Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 154

وَلَا تَقُولُواْ لِمَن يُقۡتَلُ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ أَمۡوَٰتُۢۚ بَلۡ أَحۡيَآءٞ وَلَٰكِن لَّا تَشۡعُرُونَ

Na msiseme kuwa, waliouawa katika njia ya Allah ni wafu. Bali wapo hai, lakini hamtambui



Surah: AL-IMRAN 

Ayah : 140

إِن يَمۡسَسۡكُمۡ قَرۡحٞ فَقَدۡ مَسَّ ٱلۡقَوۡمَ قَرۡحٞ مِّثۡلُهُۥۚ وَتِلۡكَ ٱلۡأَيَّامُ نُدَاوِلُهَا بَيۡنَ ٱلنَّاسِ وَلِيَعۡلَمَ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَيَتَّخِذَ مِنكُمۡ شُهَدَآءَۗ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Ikiwa yamekupateni majeraha, basi kwa hakika watu walipata majeraha kama hayo. Na hizo ni siku tunazizungusha kwa zamu kwa watu ili Allah awabainishe wale walioamini na afanye Mashahidi miongoni mwenu, na Allah hawapendi madhalimu



Surah: AL-IMRAN 

Ayah : 157

وَلَئِن قُتِلۡتُمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ أَوۡ مُتُّمۡ لَمَغۡفِرَةٞ مِّنَ ٱللَّهِ وَرَحۡمَةٌ خَيۡرٞ مِّمَّا يَجۡمَعُونَ

Na ikiwa mtauliwa katika njia ya Allah au mkifa, hakika msamaha na rehema zitokazo kwa Allah ni bora kuliko yote wanayoyakusanya



Surah: AL-IMRAN 

Ayah : 158

وَلَئِن مُّتُّمۡ أَوۡ قُتِلۡتُمۡ لَإِلَى ٱللَّهِ تُحۡشَرُونَ

Na mkifa au mkiuliwa ni kwa Allah tu mtakusanywa



Surah: AL-IMRAN 

Ayah : 169

وَلَا تَحۡسَبَنَّ ٱلَّذِينَ قُتِلُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ أَمۡوَٰتَۢاۚ بَلۡ أَحۡيَآءٌ عِندَ رَبِّهِمۡ يُرۡزَقُونَ

Na kamwe msiwadhanie waliouliwa katika njia ya Allah kuwa ni wafu, bali wako hai kwa Mola wao wanaruzukiwa



Surah: AL-IMRAN 

Ayah : 170

فَرِحِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمُ ٱللَّهُ مِن فَضۡلِهِۦ وَيَسۡتَبۡشِرُونَ بِٱلَّذِينَ لَمۡ يَلۡحَقُواْ بِهِم مِّنۡ خَلۡفِهِمۡ أَلَّا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Wanafurahia waliyopewa na Allah miongoni mwa fadhila zake, na wanawabashiria walio nyuma yao ambao bado hawajajiunga nao, ya kwamba: Hakutakuwa na khofu yoyote juu yao, na wala hawatahuzunika



Surah: AL-IMRAN 

Ayah : 171

۞يَسۡتَبۡشِرُونَ بِنِعۡمَةٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَفَضۡلٖ وَأَنَّ ٱللَّهَ لَا يُضِيعُ أَجۡرَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Wanawapa bishara ya neema zitokanazo kwa Mola wao na fadhila na hakika Allah hapotezi malipo ya waumini



Surah: AL-IMRAN 

Ayah : 195

فَٱسۡتَجَابَ لَهُمۡ رَبُّهُمۡ أَنِّي لَآ أُضِيعُ عَمَلَ عَٰمِلٖ مِّنكُم مِّن ذَكَرٍ أَوۡ أُنثَىٰۖ بَعۡضُكُم مِّنۢ بَعۡضٖۖ فَٱلَّذِينَ هَاجَرُواْ وَأُخۡرِجُواْ مِن دِيَٰرِهِمۡ وَأُوذُواْ فِي سَبِيلِي وَقَٰتَلُواْ وَقُتِلُواْ لَأُكَفِّرَنَّ عَنۡهُمۡ سَيِّـَٔاتِهِمۡ وَلَأُدۡخِلَنَّهُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ ثَوَابٗا مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِۚ وَٱللَّهُ عِندَهُۥ حُسۡنُ ٱلثَّوَابِ

Mola wao akawajibu: Mimi sipotezi tendo la mtendaji yeyote miongoni mwenu awe mwanaume au mwanamke nyinyi kwa nyinyi, basi wale waliohama na wakatolewa majumbani mwao na wakaudhiwa na kukerwa katika njia yangu, na wakapigana na wakauliwa naapa nitawafutia makosa yao na naapa nitawaingiza katika Pepo inayotiririka chini yake mito ikiwa malipo kutoka kwa Allah, na kwa Allah ndiko kuliko na malipo mazuri



Surah: ANNISAI 

Ayah : 69

وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ مَعَ ٱلَّذِينَ أَنۡعَمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ وَٱلصِّدِّيقِينَ وَٱلشُّهَدَآءِ وَٱلصَّـٰلِحِينَۚ وَحَسُنَ أُوْلَـٰٓئِكَ رَفِيقٗا

Na wenye kumtii Allah na Mtume, basi hao watakuwa pamoja na wale ambao Allah amewaneemesha ikiwa ni pamoja na Manabii na Wenye kusadikisha (Maswahaba) na Mashahidi na Watu Wema.[1] Na ni uzuri ulioje kuwa pamoja na watu hao!


1- - Aya hapa inawabainisha walioneemeshwa na ambao katika Aya ya 6 na ya 7 ya Sura Alfaatiha (1) Waislamu wametakiwa kuwaiga na kufuata njia, muongozo na sera zao. Swahaba, wakiongozwa na Abubakar, Umar, Uthman na Ali (Allah awawie radhi) wanahusika katika Aya hii kwa sababu kuna Hadithi kadhaa za Mtume (Allah amshushie rehema na amani, zinazowataja kuwa wamo Mashahidi na Wasadikishaji.


Surah: ANNISAI 

Ayah : 74

۞فَلۡيُقَٰتِلۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ ٱلَّذِينَ يَشۡرُونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا بِٱلۡأٓخِرَةِۚ وَمَن يُقَٰتِلۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ فَيُقۡتَلۡ أَوۡ يَغۡلِبۡ فَسَوۡفَ نُؤۡتِيهِ أَجۡرًا عَظِيمٗا

Basi wapigane katika njia ya Allah wale ambao wanauza uhai (wao) wa duniani kwa Akhera. Na yeyote anayepigana katika njia ya Allah kisha akauliwa au akashinda, basi ni punde tu tutampa malipo makubwa



Surah: AL-HAJJ 

Ayah : 58

وَٱلَّذِينَ هَاجَرُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ ثُمَّ قُتِلُوٓاْ أَوۡ مَاتُواْ لَيَرۡزُقَنَّهُمُ ٱللَّهُ رِزۡقًا حَسَنٗاۚ وَإِنَّ ٱللَّهَ لَهُوَ خَيۡرُ ٱلرَّـٰزِقِينَ

Na walio hama kwa ajili ya Allah, kisha wakauwawa au wakafa, bila ya shaka Allah atawaruzuku riziki njema. Na hakika Allah ni Mbora wa wanao ruzuku



Surah: AL-HAJJ 

Ayah : 59

لَيُدۡخِلَنَّهُم مُّدۡخَلٗا يَرۡضَوۡنَهُۥۚ وَإِنَّ ٱللَّهَ لَعَلِيمٌ حَلِيمٞ

Bila ya shaka atawaingiza pahala watakapo paridhia. Na hakika Allah ni Mjuzi na Mpole



Surah: MUHAMMAD 

Ayah : 4

فَإِذَا لَقِيتُمُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فَضَرۡبَ ٱلرِّقَابِ حَتَّىٰٓ إِذَآ أَثۡخَنتُمُوهُمۡ فَشُدُّواْ ٱلۡوَثَاقَ فَإِمَّا مَنَّۢا بَعۡدُ وَإِمَّا فِدَآءً حَتَّىٰ تَضَعَ ٱلۡحَرۡبُ أَوۡزَارَهَاۚ ذَٰلِكَۖ وَلَوۡ يَشَآءُ ٱللَّهُ لَٱنتَصَرَ مِنۡهُمۡ وَلَٰكِن لِّيَبۡلُوَاْ بَعۡضَكُم بِبَعۡضٖۗ وَٱلَّذِينَ قُتِلُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ فَلَن يُضِلَّ أَعۡمَٰلَهُمۡ

Basi mnapo wakuta walio kufuru wapigeni shingoni mwao, mpaka mkiwadhoofisha wafungeni pingu. Tena waachilieni kwa hisani au wajikomboe, mpaka vita vipoe. Ndio hivyo. Na lau Allah angelitaka angeli washinda mwenyewe, lakini haya ni kwasababu akutieni mitihani nyinyi kwa nyinyi. Na waliouliwa katika njia ya Allah hatazipoteza amali zao



Surah: AL-HADIID

Ayah : 19

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ بِٱللَّهِ وَرُسُلِهِۦٓ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلصِّدِّيقُونَۖ وَٱلشُّهَدَآءُ عِندَ رَبِّهِمۡ لَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ وَنُورُهُمۡۖ وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَآ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَحِيمِ

Na wale waliomwamini Allah na Mtume Wake, hao ndio waliosadikisha na Mashahidi mbele ya Mola wao. Watapa ujira wao na nuru yao. Na wale waliokufuru na wakakadhibisha Aya Zetu hao ni watu wa motoni