Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 17

ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nenda kwa Firauna, hakika yeye amepindukia mipaka



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 18

فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ

Umwambie: Je, unataka utakasike?



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 19

وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ

Na nikuongoze kwa Mola wako umuogope?



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 20

فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Basi akamuonyesha Ishara (muujiza) mkubwa kabisa



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 21

فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ

Lakini aliikadhibisha na akaasi



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 22

ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ

Kisha akageuka nyuma na kufanya juhudi, (ya kukanusha)



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 23

فَحَشَرَ فَنَادَىٰ

Akakusanya watu akatangaza



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 24

فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mkuu kabisa



Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 25

فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ

Basi hapo Allah akamshika na kumuadhibu kwa adhabu ya mwisho na mwanzo.[1]


1- - Allah akampa adhabu kwa kauli yake ya mwisho, nayo ni vile kusema: “Mimi ndiye Mola wenu Mlezi aliye mkubwa kabisa. Na akampa adhabu kwa kauli yake ya mwanzo, nayo ni kumkadhibisha Musa”.


Surah: ANNAAZIAAT 

Ayah : 26

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ

Hakika katika hayo bila shaka kuna funzo kwa yule anayeogopa