Surah: AZZUKHRUF 

Ayah : 3

إِنَّا جَعَلۡنَٰهُ قُرۡءَٰنًا عَرَبِيّٗا لَّعَلَّكُمۡ تَعۡقِلُونَ

Hakika, Sisi tumekifanya (hicho kitabu) Qur’ani ya Kiarabu ili mfahamu



Surah: AZZUKHRUF 

Ayah : 4

وَإِنَّهُۥ فِيٓ أُمِّ ٱلۡكِتَٰبِ لَدَيۡنَا لَعَلِيٌّ حَكِيمٌ

Na hakika kitabu hicho katika Kitabu Mama kilichopo kwetu, kwa yakini kabisa, ni kitukufu, chenye hekima nyingi



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 2

وَٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ

Nina apa kwa Kitabu kinacho bainisha



Surah: ADDUKHAAN 

Ayah : 3

إِنَّآ أَنزَلۡنَٰهُ فِي لَيۡلَةٖ مُّبَٰرَكَةٍۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ

Hakika, tumekiteremsha (kitabu hiki cha Qur’ani) katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi tumekuwa waonyaji



Surah: AL-JAATHIYA 

Ayah : 2

تَنزِيلُ ٱلۡكِتَٰبِ مِنَ ٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَكِيمِ

(Huu) Ni uteremsho wa Kitabu kutoka kwa Allah, Mwenye nguvu kubwa, Mwenye hekima sana



Surah: AL-JAATHIYA 

Ayah : 6

تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱللَّهِ نَتۡلُوهَا عَلَيۡكَ بِٱلۡحَقِّۖ فَبِأَيِّ حَدِيثِۭ بَعۡدَ ٱللَّهِ وَءَايَٰتِهِۦ يُؤۡمِنُونَ

Hizo Aya za Allah tunakusomea kwa haki. Basi ni mazungumzo gani watayaamini baada ya Allah na Aya zake?



Surah: AL-AHQAAF 

Ayah : 2

تَنزِيلُ ٱلۡكِتَٰبِ مِنَ ٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَكِيمِ

(Huu) Ni uteremsho wa Kitabu kutoka kwa Allah, Mwenye nguvu kubwa, Mwenye hekima sana



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 77

إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ

Hakika ya hiyo ni Kurani tukufu



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 78

فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ

Katika Kitabu kilichohifadhiwa



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 79

لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ

Haigusi isipokuwa waliotakaswa kabisa (Walio twahara)



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 80

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni uteremsho kutoka kwa Mola wa walimwengu wote



Surah: AL-HADIID

Ayah : 9

هُوَ ٱلَّذِي يُنَزِّلُ عَلَىٰ عَبۡدِهِۦٓ ءَايَٰتِۭ بَيِّنَٰتٖ لِّيُخۡرِجَكُم مِّنَ ٱلظُّلُمَٰتِ إِلَى ٱلنُّورِۚ وَإِنَّ ٱللَّهَ بِكُمۡ لَرَءُوفٞ رَّحِيمٞ

Yeye Ndiye Yule Anayemte-remshia mja Wake Aya zinazo bainisha ili Akutoeni katika giza na kukuingizeni kwenye Nuru. Na hakika Allah kwenu ni Mwenye huruma mno, Mwenye kurehemu



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 43

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni Uteremsho Kutoka Kwa Mola Wa Viumbe Vyote



Surah: AL-INSAAN

Ayah : 23

إِنَّا نَحۡنُ نَزَّلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡقُرۡءَانَ تَنزِيلٗا

Hakika Sisi tumekuteremshia Qur’ani kidogo kidogo (hatua kwa hatua)