وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِۚ وَكَفَىٰ بِٱللَّهِ وَكِيلًا

Na wanasema: Tumetii. Lakini wakiondoka kwako kundi miongoni mwao linapanga njama usiku tofauti na yale unayosema, na Allah anayaandika wanayo yapanga usiku. Basi wapuuze, na mtegemee Allah, na inatosha kwamba Allah ni Mwenye kutegemewa



Surah: YUNUS 

Ayah : 21

وَإِذَآ أَذَقۡنَا ٱلنَّاسَ رَحۡمَةٗ مِّنۢ بَعۡدِ ضَرَّآءَ مَسَّتۡهُمۡ إِذَا لَهُم مَّكۡرٞ فِيٓ ءَايَاتِنَاۚ قُلِ ٱللَّهُ أَسۡرَعُ مَكۡرًاۚ إِنَّ رُسُلَنَا يَكۡتُبُونَ مَا تَمۡكُرُونَ

Na tunapowaonjesha watu rehema yoyote baada ya shida iliyowagusa, ghafla huanza kufanya vitimbi katika Aya zetu. Sema: Allah ni mwepesi zaidi wa (kutengua hila na vitimbi). Hakika, wajumbe wetu (Malaika waandishi) wanaandika vitimbi mnavyovifanya



Surah: AL-ISRAA 

Ayah : 13

وَكُلَّ إِنسَٰنٍ أَلۡزَمۡنَٰهُ طَـٰٓئِرَهُۥ فِي عُنُقِهِۦۖ وَنُخۡرِجُ لَهُۥ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ كِتَٰبٗا يَلۡقَىٰهُ مَنشُورًا

Na kila mtu tumemfungia a’mali yake shingoni mwake. Na Siku ya Kiyama tutamtolea kitabu atakacho kikuta kiwazi kimekunjuliwa



Surah: AL-ISRAA 

Ayah : 14

ٱقۡرَأۡ كِتَٰبَكَ كَفَىٰ بِنَفۡسِكَ ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكَ حَسِيبٗا

Ataambiwa: Soma kitabu chako! Nafsi yako inakutosha leo kukuhesabu



Surah: AL-ISRAA 

Ayah : 71

يَوۡمَ نَدۡعُواْ كُلَّ أُنَاسِۭ بِإِمَٰمِهِمۡۖ فَمَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَأُوْلَـٰٓئِكَ يَقۡرَءُونَ كِتَٰبَهُمۡ وَلَا يُظۡلَمُونَ فَتِيلٗا

Siku tutakapo waita kila kikundi cha watu kwa mujibu wa wakifuatacho - basi atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, basi hao watasoma kitabu chao wala hawatadhulumiwa hata chembe



Surah: AL-KAHF 

Ayah : 49

وَوُضِعَ ٱلۡكِتَٰبُ فَتَرَى ٱلۡمُجۡرِمِينَ مُشۡفِقِينَ مِمَّا فِيهِ وَيَقُولُونَ يَٰوَيۡلَتَنَا مَالِ هَٰذَا ٱلۡكِتَٰبِ لَا يُغَادِرُ صَغِيرَةٗ وَلَا كَبِيرَةً إِلَّآ أَحۡصَىٰهَاۚ وَوَجَدُواْ مَا عَمِلُواْ حَاضِرٗاۗ وَلَا يَظۡلِمُ رَبُّكَ أَحَدٗا

Na kitawekwa kitabu. Basi utawaona wakosefu wanavyo ogopa kwa yale yaliomo humo. Na watasema: Ole wetu! Kitabu hichi kina nini! Hakiachi dogo wala kubwa ila isipokuwa limelisajiliwa? Na watayakuta yote waliyo yatenda yamehudhuria hapo. Na Mola wako Mlezi hamdhulumu yeyote



Surah: MARYAM 

Ayah : 79

كَلَّاۚ سَنَكۡتُبُ مَا يَقُولُ وَنَمُدُّ لَهُۥ مِنَ ٱلۡعَذَابِ مَدّٗا

Hasha! Tutaandika anayo yasema, tutamkunjulia muda wa adhabu



Surah: ALMUUMINUUN 

Ayah : 62

وَلَا نُكَلِّفُ نَفۡسًا إِلَّا وُسۡعَهَاۚ وَلَدَيۡنَا كِتَٰبٞ يَنطِقُ بِٱلۡحَقِّ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na hatuilazimishi nafsi ila kwa kadri ya uwezo wake. Na tunacho kitabu kisemacho kweli. Nao hawatadhulumiwa



Surah: YAASIIN 

Ayah : 12

إِنَّا نَحۡنُ نُحۡيِ ٱلۡمَوۡتَىٰ وَنَكۡتُبُ مَا قَدَّمُواْ وَءَاثَٰرَهُمۡۚ وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ فِيٓ إِمَامٖ مُّبِينٖ

Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha



Surah: AZZUKHRUF 

Ayah : 19

وَجَعَلُواْ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ ٱلَّذِينَ هُمۡ عِبَٰدُ ٱلرَّحۡمَٰنِ إِنَٰثًاۚ أَشَهِدُواْ خَلۡقَهُمۡۚ سَتُكۡتَبُ شَهَٰدَتُهُمۡ وَيُسۡـَٔلُونَ

Na wakawafanya Malaika, ambao ni waja wa Mwingi wa Rehema, kuwa ni wanawake! Kwani wameshuhudia kuumbwa kwao? Ushahidi wao utaandikwa na wao watahojiwa!



Surah: AZZUKHRUF 

Ayah : 80

أَمۡ يَحۡسَبُونَ أَنَّا لَا نَسۡمَعُ سِرَّهُمۡ وَنَجۡوَىٰهُمۚ بَلَىٰ وَرُسُلُنَا لَدَيۡهِمۡ يَكۡتُبُونَ

Au wanadhani kwamba hatusikii siri zao na minong’ono yao? Wapi! Na wajumbe wetu wapo karibu nao, wanayaandika



Surah: AL-JAATHIYA 

Ayah : 28

وَتَرَىٰ كُلَّ أُمَّةٖ جَاثِيَةٗۚ كُلُّ أُمَّةٖ تُدۡعَىٰٓ إِلَىٰ كِتَٰبِهَا ٱلۡيَوۡمَ تُجۡزَوۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Na utauona kila umma umepiga magoti, na kila umma utaitwa kwenda kusoma kitabu chake: Leo mtalipwa mliyo kuwa mkiyatenda



Surah: AL-JAATHIYA 

Ayah : 29

هَٰذَا كِتَٰبُنَا يَنطِقُ عَلَيۡكُم بِٱلۡحَقِّۚ إِنَّا كُنَّا نَسۡتَنسِخُ مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Hiki kitabu chetu kinasema juu yenu kwa haki. Hakika Sisi tulikuwa tukiyaandika mliyo kuwa mkiyatenda



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 19

فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَيَقُولُ هَآؤُمُ ٱقۡرَءُواْ كِتَٰبِيَهۡ

Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 25

وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِشِمَالِهِۦ فَيَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي لَمۡ أُوتَ كِتَٰبِيَهۡ

Na ama yule atakayepewa kitabu chake kushotoni mwake; atasema: Ee! Laiti nisingelipewa kitabu changu!



Surah: ANNABAI 

Ayah : 29

وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ كِتَٰبٗا

Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika



Surah: ATTAK-WIIR 

Ayah : 10

وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتۡ

Na sahifa (kurasa) za kurekodi (matendo ya waja) zitakapo kunjuliwa, [wakati wa kuhesabiwa watu]



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 7

كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلۡفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٖ

Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 8

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سِجِّينٞ

Unajua nini Sijjin?



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 9

كِتَٰبٞ مَّرۡقُومٞ

Kitabu kilicho andikwa



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 18

كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلۡأَبۡرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ

Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I’liyyin



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 19

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا عِلِّيُّونَ

Na nini kitakacho kujulisha nini I’liyyin?



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 20

كِتَٰبٞ مَّرۡقُومٞ

Ni Kitabu kilicho andikwa



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 21

يَشۡهَدُهُ ٱلۡمُقَرَّبُونَ

Wanakishuhudia walio kurubishwa (na Allah)



Surah: AL-INSHIQAAQ 

Ayah : 7

فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ

Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,



Surah: AL-INSHIQAAQ 

Ayah : 8

فَسَوۡفَ يُحَاسَبُ حِسَابٗا يَسِيرٗا

Basi huyo atahesabiwa hisabu nyepesi,



Surah: AL-INSHIQAAQ 

Ayah : 9

وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورٗا

Na arudi kwa watu wake na furaha



Surah: AL-INSHIQAAQ 

Ayah : 10

وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهۡرِهِۦ

Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,



Surah: AL-INSHIQAAQ 

Ayah : 11

فَسَوۡفَ يَدۡعُواْ ثُبُورٗا

Basi huyo ataomba kuteketea