Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 134

تِلۡكَ أُمَّةٞ قَدۡ خَلَتۡۖ لَهَا مَا كَسَبَتۡ وَلَكُم مَّا كَسَبۡتُمۡۖ وَلَا تُسۡـَٔلُونَ عَمَّا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Huo ni umma umeshapita. Utapata ulicho kichuma na nyinyi mtapata mlicho kichuma. Na hamtaulizwa kuhusu waliyokuwa wakiyafanya



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 141

تِلۡكَ أُمَّةٞ قَدۡ خَلَتۡۖ لَهَا مَا كَسَبَتۡ وَلَكُم مَّا كَسَبۡتُمۡۖ وَلَا تُسۡـَٔلُونَ عَمَّا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Huo ni umma umeshapita. Utapata ulichokichuma na nyinyi mtapata mlichokichuma. Na hamtaulizwa kuhusu waliyokuwa wakiyafanya



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 284

لِّلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۗ وَإِن تُبۡدُواْ مَا فِيٓ أَنفُسِكُمۡ أَوۡ تُخۡفُوهُ يُحَاسِبۡكُم بِهِ ٱللَّهُۖ فَيَغۡفِرُ لِمَن يَشَآءُ وَيُعَذِّبُ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ

Ni vya Allah tu vyote vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Na kama mkidhihirisha yaliyomo katika nyoyo zenu, au mkiyaficha, Allah atakuhojini kwayo; kwahiyo atamsamehe amtakaye, na atamuadhibu amtakaye. Na Allah ni Mwenye uweza mno wa kila kitu



Surah: AL-IMRAN 

Ayah : 199

وَإِنَّ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ لَمَن يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكُمۡ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡهِمۡ خَٰشِعِينَ لِلَّهِ لَا يَشۡتَرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ ثَمَنٗا قَلِيلًاۚ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ

Na kwa hakika katika Watu wa kitabu wapo wanaomuamini Allah hasa na kilichoteremshwa kwenu na kilichoteremshwa kwao, huku wakinyenyekea kwa Allah. Hawauzi Aya za Allah kwa thamani ndogo (ya dunia). Hao malipo yao yako kwa Mola wao mlezi, hakika Allah ni mwepesi mno wa kuhesabu



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 62

ثُمَّ رُدُّوٓاْ إِلَى ٱللَّهِ مَوۡلَىٰهُمُ ٱلۡحَقِّۚ أَلَا لَهُ ٱلۡحُكۡمُ وَهُوَ أَسۡرَعُ ٱلۡحَٰسِبِينَ

Kisha watarudishwa kwa Allah, Mola wao wa haki. Ehee, elewa kwamba, hukumu ni yake yeye (Allah) tu, na yeye ni Mwepesi sana wa wanaohesabu



Surah: AR-RA’D 

Ayah : 21

وَٱلَّذِينَ يَصِلُونَ مَآ أَمَرَ ٱللَّهُ بِهِۦٓ أَن يُوصَلَ وَيَخۡشَوۡنَ رَبَّهُمۡ وَيَخَافُونَ سُوٓءَ ٱلۡحِسَابِ

Na wale (wenye akili ndio) ambao huyaunga aliyoamrisha Allah yaungwe, na wanaihofu hesabu mbaya



Surah: AR-RA’D 

Ayah : 41

أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ أَنَّا نَأۡتِي ٱلۡأَرۡضَ نَنقُصُهَا مِنۡ أَطۡرَافِهَاۚ وَٱللَّهُ يَحۡكُمُ لَا مُعَقِّبَ لِحُكۡمِهِۦۚ وَهُوَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ

Je, (watu wa Makkah na wengine) hawaoni tunavyo ipunguza ardhi (wanayoishi) nchani mwake?[1] Na Allah anahukumu, na hapana wa kupinga hukumu yake, naye ni Mwepesi wa kuhesabu


1- - Kusudio la kupunguzwa kwa ardhi hapa, ni pamoja na kuangamizwa na kutawaliwa na Waislamu baadhi
ya mipaka au maeneo yake.


Surah: IBRAHIM 

Ayah : 51

لِيَجۡزِيَ ٱللَّهُ كُلَّ نَفۡسٖ مَّا كَسَبَتۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ

(Watu watatoka makaburini) ili Allah ailipe kila nafsi kwa yale iliyo yachuma. Hakika Allah ni Mwepesi wa kuhesabu



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 56

وَيَجۡعَلُونَ لِمَا لَا يَعۡلَمُونَ نَصِيبٗا مِّمَّا رَزَقۡنَٰهُمۡۗ تَٱللَّهِ لَتُسۡـَٔلُنَّ عَمَّا كُنتُمۡ تَفۡتَرُونَ

Na (katika ubaya wao) wana-tenga fungu katika vile tuli-vyowaruzuku kuvipa vile visivyojua chochote (Waungu wao). Naapa kwa haki ya Allah, bila shaka mtaulizwa kuhusu yote mliyokuwa mkiyatunga



Surah: ANNAHLI 

Ayah : 93

وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَجَعَلَكُمۡ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ وَلَٰكِن يُضِلُّ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَلَتُسۡـَٔلُنَّ عَمَّا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Na Allah angelitaka, kwa yakini angeliwafanyeni umma moja; lakini anayetaka (upotevu) anampoteza, na anayetaka (mwongozo) anamwongoza; na hakika mtaulizwa yale mliyokuwa mkiyafanya



Surah: AL-ISRAA 

Ayah : 13

وَكُلَّ إِنسَٰنٍ أَلۡزَمۡنَٰهُ طَـٰٓئِرَهُۥ فِي عُنُقِهِۦۖ وَنُخۡرِجُ لَهُۥ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ كِتَٰبٗا يَلۡقَىٰهُ مَنشُورًا

Na kila mtu tumemfungia a’mali yake shingoni mwake. Na Siku ya Kiyama tutamtolea kitabu atakacho kikuta kiwazi kimekunjuliwa



Surah: AL-ISRAA 

Ayah : 14

ٱقۡرَأۡ كِتَٰبَكَ كَفَىٰ بِنَفۡسِكَ ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكَ حَسِيبٗا

Ataambiwa: Soma kitabu chako! Nafsi yako inakutosha leo kukuhesabu



Surah: AL-ISRAA 

Ayah : 34

وَلَا تَقۡرَبُواْ مَالَ ٱلۡيَتِيمِ إِلَّا بِٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ أَشُدَّهُۥۚ وَأَوۡفُواْ بِٱلۡعَهۡدِۖ إِنَّ ٱلۡعَهۡدَ كَانَ مَسۡـُٔولٗا

Wala msiyakaribie mali ya yatima, isipokuwa kwa njia iliyo bora, mpaka afike utuuzimani. Na timizeni ahadi. Kwa hakika ahadi ni yenye kuulizwa



Surah: AL-ISRAA 

Ayah : 36

وَلَا تَقۡفُ مَا لَيۡسَ لَكَ بِهِۦ عِلۡمٌۚ إِنَّ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡبَصَرَ وَٱلۡفُؤَادَ كُلُّ أُوْلَـٰٓئِكَ كَانَ عَنۡهُ مَسۡـُٔولٗا

Wala usiyafuate usiyo na ujuzi nayo. Hakika masikio, na macho, na moyo - hivyo vyote vitasailiwa (vitaulizwa)



Surah: AL-ANBIYAA 

Ayah : 47

وَنَضَعُ ٱلۡمَوَٰزِينَ ٱلۡقِسۡطَ لِيَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ فَلَا تُظۡلَمُ نَفۡسٞ شَيۡـٔٗاۖ وَإِن كَانَ مِثۡقَالَ حَبَّةٖ مِّنۡ خَرۡدَلٍ أَتَيۡنَا بِهَاۗ وَكَفَىٰ بِنَا حَٰسِبِينَ

Nasi tutaweka mizani za uadilifu Siku ya Kiyama. Basi nafsi haitadhulumiwa kitu chochote. Hata ikiwa ni uzito wa chembe ya khardali tutaileta. Nasi tunatosha kuwa washika hesabu



Surah: ANNUUR 

Ayah : 23

إِنَّ ٱلَّذِينَ يَرۡمُونَ ٱلۡمُحۡصَنَٰتِ ٱلۡغَٰفِلَٰتِ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ لُعِنُواْ فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِ وَلَهُمۡ عَذَابٌ عَظِيمٞ

Hakika wanao wasingizia wanawake, wanao jihishimu, walio ghafilika (wasiofanya machafu), Waumini, wamelaaniwa duniani na Akhera, nao watapata adhabu kubwa



Surah: ANNUUR 

Ayah : 24

يَوۡمَ تَشۡهَدُ عَلَيۡهِمۡ أَلۡسِنَتُهُمۡ وَأَيۡدِيهِمۡ وَأَرۡجُلُهُم بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Siku ambayo zitawashuhudia ndimi zao na mikono yao na miguu yao kwa waliyokuwa wakiyatenda



Surah: ANNUUR 

Ayah : 25

يَوۡمَئِذٖ يُوَفِّيهِمُ ٱللَّهُ دِينَهُمُ ٱلۡحَقَّ وَيَعۡلَمُونَ أَنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلۡحَقُّ ٱلۡمُبِينُ

Siku hiyo Allah atawapa sawa sawa malipo yao ya haki, na watajua kwamba hakika Allah ndiye Haki Iliyo Wazi



Surah: ANNUUR 

Ayah : 39

وَٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَعۡمَٰلُهُمۡ كَسَرَابِۭ بِقِيعَةٖ يَحۡسَبُهُ ٱلظَّمۡـَٔانُ مَآءً حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءَهُۥ لَمۡ يَجِدۡهُ شَيۡـٔٗا وَوَجَدَ ٱللَّهَ عِندَهُۥ فَوَفَّىٰهُ حِسَابَهُۥۗ وَٱللَّهُ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ

Na walio kufuru vitendo vyao ni kama sarabi (mazigazi) uwandani. Mwenye kiu huyadhania ni maji. Hata akiyaendea hapati chochote. Na atamkuta Allah hapo naye amlipe hesabu yake sawa sawa. Na Allah ni Mwepesi wa kuhisabu



Surah: AL-ANKABUUT 

Ayah : 10

وَمِنَ ٱلنَّاسِ مَن يَقُولُ ءَامَنَّا بِٱللَّهِ فَإِذَآ أُوذِيَ فِي ٱللَّهِ جَعَلَ فِتۡنَةَ ٱلنَّاسِ كَعَذَابِ ٱللَّهِۖ وَلَئِن جَآءَ نَصۡرٞ مِّن رَّبِّكَ لَيَقُولُنَّ إِنَّا كُنَّا مَعَكُمۡۚ أَوَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِأَعۡلَمَ بِمَا فِي صُدُورِ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na katika watu wapo wanao sema: Tumemuamini Allah. Lakini wanapo pewa maudhi kwa ajili ya Allah, wanayafanya mateso ya watu kama ni adhabu ya Allah. Na inapo kuja nusura kutoka kwa Mola wako Mlezi husema: Hakika sisi tulikuwa pamoja nanyi. Kwani Allah hayajui yaliomo vifuani mwa walimwengu?



Surah: AL-ANKABUUT 

Ayah : 13

وَلَيَحۡمِلُنَّ أَثۡقَالَهُمۡ وَأَثۡقَالٗا مَّعَ أَثۡقَالِهِمۡۖ وَلَيُسۡـَٔلُنَّ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ عَمَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ

Na hapana shaka wataibeba mizigo yao na mizigo mingine pamoja na mizigo yao. Na kwa yakini wataulizwa Siku ya Kiyama juu ya waliyokuwa wakiyazua



Surah: SABAA 

Ayah : 25

قُل لَّا تُسۡـَٔلُونَ عَمَّآ أَجۡرَمۡنَا وَلَا نُسۡـَٔلُ عَمَّا تَعۡمَلُونَ

Sema: Nyinyi hamtaulizwa kwa makosa tuliyo yafanya, wala sisi hatutaulizwa kwa mnayo yatenda nyinyi



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 22

۞ٱحۡشُرُواْ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ وَأَزۡوَٰجَهُمۡ وَمَا كَانُواْ يَعۡبُدُونَ

Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 23

مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهۡدُوهُمۡ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلۡجَحِيمِ

Badala ya Allah. Waongozeni njia ya Jahannamu!



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 24

وَقِفُوهُمۡۖ إِنَّهُم مَّسۡـُٔولُونَ

Na wasimamisheni. Hakika hao wataulizwa:



Surah: GHAAFIR 

Ayah : 17

ٱلۡيَوۡمَ تُجۡزَىٰ كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡۚ لَا ظُلۡمَ ٱلۡيَوۡمَۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ

Leo kila nafsi italipwa kwa iliyo chuma. Hapana dhulma leo. Hakika Allah ni Mwepesi wa kuhesabu



Surah: AZZUKHRUF 

Ayah : 19

وَجَعَلُواْ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ ٱلَّذِينَ هُمۡ عِبَٰدُ ٱلرَّحۡمَٰنِ إِنَٰثًاۚ أَشَهِدُواْ خَلۡقَهُمۡۚ سَتُكۡتَبُ شَهَٰدَتُهُمۡ وَيُسۡـَٔلُونَ

Na wakawafanya Malaika, ambao ni waja wa Mwingi wa Rehema, kuwa ni wanawake! Kwani wameshuhudia kuumbwa kwao? Ushahidi wao utaandikwa na wao watahojiwa!



Surah: AZZUKHRUF 

Ayah : 44

وَإِنَّهُۥ لَذِكۡرٞ لَّكَ وَلِقَوۡمِكَۖ وَسَوۡفَ تُسۡـَٔلُونَ

Na hakika haya ni ukumbusho kwako na kwa watu wako. Na mtakuja ulizwa



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 19

فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَيَقُولُ هَآؤُمُ ٱقۡرَءُواْ كِتَٰبِيَهۡ

Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!



Surah: ALHAAQQA 

Ayah : 20

إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَٰقٍ حِسَابِيَهۡ

Hakika mimi niliyakinisha kuwa hakiki mimi ni mwenye kukutana na hesabu yangu!