Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 42

قَالَ نَعَمۡ وَإِنَّكُمۡ إِذٗا لَّمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 43

قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلۡقُواْ مَآ أَنتُم مُّلۡقُونَ

Mussa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 44

فَأَلۡقَوۡاْ حِبَالَهُمۡ وَعِصِيَّهُمۡ وَقَالُواْ بِعِزَّةِ فِرۡعَوۡنَ إِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبُونَ

Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 45

فَأَلۡقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلۡقَفُ مَا يَأۡفِكُونَ

Mussa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 46

فَأُلۡقِيَ ٱلسَّحَرَةُ سَٰجِدِينَ

Hapo wachawi walipinduka wakasujudu



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 47

قَالُوٓاْ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 48

رَبِّ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ

Mola Mlezi wa Mussa na Harun



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 49

قَالَ ءَامَنتُمۡ لَهُۥ قَبۡلَ أَنۡ ءَاذَنَ لَكُمۡۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِي عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحۡرَ فَلَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيۡدِيَكُمۡ وَأَرۡجُلَكُم مِّنۡ خِلَٰفٖ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمۡ أَجۡمَعِينَ

(Firauni) akasema: Je! Mme-muamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutofautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 50

قَالُواْ لَا ضَيۡرَۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ

Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 51

إِنَّا نَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَٰيَٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 52

۞وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنۡ أَسۡرِ بِعِبَادِيٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ

Na tulimuamrisha Mussa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 53

فَأَرۡسَلَ فِرۡعَوۡنُ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 54

إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَشِرۡذِمَةٞ قَلِيلُونَ

(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 55

وَإِنَّهُمۡ لَنَا لَغَآئِظُونَ

Nao wanatuudhi



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 56

وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَٰذِرُونَ

Na sisi ni wengi, wenye kuchukua tahadhari



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 57

فَأَخۡرَجۡنَٰهُم مِّن جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 58

وَكُنُوزٖ وَمَقَامٖ كَرِيمٖ

Na makhazina, na vyeo vya heshima



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 59

كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ

Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 60

فَأَتۡبَعُوهُم مُّشۡرِقِينَ

Basi wakawafuata lilipo chomoza jua



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 61

فَلَمَّا تَرَـٰٓءَا ٱلۡجَمۡعَانِ قَالَ أَصۡحَٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدۡرَكُونَ

Na yalipoonana majeshi mawili haya, watu wa Mussa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 62

قَالَ كَلَّآۖ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهۡدِينِ

(Mussa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 63

فَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱضۡرِب بِّعَصَاكَ ٱلۡبَحۡرَۖ فَٱنفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرۡقٖ كَٱلطَّوۡدِ ٱلۡعَظِيمِ

Tulimletea wahyi Mussa tuka-mwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 64

وَأَزۡلَفۡنَا ثَمَّ ٱلۡأٓخَرِينَ

Na tukawajongeza hapo wale wengine



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 65

وَأَنجَيۡنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ

Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 66

ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawazamisha hao wengine



Surah: ASH-SHUARAA 

Ayah : 67

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini



Surah: ANNAMLI 

Ayah : 7

إِذۡ قَالَ مُوسَىٰ لِأَهۡلِهِۦٓ إِنِّيٓ ءَانَسۡتُ نَارٗا سَـَٔاتِيكُم مِّنۡهَا بِخَبَرٍ أَوۡ ءَاتِيكُم بِشِهَابٖ قَبَسٖ لَّعَلَّكُمۡ تَصۡطَلُونَ

(Kumbuka) Mussa alipo waambia ahali zake: Hakika nimeona moto, nitakwenda nikuleteeni khabari, au nitakuleteeni kijinga kinacho waka ili mpate kuota moto



Surah: ANNAMLI 

Ayah : 8

فَلَمَّا جَآءَهَا نُودِيَ أَنۢ بُورِكَ مَن فِي ٱلنَّارِ وَمَنۡ حَوۡلَهَا وَسُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Basi alipo fika ilinadiwa: Amebarikiwa aliomo katika moto huu na walioko pembezoni mwake. Na ametakasika Allah, Mola Mlezi wa walimwengu wote



Surah: ANNAMLI 

Ayah : 9

يَٰمُوسَىٰٓ إِنَّهُۥٓ أَنَا ٱللَّهُ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Ewe Mussa! Hakika Mimi ndiye Allah, Mwenye nguvu, Mwenye hekima



Surah: ANNAMLI 

Ayah : 10

وَأَلۡقِ عَصَاكَۚ فَلَمَّا رَءَاهَا تَهۡتَزُّ كَأَنَّهَا جَآنّٞ وَلَّىٰ مُدۡبِرٗا وَلَمۡ يُعَقِّبۡۚ يَٰمُوسَىٰ لَا تَخَفۡ إِنِّي لَا يَخَافُ لَدَيَّ ٱلۡمُرۡسَلُونَ

Na itupe fimbo yako! Alipoiona ikitikisika kama nyoka, aligeuka nyuma wala hakungoja. Ewe Mussa! Usikhofu! Hakika hawakhofu mbele yangu Mitume