Surah: ANNISAI 

Ayah : 163

۞إِنَّآ أَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡكَ كَمَآ أَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ نُوحٖ وَٱلنَّبِيِّـۧنَ مِنۢ بَعۡدِهِۦۚ وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡمَٰعِيلَ وَإِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ وَٱلۡأَسۡبَاطِ وَعِيسَىٰ وَأَيُّوبَ وَيُونُسَ وَهَٰرُونَ وَسُلَيۡمَٰنَۚ وَءَاتَيۡنَا دَاوُۥدَ زَبُورٗا

Hakika, sisi tumekufunulia (Wahyi) kama tulivyomfunulia (Wahyi) Nuhu na Manabii (wengine) baada yake. Na tumemfunulia (Wahyi) Ibrahimu na Ismail na Isihaka na Yakubu na kizazi (chake) na Issa na Ayubu na Yunus na Haruna na Sulaimani. Na tulimpa Daudi Zaburi



Surah: AL-AN’AAM 

Ayah : 86

وَإِسۡمَٰعِيلَ وَٱلۡيَسَعَ وَيُونُسَ وَلُوطٗاۚ وَكُلّٗا فَضَّلۡنَا عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na Ismaili na Alyasaa na Yunus na Lutwi. Na wote (hao) tumewafanya bora kuliko walimwengu (wengine wa zama zao)



Surah: YUNUS 

Ayah : 98

فَلَوۡلَا كَانَتۡ قَرۡيَةٌ ءَامَنَتۡ فَنَفَعَهَآ إِيمَٰنُهَآ إِلَّا قَوۡمَ يُونُسَ لَمَّآ ءَامَنُواْ كَشَفۡنَا عَنۡهُمۡ عَذَابَ ٱلۡخِزۡيِ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَمَتَّعۡنَٰهُمۡ إِلَىٰ حِينٖ

Basi laiti ungepatikana mji ulioamini na imani yake ikaunufaisha, isipokuwa tu watu wa Yunus. Walipoamini, tuliwaondolea adhabu ya fedheha katika maisha ya duniani na tukawaneemesha kwa muda[1]


1- - Aya hii inaeleza kuwa, hakuna kutubu wakati inapofika adhabu, isipokuwa tu hilo lilitokea kwa watu wa Nabii Yunus tu (Allah amshushie amani). Allah aliwaondolea adhabu baada ya kutubu na kufuata yale ambayo Mtume wao Yunus (Allah amshushie amani) aliwaambia.


Surah: AL-ANBIYAA 

Ayah : 87

وَذَا ٱلنُّونِ إِذ ذَّهَبَ مُغَٰضِبٗا فَظَنَّ أَن لَّن نَّقۡدِرَ عَلَيۡهِ فَنَادَىٰ فِي ٱلظُّلُمَٰتِ أَن لَّآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنتَ سُبۡحَٰنَكَ إِنِّي كُنتُ مِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na Dhun-Nun alipo ondoka hali ameghadhibika, na akadhani ya kwamba hatutakuwa na uwezo juu yake. Basi aliita katika giza: Hapana mungu isipo kuwa Wewe Subhanaka Uliye takasika. Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa wenye kudhulumu



Surah: AL-ANBIYAA 

Ayah : 88

فَٱسۡتَجَبۡنَا لَهُۥ وَنَجَّيۡنَٰهُ مِنَ ٱلۡغَمِّۚ وَكَذَٰلِكَ نُـۨجِي ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Basi tukamwitikia na tuka-muokoa kutokana na dhiki. Na hivyo ndivyo tunavyo waokoa Waumini



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 139

وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 140

إِذۡ أَبَقَ إِلَى ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ

Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 141

فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلۡمُدۡحَضِينَ

Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 142

فَٱلۡتَقَمَهُ ٱلۡحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٞ

Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 143

فَلَوۡلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلۡمُسَبِّحِينَ

Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Allah,



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 144

لَلَبِثَ فِي بَطۡنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ

Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 145

۞فَنَبَذۡنَٰهُ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٞ

Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 146

وَأَنۢبَتۡنَا عَلَيۡهِ شَجَرَةٗ مِّن يَقۡطِينٖ

Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung’unye



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 147

وَأَرۡسَلۡنَٰهُ إِلَىٰ مِاْئَةِ أَلۡفٍ أَوۡ يَزِيدُونَ

Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi



Surah: ASSWAAFFAAT 

Ayah : 148

فَـَٔامَنُواْ فَمَتَّعۡنَٰهُمۡ إِلَىٰ حِينٖ

Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 48

فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلۡحُوتِ إِذۡ نَادَىٰ وَهُوَ مَكۡظُومٞ

Basi subiri hukumu ya mola wako, wala usiwe kama sahibu wa nyangumi, alipomwita (Mola wake) na hali yeye alikuwa mwenye huzuni nyingi (Amebanwa na Dhiki)



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 49

لَّوۡلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعۡمَةٞ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ مَذۡمُومٞ

Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa



Surah: AL-QALAM 

Ayah : 50

فَٱجۡتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Lakini mola wake alimchagua na akamfanya kuwa ni miongoni mwa watu wema