Surah: AL-AHQAAF 

Ayah : 18

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ حَقَّ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقَوۡلُ فِيٓ أُمَمٖ قَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِهِم مِّنَ ٱلۡجِنِّ وَٱلۡإِنسِۖ إِنَّهُمۡ كَانُواْ خَٰسِرِينَ

Hao ndio ambao imehakikikishwa hukumu juu yao kama mataifa yaliyo kwisha pita kabla yao miongoni mwa majini na watu. Hakika hao wamekuwa ni wenye hasara



Surah: AL-AHQAAF 

Ayah : 29

وَإِذۡ صَرَفۡنَآ إِلَيۡكَ نَفَرٗا مِّنَ ٱلۡجِنِّ يَسۡتَمِعُونَ ٱلۡقُرۡءَانَ فَلَمَّا حَضَرُوهُ قَالُوٓاْ أَنصِتُواْۖ فَلَمَّا قُضِيَ وَلَّوۡاْ إِلَىٰ قَوۡمِهِم مُّنذِرِينَ

Na wakati tulipo waleta kundi la majini kuja kwako kusikiliza Qur’ani. Basi walipo ihudhuria walisema: Sikilizeni! Na ilipo kwisha somwa, walirudi kwa watu wao kwenda kuwaonya



Surah: AL-AHQAAF 

Ayah : 30

قَالُواْ يَٰقَوۡمَنَآ إِنَّا سَمِعۡنَا كِتَٰبًا أُنزِلَ مِنۢ بَعۡدِ مُوسَىٰ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ يَهۡدِيٓ إِلَى ٱلۡحَقِّ وَإِلَىٰ طَرِيقٖ مُّسۡتَقِيمٖ

Wakasema: Enyi watu wetu! Sisi tumesikia Kitabu kilicho teremshwa baada ya Mussa, kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake, na kinacho ongoza kwenye Haki na kwenye Njia Iliyo Nyooka



Surah: AL-AHQAAF 

Ayah : 31

يَٰقَوۡمَنَآ أَجِيبُواْ دَاعِيَ ٱللَّهِ وَءَامِنُواْ بِهِۦ يَغۡفِرۡ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمۡ وَيُجِرۡكُم مِّنۡ عَذَابٍ أَلِيمٖ

Enyi watu wetu! Muitikieni Mwenye kuitia kwa Allah, na muaminini, Allah atakusameheni, na atakukingeni na adhabu chungu



Surah: AL-AHQAAF 

Ayah : 32

وَمَن لَّا يُجِبۡ دَاعِيَ ٱللَّهِ فَلَيۡسَ بِمُعۡجِزٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَيۡسَ لَهُۥ مِن دُونِهِۦٓ أَوۡلِيَآءُۚ أُوْلَـٰٓئِكَ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ

Na wasio mwitikia Mwitaji wa Allah basi hao hawatashinda katika ardhi, wala hawatakuwa na walinzi mbele yake. Hao wamo katika upotovu ulio dhahiri



Surah: ADH-DHAARIYAAT 

Ayah : 56

وَمَا خَلَقۡتُ ٱلۡجِنَّ وَٱلۡإِنسَ إِلَّا لِيَعۡبُدُونِ

Na sikuwaumba majini na wanadamu ila kwa ajili ya kuniabudu



Surah: ARRAHMAAN 

Ayah : 15

وَخَلَقَ ٱلۡجَآنَّ مِن مَّارِجٖ مِّن نَّارٖ

Na Akaumba majini kutokana na ulimi wa moto



Surah: AL-MULK 

Ayah : 5

وَلَقَدۡ زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِمَصَٰبِيحَ وَجَعَلۡنَٰهَا رُجُومٗا لِّلشَّيَٰطِينِۖ وَأَعۡتَدۡنَا لَهُمۡ عَذَابَ ٱلسَّعِيرِ

Na kwa hakika, tumeipamba mbingu ya karibu kwa mataa (nyota), na tumeyafanya ili kuwapigia mashetani, na tumewaandalia (hao mashetani) adhabu ya Moto uwakao kwa nguvu



Surah: ALJINN 

Ayah : 1

قُلۡ أُوحِيَ إِلَيَّ أَنَّهُ ٱسۡتَمَعَ نَفَرٞ مِّنَ ٱلۡجِنِّ فَقَالُوٓاْ إِنَّا سَمِعۡنَا قُرۡءَانًا عَجَبٗا

Sema: Nimefunuliwa Wahyi kwamba, kundi miongoni mwa majini lilisikiliza (Qur’ani) likasema: Hakika sisi tumeisikia Qurani ya ajabu sana



Surah: ALJINN 

Ayah : 2

يَهۡدِيٓ إِلَى ٱلرُّشۡدِ فَـَٔامَنَّا بِهِۦۖ وَلَن نُّشۡرِكَ بِرَبِّنَآ أَحَدٗا

Inaongoza kwenye uongofu, kwa hivyo tumeiamini, na wala hatutamshirikisha yeyote kwa Mola wetu Mlezi



Surah: ALJINN 

Ayah : 3

وَأَنَّهُۥ تَعَٰلَىٰ جَدُّ رَبِّنَا مَا ٱتَّخَذَ صَٰحِبَةٗ وَلَا وَلَدٗا

Na kwa hakika utukufu wa Mola wetu umetukuka kabisa; Hakujifanyia Mke wala Mtoto (hana mke wala mwana)



Surah: ALJINN 

Ayah : 4

وَأَنَّهُۥ كَانَ يَقُولُ سَفِيهُنَا عَلَى ٱللَّهِ شَطَطٗا

Na kwa hakika hali ilivyo, wapumbavu miongoni mwetu walikuwa wakisema juu ya Allah uongo uliopindukia mipaka



Surah: ALJINN 

Ayah : 5

وَأَنَّا ظَنَنَّآ أَن لَّن تَقُولَ ٱلۡإِنسُ وَٱلۡجِنُّ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبٗا

Na kwamba sisi tulidhania wanadamu na majini hawatosema uongo juu ya Allaah, (hawatomzulia uongo Allah)



Surah: ALJINN 

Ayah : 6

وَأَنَّهُۥ كَانَ رِجَالٞ مِّنَ ٱلۡإِنسِ يَعُوذُونَ بِرِجَالٖ مِّنَ ٱلۡجِنِّ فَزَادُوهُمۡ رَهَقٗا

Na kwamba wanaume miongoni mwa wanadamu walikuwa wanajikinga kwa wanaume miongoni mwa majini, basi wakawazidishia wao madhambi, (uvukaji mipaka ya kuasi na khofu)



Surah: ALJINN 

Ayah : 7

وَأَنَّهُمۡ ظَنُّواْ كَمَا ظَنَنتُمۡ أَن لَّن يَبۡعَثَ ٱللَّهُ أَحَدٗا

Na kwa hakika wao walidhani, kama mlivyo dhani nyinyi, ya kuwa Allah hatamleta Mtume yeyote. (au Hatomfufua yeyote yule)



Surah: ALJINN 

Ayah : 8

وَأَنَّا لَمَسۡنَا ٱلسَّمَآءَ فَوَجَدۡنَٰهَا مُلِئَتۡ حَرَسٗا شَدِيدٗا وَشُهُبٗا

Nasi tulizigusa mbingu, (au tulitafuta kuzifikia mbingu) na tukaziona zimejaa walinzi wenye nguvu na vimondo



Surah: ALJINN 

Ayah : 9

وَأَنَّا كُنَّا نَقۡعُدُ مِنۡهَا مَقَٰعِدَ لِلسَّمۡعِۖ فَمَن يَسۡتَمِعِ ٱلۡأٓنَ يَجِدۡ لَهُۥ شِهَابٗا رَّصَدٗا

Na hakika sisi tulikuwa tukikaa humo katika baadhi ya makao ili kusikiliza; lakini anaetaka kusikiliza hivi sasa atakuta kimondo kinamvizia!



Surah: ALJINN 

Ayah : 10

وَأَنَّا لَا نَدۡرِيٓ أَشَرٌّ أُرِيدَ بِمَن فِي ٱلۡأَرۡضِ أَمۡ أَرَادَ بِهِمۡ رَبُّهُمۡ رَشَدٗا

Nasi hatujui kama wanatakiwa shari wale wanao kaa kwenye ardhi au Mola wao Mlezi anawatakia uongofu



Surah: ALJINN 

Ayah : 11

وَأَنَّا مِنَّا ٱلصَّـٰلِحُونَ وَمِنَّا دُونَ ذَٰلِكَۖ كُنَّا طَرَآئِقَ قِدَدٗا

Na hakika katika sisi wamo walio wema, na wengine wetu ni kinyume na hivyo. Tumekuwa njia mbali mbali



Surah: ALJINN 

Ayah : 12

وَأَنَّا ظَنَنَّآ أَن لَّن نُّعۡجِزَ ٱللَّهَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَن نُّعۡجِزَهُۥ هَرَبٗا

Nasi tulikuwa na yakini kwamba hatutoweza kumshinda Allah ardhini, na wala hatutoweza kumponyoka Allah kwa kukimbia



Surah: ALJINN 

Ayah : 13

وَأَنَّا لَمَّا سَمِعۡنَا ٱلۡهُدَىٰٓ ءَامَنَّا بِهِۦۖ فَمَن يُؤۡمِنۢ بِرَبِّهِۦ فَلَا يَخَافُ بَخۡسٗا وَلَا رَهَقٗا

Nasi tulipo usikia uongofu tuliuamini. Basi mwenye kumuamini Mola wake basi haogopi kupunjwa wala kudhulumiwa



Surah: ALJINN 

Ayah : 14

وَأَنَّا مِنَّا ٱلۡمُسۡلِمُونَ وَمِنَّا ٱلۡقَٰسِطُونَۖ فَمَنۡ أَسۡلَمَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ تَحَرَّوۡاْ رَشَدٗا

Na hakika sisi miongoni mwetu ni Waislamu, na miongoni mwetu wapo wakengeukaji; (wanao acha haki). Hivyo atakaye silimu, hao ndio waliofuata uongofu



Surah: ALJINN 

Ayah : 15

وَأَمَّا ٱلۡقَٰسِطُونَ فَكَانُواْ لِجَهَنَّمَ حَطَبٗا

Na ama wanaoacha haki, hao watakuwa kuni za Moto wa Jahannamu



Surah: ALJINN 

Ayah : 16

وَأَلَّوِ ٱسۡتَقَٰمُواْ عَلَى ٱلطَّرِيقَةِ لَأَسۡقَيۡنَٰهُم مَّآءً غَدَقٗا

(Allah Anasema): Kwamba lau wangelinyooka na wakasimama sawasawa kwenye njia, bila shaka Tungeli wanywesha maji kwa wingi



Surah: ALJINN 

Ayah : 17

لِّنَفۡتِنَهُمۡ فِيهِۚ وَمَن يُعۡرِضۡ عَن ذِكۡرِ رَبِّهِۦ يَسۡلُكۡهُ عَذَابٗا صَعَدٗا

Ili tuwatie katika majaribio kwayo. Na anayepuuza Ukumbusho wa Mola wake, Atamsukuma kwenye adhabu ngumu