Surah: A’BASA

Ayah : 25

أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا

Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu



Surah: A’BASA

Ayah : 26

ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا

Kisha Tukaipasua ardhi mipasuko



Surah: A’BASA

Ayah : 27

فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا

Kisha tukaotesha humo nafaka mbali mbali



Surah: A’BASA

Ayah : 28

وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا

Na mizabibu na mimea ya mboga (ikatwayo ikamea tena)



Surah: A’BASA

Ayah : 29

وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا

Na mizaituni na mitende



Surah: A’BASA

Ayah : 30

وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا

Na mabustani yaliyositawi na kusongamana miti yake



Surah: A’BASA

Ayah : 31

وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا

Na matunda na majani ya malisho ya wanyama



Surah: A’BASA

Ayah : 32

مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ

Ni manufaa kwenu na kwa wanyama wenu wa mifugo



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 5

فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ

Hebu na ajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 6

خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ

Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 7

يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ

Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu



Surah: ATTAARIQ 

Ayah : 8

إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ

Hakika Yeye ana uwezo wa kumrudisha



Surah:  AL-GHAASHIYAH 

Ayah : 17

أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ

Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?



Surah:  AL-GHAASHIYAH 

Ayah : 18

وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ

Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?



Surah:  AL-GHAASHIYAH 

Ayah : 19

وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ

Na milima jinsi ilivyo thibitishwa (simamishwa)?



Surah:  AL-GHAASHIYAH 

Ayah : 20

وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ

Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?



Surah: AL-A’LAQ 

Ayah : 1

ٱقۡرَأۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلَّذِي خَلَقَ

Soma kwa jina la Mola wako Mlezi ambaye ameumba