Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 27

قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِيٓ أُرۡسِلَ إِلَيۡكُمۡ لَمَجۡنُونٞ

(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 28

قَالَ رَبُّ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡقِلُونَ

(Mussa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na vilivyomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 29

قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذۡتَ إِلَٰهًا غَيۡرِي لَأَجۡعَلَنَّكَ مِنَ ٱلۡمَسۡجُونِينَ

(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 30

قَالَ أَوَلَوۡ جِئۡتُكَ بِشَيۡءٖ مُّبِينٖ

Akasema: Je! Ijapokuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 31

قَالَ فَأۡتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ

Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 32

فَأَلۡقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعۡبَانٞ مُّبِينٞ

Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 33

وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِيَ بَيۡضَآءُ لِلنَّـٰظِرِينَ

Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 34

قَالَ لِلۡمَلَإِ حَوۡلَهُۥٓ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٞ

(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 35

يُرِيدُ أَن يُخۡرِجَكُم مِّنۡ أَرۡضِكُم بِسِحۡرِهِۦ فَمَاذَا تَأۡمُرُونَ

Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 36

قَالُوٓاْ أَرۡجِهۡ وَأَخَاهُ وَٱبۡعَثۡ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 37

يَأۡتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٖ

Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 38

فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 39

وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلۡ أَنتُم مُّجۡتَمِعُونَ

Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 40

لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ

Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 41

فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُواْ لِفِرۡعَوۡنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجۡرًا إِن كُنَّا نَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبِينَ

Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 42

قَالَ نَعَمۡ وَإِنَّكُمۡ إِذٗا لَّمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 43

قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلۡقُواْ مَآ أَنتُم مُّلۡقُونَ

Mussa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 44

فَأَلۡقَوۡاْ حِبَالَهُمۡ وَعِصِيَّهُمۡ وَقَالُواْ بِعِزَّةِ فِرۡعَوۡنَ إِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبُونَ

Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 45

فَأَلۡقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلۡقَفُ مَا يَأۡفِكُونَ

Mussa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 46

فَأُلۡقِيَ ٱلسَّحَرَةُ سَٰجِدِينَ

Hapo wachawi walipinduka wakasujudu



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 47

قَالُوٓاْ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 48

رَبِّ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ

Mola Mlezi wa Mussa na Harun



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 49

قَالَ ءَامَنتُمۡ لَهُۥ قَبۡلَ أَنۡ ءَاذَنَ لَكُمۡۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِي عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحۡرَ فَلَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيۡدِيَكُمۡ وَأَرۡجُلَكُم مِّنۡ خِلَٰفٖ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمۡ أَجۡمَعِينَ

(Firauni) akasema: Je! Mme-muamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutofautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 50

قَالُواْ لَا ضَيۡرَۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ

Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 51

إِنَّا نَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَٰيَٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 52

۞وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنۡ أَسۡرِ بِعِبَادِيٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ

Na tulimuamrisha Mussa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 53

فَأَرۡسَلَ فِرۡعَوۡنُ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 54

إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَشِرۡذِمَةٞ قَلِيلُونَ

(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 55

وَإِنَّهُمۡ لَنَا لَغَآئِظُونَ

Nao wanatuudhi



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 56

وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَٰذِرُونَ

Na sisi ni wengi, wenye kuchukua tahadhari