Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 42

وَلَا تَلۡبِسُواْ ٱلۡحَقَّ بِٱلۡبَٰطِلِ وَتَكۡتُمُواْ ٱلۡحَقَّ وَأَنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Na msichanganye haki na batili na msifiche haki na ilhali mnajua



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 140

أَمۡ تَقُولُونَ إِنَّ إِبۡرَٰهِـۧمَ وَإِسۡمَٰعِيلَ وَإِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ وَٱلۡأَسۡبَاطَ كَانُواْ هُودًا أَوۡ نَصَٰرَىٰۗ قُلۡ ءَأَنتُمۡ أَعۡلَمُ أَمِ ٱللَّهُۗ وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّن كَتَمَ شَهَٰدَةً عِندَهُۥ مِنَ ٱللَّهِۗ وَمَا ٱللَّهُ بِغَٰفِلٍ عَمَّا تَعۡمَلُونَ

Au mnasema kuwa, Ibrahimu na Ismaili na Isihaka na Yakubu na watoto wake walikuwa Wayahudi au Wanaswara? Sema: Hivi nyinyi ndio wajuzi zaidi au Allah? Na ni nani aliyedhalimu mno kuliko yule aliyeuficha ushahidi alionao kutoka kwa Allah? Na Allah si mwenye kughafilika na yote mnayoyafanya



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 159

إِنَّ ٱلَّذِينَ يَكۡتُمُونَ مَآ أَنزَلۡنَا مِنَ ٱلۡبَيِّنَٰتِ وَٱلۡهُدَىٰ مِنۢ بَعۡدِ مَا بَيَّنَّـٰهُ لِلنَّاسِ فِي ٱلۡكِتَٰبِ أُوْلَـٰٓئِكَ يَلۡعَنُهُمُ ٱللَّهُ وَيَلۡعَنُهُمُ ٱللَّـٰعِنُونَ

Hakika, wale wanaoficha hoja za wazi na muongozo tuliouteremsha baada ya kuwa tumeubainisha kwa watu kitabuni, hao Allah anawalaani na pia wanalaaniwa na wenye kulaani



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 174

إِنَّ ٱلَّذِينَ يَكۡتُمُونَ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَيَشۡتَرُونَ بِهِۦ ثَمَنٗا قَلِيلًا أُوْلَـٰٓئِكَ مَا يَأۡكُلُونَ فِي بُطُونِهِمۡ إِلَّا ٱلنَّارَ وَلَا يُكَلِّمُهُمُ ٱللَّهُ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ وَلَا يُزَكِّيهِمۡ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٌ

Hakika, wale wanaoficha yaliyoteremshwa na Allah katika kitabu, na kufadhilisha kwayo thamani ndogo, hao hawali matumboni mwao isipokuwa moto tu, wala Allah hatawasemeza Siku ya Kiyama wala hatawatakasa; na watapata adhabu iumizayo



Surah: AL-IMRAN 

Ayah : 137

قَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِكُمۡ سُنَنٞ فَسِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَٱنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُكَذِّبِينَ

Yamepita kabla yenu mataifa (mengi)[1], basi tembeeni ardhini na muone ulikuwaje mwisho wa wanaokanusha (muongozo wa Allah)


1- - Makusudio hapa ni kuwakumbusha Waislamu kuwa, yamepita mataifa mengi yaliyokuwa na tabia na
nyendo za kupinga muongozo wa Allah na hatimae kuadhibiwa kwa adhabu za aina tafauti tafauti.
Waislamu hapa wanatakiwa kuyatembelea maeneo ya mataifa yaliyopita na ambayo yaliadhibiwa kwa
kutafakari na pia kwa kuona kwa macho lengo likiwa kupata maonyo na mafunzo na sio kutalii na
kuburudika.


Surah: AL-IMRAN 

Ayah : 187

وَإِذۡ أَخَذَ ٱللَّهُ مِيثَٰقَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ لَتُبَيِّنُنَّهُۥ لِلنَّاسِ وَلَا تَكۡتُمُونَهُۥ فَنَبَذُوهُ وَرَآءَ ظُهُورِهِمۡ وَٱشۡتَرَوۡاْ بِهِۦ ثَمَنٗا قَلِيلٗاۖ فَبِئۡسَ مَا يَشۡتَرُونَ

Na kumbuka pale Allah alipochukua ahadi nzito, kwa ambao wamepewa kitabu kuwa lazima mtakibainisha kwa watu na hamtakificha, wakaitupa ahadi hiyo nyuma ya migongo yao, wakiuza ahadi kwa thamani ndogo, basi biashara mbaya ni hiyo waliyoifanya



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 11

قُلۡ سِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ ثُمَّ ٱنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُكَذِّبِينَ

Sema: Tembeeni ardhini kisha tazameni namna ulivyokuwa mwisho wa wenye kukadhibisha (wenye kupinga)



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 99

وَهُوَ ٱلَّذِيٓ أَنزَلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَخۡرَجۡنَا بِهِۦ نَبَاتَ كُلِّ شَيۡءٖ فَأَخۡرَجۡنَا مِنۡهُ خَضِرٗا نُّخۡرِجُ مِنۡهُ حَبّٗا مُّتَرَاكِبٗا وَمِنَ ٱلنَّخۡلِ مِن طَلۡعِهَا قِنۡوَانٞ دَانِيَةٞ وَجَنَّـٰتٖ مِّنۡ أَعۡنَابٖ وَٱلزَّيۡتُونَ وَٱلرُّمَّانَ مُشۡتَبِهٗا وَغَيۡرَ مُتَشَٰبِهٍۗ ٱنظُرُوٓاْ إِلَىٰ ثَمَرِهِۦٓ إِذَآ أَثۡمَرَ وَيَنۡعِهِۦٓۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكُمۡ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ

Na yeye ndiye aliyeteremsha maji (mvua) kutoka mawinguni, basi kwa maji hayo tukatoa (tukaotesha) mimea ya kila kitu (aina). Tumetoa humo mimea ya kijani (ambapo) tunatoa kutokana na hiyo (mimea ya kijani) punje zilizopandana. Na katika mitende katika makole yake yapo yaliyoinama, na bustani za mizabibu na mizaituni na makomamanga yaliyofanana na yasiyofanana. Angalieni matunda yake yanapozaa na yanapoiva. Hakika, katika hayo kuna alama (mazingatio) kwa wanaoamini



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 86

وَلَا تَقۡعُدُواْ بِكُلِّ صِرَٰطٖ تُوعِدُونَ وَتَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ مَنۡ ءَامَنَ بِهِۦ وَتَبۡغُونَهَا عِوَجٗاۚ وَٱذۡكُرُوٓاْ إِذۡ كُنتُمۡ قَلِيلٗا فَكَثَّرَكُمۡۖ وَٱنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُفۡسِدِينَ

Na msikae kwenye kila njia (msiwe kikwazo) mkitisha (watu) na kuwazuia wale walioiamini njia ya Allah wasiifuate, na mkitaka njia hiyo ipinde. Na kumbukeni mlipokuwa wachache, basi (Allah) akakufanyeni wengi, na tazameni; ulikuwaje mwisho wa waharibifu?



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 185

أَوَلَمۡ يَنظُرُواْ فِي مَلَكُوتِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا خَلَقَ ٱللَّهُ مِن شَيۡءٖ وَأَنۡ عَسَىٰٓ أَن يَكُونَ قَدِ ٱقۡتَرَبَ أَجَلُهُمۡۖ فَبِأَيِّ حَدِيثِۭ بَعۡدَهُۥ يُؤۡمِنُونَ

Hivi hawautafakari ufalme (mkubwa) wa mbinguni na ardhini na vitu vyote (vingine) ambavyo Allah ameviumba na kwamba inawezekana kuwa muda wao utakuwa umekaribia? Basi ni mazungumzo gani tena baada ya haya watayaamini?



Surah: ATTAUBA 

Ayah : 122

۞وَمَا كَانَ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ لِيَنفِرُواْ كَآفَّةٗۚ فَلَوۡلَا نَفَرَ مِن كُلِّ فِرۡقَةٖ مِّنۡهُمۡ طَآئِفَةٞ لِّيَتَفَقَّهُواْ فِي ٱلدِّينِ وَلِيُنذِرُواْ قَوۡمَهُمۡ إِذَا رَجَعُوٓاْ إِلَيۡهِمۡ لَعَلَّهُمۡ يَحۡذَرُونَ

Na hawakutakiwa Waumini watoke wote (kwenda vitani). Basi kwa nini hawatoki baadhi katika kila kundi miongoni mwao, wakajifunze vyema Dini, na kisha waje kuwaonya wenzao watakaporejea kwao, ili nao wapate kujihadhari?



Surah: YUNUS 

Ayah : 101

قُلِ ٱنظُرُواْ مَاذَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَمَا تُغۡنِي ٱلۡأٓيَٰتُ وَٱلنُّذُرُ عَن قَوۡمٖ لَّا يُؤۡمِنُونَ

Sema: Tazameni; kuna nini mbinguni na ardhini? Na Aya na maonyo hayawasaidii watu wasioamini



Surah: YUSUF 

Ayah : 109

وَمَآ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ إِلَّا رِجَالٗا نُّوحِيٓ إِلَيۡهِم مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡقُرَىٰٓۗ أَفَلَمۡ يَسِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَيَنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۗ وَلَدَارُ ٱلۡأٓخِرَةِ خَيۡرٞ لِّلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Na hatukutuma kabla yako isipokuwa (Mitume) wanaume tunaowafunulia (tunaowashushia Wahyi) miongoni mwa watu wa mijini. Je, hivi hawatembei katika ardhi wakaona jinsi ulivyokuwa mwisho wa waliokuwa kabla yao? Na hakika, nyumba ya Akhera ni bora kwa wanaomcha Allah. Basi hamtumii akili?



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 36

وَلَقَدۡ بَعَثۡنَا فِي كُلِّ أُمَّةٖ رَّسُولًا أَنِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ وَٱجۡتَنِبُواْ ٱلطَّـٰغُوتَۖ فَمِنۡهُم مَّنۡ هَدَى ٱللَّهُ وَمِنۡهُم مَّنۡ حَقَّتۡ عَلَيۡهِ ٱلضَّلَٰلَةُۚ فَسِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَٱنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُكَذِّبِينَ

Na bila shaka tulipeleka Mtume katika kila umma wakawaambia kwamba: Muabuduni Allah (peke yake) na epukeni (kuabudu) Twaghuti[1]. Basi miongoni mwao Allah amewaongoza (njia sahihi ya Uislamu), na miongoni mwao umewathibitikia upotevu. Basi tembeeni (nendeni) ardhini na muangalie vipi ulikuwa mwisho wa wakadhibishaji


1- - Twaghuti ni kitu chochote kinachoabudiwa badala ya Allah kama sanamu, mawe shetani n.k.


Surah: ANNAHLI 

Ayah : 43

وَمَآ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ إِلَّا رِجَالٗا نُّوحِيٓ إِلَيۡهِمۡۖ فَسۡـَٔلُوٓاْ أَهۡلَ ٱلذِّكۡرِ إِن كُنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ

Na hatukutuma kabla yako (ewe Muhammad) isipokuwa (Mitume) wanaume ambao tuliwapa wah-yi (ufunuo) basi (ikiwa enyi Washirikina hamuamini) waulizeni watunzaji wa vitabu vitakatifu (watakuelezeni) ikiwa ninyi hamjui



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 44

بِٱلۡبَيِّنَٰتِ وَٱلزُّبُرِۗ وَأَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ٱلذِّكۡرَ لِتُبَيِّنَ لِلنَّاسِ مَا نُزِّلَ إِلَيۡهِمۡ وَلَعَلَّهُمۡ يَتَفَكَّرُونَ

(Tuliwatuma) wakiwa na dalili za wazi. Na tumekuteremshia (ewe Muhammad) ukumbusho (Qur’ani) ili uwabainishie watu (kilichojificha katika maana na hukumu zake), na ili wapate kutafakari



Surah: TWAHA 

Ayah : 114

فَتَعَٰلَى ٱللَّهُ ٱلۡمَلِكُ ٱلۡحَقُّۗ وَلَا تَعۡجَلۡ بِٱلۡقُرۡءَانِ مِن قَبۡلِ أَن يُقۡضَىٰٓ إِلَيۡكَ وَحۡيُهُۥۖ وَقُل رَّبِّ زِدۡنِي عِلۡمٗا

Ametukuka Allah, Mfalme wa Haki. Wala usiifanyie haraka hii Qur’ani, kabla haujamalizika ufunuo wake. Na sema: Mola wangu Mlezi! Nizidishie ilimu



Surah: ALFURQAAN 

Ayah : 59

ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَا فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰ عَلَى ٱلۡعَرۡشِۖ ٱلرَّحۡمَٰنُ فَسۡـَٔلۡ بِهِۦ خَبِيرٗا

Ambaye ameziumba mbingu na ardhi, na viliomo ndani yake kwa siku sita. Kisha akatawala juu ya A’rshi, Arrahman, Mwingi wa Rehema! Uliza khabari zake kwa wamjuaye



Surah: AL-QASWAS 

Ayah : 69

وَرَبُّكَ يَعۡلَمُ مَا تُكِنُّ صُدُورُهُمۡ وَمَا يُعۡلِنُونَ

Na Mola wako Mlezi anayajua yaliyo ficha vifua vyao, na wanayo yatangaza



Surah: AL-ANKABUUT 

Ayah : 20

قُلۡ سِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَٱنظُرُواْ كَيۡفَ بَدَأَ ٱلۡخَلۡقَۚ ثُمَّ ٱللَّهُ يُنشِئُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأٓخِرَةَۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ

Sema: Tembeeni katika ardhi na tazameni jinsi alivyoanzisha uumbaji; kisha Allah ndiye anaye umba umbo la baadaye. Hakika Allah ni Muweza juu ya kila kitu



Surah: ARRUUM 

Ayah : 9

أَوَلَمۡ يَسِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَيَنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۚ كَانُوٓاْ أَشَدَّ مِنۡهُمۡ قُوَّةٗ وَأَثَارُواْ ٱلۡأَرۡضَ وَعَمَرُوهَآ أَكۡثَرَ مِمَّا عَمَرُوهَا وَجَآءَتۡهُمۡ رُسُلُهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِۖ فَمَا كَانَ ٱللَّهُ لِيَظۡلِمَهُمۡ وَلَٰكِن كَانُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ يَظۡلِمُونَ

Je! Hawatembei katika ardhi wakaona ulivyo kuwa mwisho wa walio kuwa kabla yao? Nao walikuwa na nguvu zaidi kuliko wao, na wakailima ardhi na wakaistawisha zaidi kuliko walivyo istawisha wao. Na Mitume wao wakawajia na dalili zilizo wazi. Basi hakuwa Allah ni mwenye kuwadhulumu, lakini walikuwa wakijidhulumu nafsi zao



Surah: ARRUUM 

Ayah : 42

قُلۡ سِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَٱنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلُۚ كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّشۡرِكِينَ

Sema: Safirini duniani muangalie ulikuwaje mwisho wa waliotangulia. Wengi wao walikuwa washirikina



Surah: FAATWIR 

Ayah : 44

أَوَلَمۡ يَسِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَيَنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ وَكَانُوٓاْ أَشَدَّ مِنۡهُمۡ قُوَّةٗۚ وَمَا كَانَ ٱللَّهُ لِيُعۡجِزَهُۥ مِن شَيۡءٖ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَلَا فِي ٱلۡأَرۡضِۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَلِيمٗا قَدِيرٗا

Je! Hawakusafiri katika ardhi wakaona vipi ulikuwa mwisho wa walio kuwa kabla yao? Na hao walikuwa wana nguvu zaidi kuliko wao. Na hapana kitu kinacho weza kumshinda Allah mbinguni wala katika ardhi. Hakika Yeye ni Mwenye kujua, Mwenye uweza



Surah: AZZUMAR 

Ayah : 9

أَمَّنۡ هُوَ قَٰنِتٌ ءَانَآءَ ٱلَّيۡلِ سَاجِدٗا وَقَآئِمٗا يَحۡذَرُ ٱلۡأٓخِرَةَ وَيَرۡجُواْ رَحۡمَةَ رَبِّهِۦۗ قُلۡ هَلۡ يَسۡتَوِي ٱلَّذِينَ يَعۡلَمُونَ وَٱلَّذِينَ لَا يَعۡلَمُونَۗ إِنَّمَا يَتَذَكَّرُ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَٰبِ

Je! Afanyae ibada nyakati za usiku kwa kusujudu na kusimama akitahadhari na Akhera, na akitaraji rehema za Mola wake Mlezi... Sema: Ati watakuwa sawa wale wanao jua na wale wasio jua? Hakika wanao kumbuka ni watu wenye akili



Surah: GHAAFIR 

Ayah : 21

۞أَوَلَمۡ يَسِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَيَنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلَّذِينَ كَانُواْ مِن قَبۡلِهِمۡۚ كَانُواْ هُمۡ أَشَدَّ مِنۡهُمۡ قُوَّةٗ وَءَاثَارٗا فِي ٱلۡأَرۡضِ فَأَخَذَهُمُ ٱللَّهُ بِذُنُوبِهِمۡ وَمَا كَانَ لَهُم مِّنَ ٱللَّهِ مِن وَاقٖ

Kwani hawatembei katika ardhi wakaona jinsi ulivyo kuwa mwisho wa walio kuwa kabla yao? Hao walikuwa wamewazidi hawa kwa nguvu na athari katika nchi. Na Allah aliwatia mkononi kwasababu ya madhambi yao. Na wala hapakuwa na wakuwalinda na Allah



Surah: GHAAFIR 

Ayah : 82

أَفَلَمۡ يَسِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَيَنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۚ كَانُوٓاْ أَكۡثَرَ مِنۡهُمۡ وَأَشَدَّ قُوَّةٗ وَءَاثَارٗا فِي ٱلۡأَرۡضِ فَمَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ

Kwani hawatembei katika ardhi wakaona ulikuwaje mwisho wa walio kuwa kabla yao? Wao walikuwa wengi kuliko hawa, na wamewashinda kwa nguvu na athari katika nchi. Wala hayakuwafaa hayo waliyo kuwa wakiyachuma



Surah: MUHAMMAD 

Ayah : 10

۞أَفَلَمۡ يَسِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَيَنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۖ دَمَّرَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡۖ وَلِلۡكَٰفِرِينَ أَمۡثَٰلُهَا

Kwani hawakutembea katika ardhi wakaona ulikuwaje mwisho wa walio kuwa kabla yao? Allah aliwaangamiza, na kwa makafiri hawa itakuwa mfano wa hayo



Surah: QAAF 

Ayah : 6

أَفَلَمۡ يَنظُرُوٓاْ إِلَى ٱلسَّمَآءِ فَوۡقَهُمۡ كَيۡفَ بَنَيۡنَٰهَا وَزَيَّنَّـٰهَا وَمَا لَهَا مِن فُرُوجٖ

Je, hawatazami mbingu juu yao, vipi Tumezijenga na Tumezipamba, na wala hazina mipasuko yoyote



Surah: AL-MUJAADILA 

Ayah : 11

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا قِيلَ لَكُمۡ تَفَسَّحُواْ فِي ٱلۡمَجَٰلِسِ فَٱفۡسَحُواْ يَفۡسَحِ ٱللَّهُ لَكُمۡۖ وَإِذَا قِيلَ ٱنشُزُواْ فَٱنشُزُواْ يَرۡفَعِ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنكُمۡ وَٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡعِلۡمَ دَرَجَٰتٖۚ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ

Enyi walioamini! Mnapoambiwa: Fanyeni nafasi katika mabaraza, basi fanyeni nafasi; Allah Atakufanyieni nafasi. Na mnapoambiwa: Inukeni, basi inukeni; Allah Atawainua wale walioamini miongoni mwenu na waliopewa elimu daraja za juu. Na Allah kwa yale myatendayo ni Mwenye khabari nayo



Surah: A’BASA

Ayah : 24

فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ

Basi atazame mwanaadam chakula chake