Surah: AL-QAMAR

Ayah : 55

فِي مَقۡعَدِ صِدۡقٍ عِندَ مَلِيكٖ مُّقۡتَدِرِۭ

Katika kizazi kilichoridhiwa mbele ya Mfalme aliye Muweza



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 46

وَلِمَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ جَنَّتَانِ

Na kwa mwenye kukhofu kusi-mamishwa mbele ya Mola wake atapata bustani mbili



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 10

وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ

Na (watakuwepo) waliotangulia mbele, (basi) watakua mbele.[1]


1- - Hawa ni wale ambao walitangulia mbele katika mambo ya kheri duniani ndio watakuwa mbele katika vyeo vya akhera.


Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 11

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ

Hao ndio watakao kurubishwa



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 12

فِي جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

katika pepo zenye neema



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 34

إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Hakika wachamungu watapata Kwa Mola wao Bustani za neema



Surah: ALMA’RIJ 

Ayah : 23

ٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ دَآئِمُونَ

Ambao wenye kudumisha Sala zao



Surah: ALMA’RIJ 

Ayah : 24

وَٱلَّذِينَ فِيٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ حَقّٞ مَّعۡلُومٞ

Na wale ambao katika Mali zao kuna haki maalumu



Surah: ALMA’RIJ 

Ayah : 25

لِّلسَّآئِلِ وَٱلۡمَحۡرُومِ

Kwa (Masikini) mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba



Surah: ALMA’RIJ 

Ayah : 26

وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na ambao wanasadikisha Siku ya Malipo, (siku ya Kiyama)



Surah: ALMA’RIJ 

Ayah : 27

وَٱلَّذِينَ هُم مِّنۡ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشۡفِقُونَ

Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao



Surah: ALMA’RIJ 

Ayah : 28

إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمۡ غَيۡرُ مَأۡمُونٖ

Hakika adhabu ya Mola wao si ya kusalimika nayo



Surah: ALMA’RIJ 

Ayah : 29

وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَٰفِظُونَ

Na ambao wanahifadhi tupu zao



Surah: ALMA’RIJ 

Ayah : 30

إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٰجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ فَإِنَّهُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ

Isipokuwa kwa wake zao, au wale iliyowamiliki mikono yao ya kuume, basi hao si wenye kulaumiwa



Surah: ALMA’RIJ 

Ayah : 31

فَمَنِ ٱبۡتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡعَادُونَ

Basi yeyote yule atakayetaka kinyume ya hayo, basi hao ndio warukao mipaka



Surah: ALMA’RIJ 

Ayah : 32

وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِأَمَٰنَٰتِهِمۡ وَعَهۡدِهِمۡ رَٰعُونَ

Na ambao amana zao na ahadi zao ni wenye kuzichunga (na kuzitimiza)



Surah: ALMA’RIJ 

Ayah : 33

وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَٰدَٰتِهِمۡ قَآئِمُونَ

Na ambao wanasimama imara katika kutoa ushahidi wao,



Surah: ALMA’RIJ 

Ayah : 34

وَٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ يُحَافِظُونَ

Na ambao kwenye Sala zao ni wenye kuzilinda



Surah: ALMA’RIJ 

Ayah : 35

أُوْلَـٰٓئِكَ فِي جَنَّـٰتٖ مُّكۡرَمُونَ

Hao ndio watakao heshimiwa Peponi



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 41

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ

Hakika wacha Mungu watakuwa katika vivuli na chemchem



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 42

وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ

Na matunda katika yale wanayoyatamani



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 43

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

(Wataabiwa): Kuleni na kunyweni kwa furaha kwasababu ya yale mliyokuwa mkiyatenda



Surah: ALMURSALAAT 

Ayah : 44

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakika sisi ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 40

وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ

Ama yule anayeogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake, na akaikataza nafsi yake na na matamanio



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 41

فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 22

إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٍ

Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 23

عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ

Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 24

تَعۡرِفُ فِي وُجُوهِهِمۡ نَضۡرَةَ ٱلنَّعِيمِ

Utatambua katika nyuso zao mng’aro wa neema,



Surah: AL-BURUJI 

Ayah : 11

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ لَهُمۡ جَنَّـٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡكَبِيرُ

Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa



Surah: AL-FAJRI 

Ayah : 27

يَـٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ

Ewe nafsi iliyo tua!