Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 31

وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ

Na maji yenye kumiminwa



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 32

وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ

Na matunda mengi



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 33

لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ

Hayana kikomo na wala hayakatazwi



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 34

وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ

Na matandiko ya kupumzikia yaliyoinuliwa



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 35

إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ

Hakika Sisi Tutawaumba (Mahurulaini) upya



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 36

فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا

Na tukawafanya kuwa bikra



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 37

عُرُبًا أَتۡرَابٗا

Wenye mahaba kwa waume zao, na wana umri unaolingana



Surah: AL-WAAQIA’H 

Ayah : 38

لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Ni kwaajili ya watu wa kuliani



Surah: AL-HADIID

Ayah : 21

سَابِقُوٓاْ إِلَىٰ مَغۡفِرَةٖ مِّن رَّبِّكُمۡ وَجَنَّةٍ عَرۡضُهَا كَعَرۡضِ ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِ أُعِدَّتۡ لِلَّذِينَ ءَامَنُواْ بِٱللَّهِ وَرُسُلِهِۦۚ ذَٰلِكَ فَضۡلُ ٱللَّهِ يُؤۡتِيهِ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ ذُو ٱلۡفَضۡلِ ٱلۡعَظِيمِ

Kimbilieni kuomba msamaha kwa Mola wenu na Pepo (ambayo) upana wake ni kama upana wa mbingu na ardhi, imeandaliwa kwa wale walio muamini Allah na Mtume Wake. Hiyo ni fadhila ya Allah, Humpa Amtakaye. Na Allah ni Mwenye fadhila kubwa



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 22

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ

Katika Bustani (Pepo) Iliyo Juu,



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 23

قُطُوفُهَا دَانِيَةٞ

Vishada Vyake (vya matunda) Vitakuwa Karibu:



Surah: AL-INSAAN

Ayah : 12

وَجَزَىٰهُم بِمَا صَبَرُواْ جَنَّةٗ وَحَرِيرٗا

Na Atawalipa kwasababu ya kusubiri kwao, Pepo na nguo za hariri



Surah: AL-INSAAN

Ayah : 13

مُّتَّكِـِٔينَ فِيهَا عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِۖ لَا يَرَوۡنَ فِيهَا شَمۡسٗا وَلَا زَمۡهَرِيرٗا

Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona (hawatahisi) humo jua kali wala baridi kali.[1]


1- - Aya ni dalili kuwa Akhera kuna adhabu ya Baridi. Kama alivyopokea Imamu Bukhariy na Muslim- kutoka kwa Abuu Hurairah (Allah amuwiye radhh) amesema; amesema Mtume wa Allah (Rehema na amani ziwe juu yake):-


Surah: AL-INSAAN

Ayah : 14

وَدَانِيَةً عَلَيۡهِمۡ ظِلَٰلُهَا وَذُلِّلَتۡ قُطُوفُهَا تَذۡلِيلٗا

Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning’inia mpaka chini



Surah: AL-INSAAN

Ayah : 15

وَيُطَافُ عَلَيۡهِم بِـَٔانِيَةٖ مِّن فِضَّةٖ وَأَكۡوَابٖ كَانَتۡ قَوَارِيرَا۠

Na watazungushiwa vyombo vya fedha, na bilauri zilokuwa za vigae



Surah: AL-INSAAN

Ayah : 16

قَوَارِيرَاْ مِن فِضَّةٖ قَدَّرُوهَا تَقۡدِيرٗا

Vigae safi kutokana na fedha wamezipima kwa kipimo



Surah: AL-INSAAN

Ayah : 17

وَيُسۡقَوۡنَ فِيهَا كَأۡسٗا كَانَ مِزَاجُهَا زَنجَبِيلًا

Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi



Surah: AL-INSAAN

Ayah : 18

عَيۡنٗا فِيهَا تُسَمَّىٰ سَلۡسَبِيلٗا

Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil



Surah: AL-INSAAN

Ayah : 19

۞وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ إِذَا رَأَيۡتَهُمۡ حَسِبۡتَهُمۡ لُؤۡلُؤٗا مَّنثُورٗا

Na watawazungukia wavulana wasio pevuka wakiwatumikia, ukiwaona utadhani ni lulu zilizo tawanywa



Surah: AL-INSAAN

Ayah : 20

وَإِذَا رَأَيۡتَ ثَمَّ رَأَيۡتَ نَعِيمٗا وَمُلۡكٗا كَبِيرًا

Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa



Surah: AL-INSAAN

Ayah : 21

عَٰلِيَهُمۡ ثِيَابُ سُندُسٍ خُضۡرٞ وَإِسۡتَبۡرَقٞۖ وَحُلُّوٓاْ أَسَاوِرَ مِن فِضَّةٖ وَسَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ شَرَابٗا طَهُورًا

Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya atilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao atawanywesha kinywaji safi kabisa



Surah: AL-INSAAN

Ayah : 22

إِنَّ هَٰذَا كَانَ لَكُمۡ جَزَآءٗ وَكَانَ سَعۡيُكُم مَّشۡكُورًا

(Wataambiwa) Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa



Surah: ANNABAI 

Ayah : 31

إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ مَفَازًا

Hakika wacha Mungu wanastahiki kufuzu



Surah: ANNABAI 

Ayah : 32

حَدَآئِقَ وَأَعۡنَٰبٗا

[watapata] Mabustani na mizabibu



Surah: ANNABAI 

Ayah : 33

وَكَوَاعِبَ أَتۡرَابٗا

Na wake wenye vifua vya kujaa, na walio lingana nao



Surah: ANNABAI 

Ayah : 34

وَكَأۡسٗا دِهَاقٗا

Na bilauri zilizo jaa,



Surah: ANNABAI 

Ayah : 35

لَّا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا كِذَّـٰبٗا

Hawatasikia humo upuuzi wala uongo



Surah: ANNABAI 

Ayah : 36

جَزَآءٗ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابٗا

Hali yakuwa ni Malipo kutoka kwa Mola wako, ni kipawa cha kutosha



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 25

يُسۡقَوۡنَ مِن رَّحِيقٖ مَّخۡتُومٍ

Watanyweshwa kinywaji safi kilichotiwa muhuri,



Surah: AL-MUTWAFFIFIIN 

Ayah : 26

خِتَٰمُهُۥ مِسۡكٞۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلۡيَتَنَافَسِ ٱلۡمُتَنَٰفِسُونَ

Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana