Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 137

وَأَوۡرَثۡنَا ٱلۡقَوۡمَ ٱلَّذِينَ كَانُواْ يُسۡتَضۡعَفُونَ مَشَٰرِقَ ٱلۡأَرۡضِ وَمَغَٰرِبَهَا ٱلَّتِي بَٰرَكۡنَا فِيهَاۖ وَتَمَّتۡ كَلِمَتُ رَبِّكَ ٱلۡحُسۡنَىٰ عَلَىٰ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ بِمَا صَبَرُواْۖ وَدَمَّرۡنَا مَا كَانَ يَصۡنَعُ فِرۡعَوۡنُ وَقَوۡمُهُۥ وَمَا كَانُواْ يَعۡرِشُونَ

Na tuliwarithisha watu waliokuwa wananyanyaswa mashariki ya ardhi (Shamu) na magharibi yake ambayo tumeibariki. Na neno zuri la Mola wako limetimia kwa Wana wa Israili kwa sababu walivumilia na tuliyaangamiza yote aliyotengeneza Firauni na watu wake, na (majumba ya kifahari) waliyokuwa wakiyajenga



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 138

وَجَٰوَزۡنَا بِبَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ ٱلۡبَحۡرَ فَأَتَوۡاْ عَلَىٰ قَوۡمٖ يَعۡكُفُونَ عَلَىٰٓ أَصۡنَامٖ لَّهُمۡۚ قَالُواْ يَٰمُوسَى ٱجۡعَل لَّنَآ إِلَٰهٗا كَمَا لَهُمۡ ءَالِهَةٞۚ قَالَ إِنَّكُمۡ قَوۡمٞ تَجۡهَلُونَ

Na tuliwavusha Wana wa Israili baharini, wakafika kwa watu wanaoabudu masanamu yao. (Wana wa Israili) Wakasema (kumwambia Mtume Musa): Ewe Musa, na sisi tufanyie Mungu kama hawa walivyo na Miungu. (Musa) Akasema: Hakika, nyinyi ni watu wajinga!



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 139

إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ مُتَبَّرٞ مَّا هُمۡ فِيهِ وَبَٰطِلٞ مَّا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Hakika, hawa kimeangamizwa ambacho wanakifanya na ni batili yote ambayo waliyokuwa wakiyatenda



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 140

قَالَ أَغَيۡرَ ٱللَّهِ أَبۡغِيكُمۡ إِلَٰهٗا وَهُوَ فَضَّلَكُمۡ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

(Musa) Alisema: Hivi nikutakieni Mungu mwingine badala ya Allah na ilhali yeye ndiye aliyekufanyeni bora kuliko walimwengu wote (wa wakati wenu)?



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 141

وَإِذۡ أَنجَيۡنَٰكُم مِّنۡ ءَالِ فِرۡعَوۡنَ يَسُومُونَكُمۡ سُوٓءَ ٱلۡعَذَابِ يُقَتِّلُونَ أَبۡنَآءَكُمۡ وَيَسۡتَحۡيُونَ نِسَآءَكُمۡۚ وَفِي ذَٰلِكُم بَلَآءٞ مِّن رَّبِّكُمۡ عَظِيمٞ

Na (kumbukeni) tulipokuokoeni kutoka kwa watu wa Firauni wakikupeni adhabu mbaya sana; wanawaua vibaya watoto wenu wanaume na kuwaacha hai watoto wenu wanawake. Na katika hayo kwenu kuna mitihani mikubwa kutoka kwa Mola wenu Mlezi



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 148

وَٱتَّخَذَ قَوۡمُ مُوسَىٰ مِنۢ بَعۡدِهِۦ مِنۡ حُلِيِّهِمۡ عِجۡلٗا جَسَدٗا لَّهُۥ خُوَارٌۚ أَلَمۡ يَرَوۡاْ أَنَّهُۥ لَا يُكَلِّمُهُمۡ وَلَا يَهۡدِيهِمۡ سَبِيلًاۘ ٱتَّخَذُوهُ وَكَانُواْ ظَٰلِمِينَ

Na watu Musa baada ya kuondoka kwake, walitengeneza kutokana na mapambo yao umbo la ndama lenye sauti (ya mlio wa ng’ombe). Hivi hawakuona kuwa (ndama yule) hawasemeshi na hawaongozi njia yoyote? Walimchukua (walimfanya kama Mungu) na walikuwa madhalimu



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 149

وَلَمَّا سُقِطَ فِيٓ أَيۡدِيهِمۡ وَرَأَوۡاْ أَنَّهُمۡ قَدۡ ضَلُّواْ قَالُواْ لَئِن لَّمۡ يَرۡحَمۡنَا رَبُّنَا وَيَغۡفِرۡ لَنَا لَنَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ

Na walipoangukia mikononi mwao (walipojuta) na kuona kuwa wameshapotea walisema: Ikiwa Mola wetu Mlezi hatatuhurumia na kutusamehe, bila shaka tutakuwa miongoni mwa wenye kupata hasara



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 150

وَلَمَّا رَجَعَ مُوسَىٰٓ إِلَىٰ قَوۡمِهِۦ غَضۡبَٰنَ أَسِفٗا قَالَ بِئۡسَمَا خَلَفۡتُمُونِي مِنۢ بَعۡدِيٓۖ أَعَجِلۡتُمۡ أَمۡرَ رَبِّكُمۡۖ وَأَلۡقَى ٱلۡأَلۡوَاحَ وَأَخَذَ بِرَأۡسِ أَخِيهِ يَجُرُّهُۥٓ إِلَيۡهِۚ قَالَ ٱبۡنَ أُمَّ إِنَّ ٱلۡقَوۡمَ ٱسۡتَضۡعَفُونِي وَكَادُواْ يَقۡتُلُونَنِي فَلَا تُشۡمِتۡ بِيَ ٱلۡأَعۡدَآءَ وَلَا تَجۡعَلۡنِي مَعَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na Musa aliporudi kwa watu wake akiwa amekasirika na kuhuzunika alisema: Ubaya ulioje wa mliyoyafanya baada kuondoka kwangu! Hivi mmeharakia amri ya Mola wenu Mlezi? Na alizitupa mbao (za Taurati) na akakamata kichwa cha ndugu yake (Haruna) akimvutia kwake na kumwambia: Ewe mtoto wa mama yangu, hakika hawa watu wamenidharau na walikaribia kuniua. Basi usiwafurahishe maadui kupitia kwangu na usiniweke pamoja na watu madhalimu



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 151

قَالَ رَبِّ ٱغۡفِرۡ لِي وَلِأَخِي وَأَدۡخِلۡنَا فِي رَحۡمَتِكَۖ وَأَنتَ أَرۡحَمُ ٱلرَّـٰحِمِينَ

(Musa) Akasema: Ewe Mola wangu, nisamehe mimi na ndugu yangu na tuingize katika rehema zako, na wewe ni Rahimu zaidi ya warahimu (wote)



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 152

إِنَّ ٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ ٱلۡعِجۡلَ سَيَنَالُهُمۡ غَضَبٞ مِّن رَّبِّهِمۡ وَذِلَّةٞ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۚ وَكَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُفۡتَرِينَ

Hakika, wale waliomfanya ndama (Mungu) itawapata adhabu ya Mola wao Mlezi na madhila katika maisha ya duniani. Na kama hivyo ndivyo tunavyowalipa wazushi



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 153

وَٱلَّذِينَ عَمِلُواْ ٱلسَّيِّـَٔاتِ ثُمَّ تَابُواْ مِنۢ بَعۡدِهَا وَءَامَنُوٓاْ إِنَّ رَبَّكَ مِنۢ بَعۡدِهَا لَغَفُورٞ رَّحِيمٞ

Na wale waliotenda maovu, kisha wakatubu baada yake na wakaamini, hakika Mola wako baada ya hayo ni Msamehevu sana, Rahimu sana



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 159

وَمِن قَوۡمِ مُوسَىٰٓ أُمَّةٞ يَهۡدُونَ بِٱلۡحَقِّ وَبِهِۦ يَعۡدِلُونَ

Na katika watu wa Musa kuna kundi linalo ongoza kwa haki, na kwa haki hiyo wanafanya uadilifu



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 160

وَقَطَّعۡنَٰهُمُ ٱثۡنَتَيۡ عَشۡرَةَ أَسۡبَاطًا أُمَمٗاۚ وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ إِذِ ٱسۡتَسۡقَىٰهُ قَوۡمُهُۥٓ أَنِ ٱضۡرِب بِّعَصَاكَ ٱلۡحَجَرَۖ فَٱنۢبَجَسَتۡ مِنۡهُ ٱثۡنَتَا عَشۡرَةَ عَيۡنٗاۖ قَدۡ عَلِمَ كُلُّ أُنَاسٖ مَّشۡرَبَهُمۡۚ وَظَلَّلۡنَا عَلَيۡهِمُ ٱلۡغَمَٰمَ وَأَنزَلۡنَا عَلَيۡهِمُ ٱلۡمَنَّ وَٱلسَّلۡوَىٰۖ كُلُواْ مِن طَيِّبَٰتِ مَا رَزَقۡنَٰكُمۡۚ وَمَا ظَلَمُونَا وَلَٰكِن كَانُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ يَظۡلِمُونَ

Na tuliwakata kata (tuliwagawa makundi makundi) katika koo na mataifa kumi na mbili. Na tulimpa Musa Wahyi wakati watu wake walipomuomba maji (kwamba): Piga jiwe kwa fimbo yako, basi zikapasuka kutoka jiwe lile chemchem kumi na mbili. Kila watu walijua mahali pao pa (kupata huduma ya maji ya) kunywa. Na tuliwafunika kivuli cha mawingu na tukawateremshia Mana na Salwa (na tukawaambia): Kuleni katika vizuri vya vile tulivyokuruzukuni. Na hawakutudhulumu, na lakini walikuwa wanajidhulumu wao wenyewe



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 161

وَإِذۡ قِيلَ لَهُمُ ٱسۡكُنُواْ هَٰذِهِ ٱلۡقَرۡيَةَ وَكُلُواْ مِنۡهَا حَيۡثُ شِئۡتُمۡ وَقُولُواْ حِطَّةٞ وَٱدۡخُلُواْ ٱلۡبَابَ سُجَّدٗا نَّغۡفِرۡ لَكُمۡ خَطِيٓـَٰٔتِكُمۡۚ سَنَزِيدُ ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Na (kumbuka) walipoambiwa: Kaeni katika mji huu na kuleni humo mpendavyo na semeni: “(Ewe Allah) Tufutie dhambi”, na ingieni katika lango (la mji huo) mkiwa wenye kusujudu (mkiwa wanyenyekevu). (Mkifanya hivyo), Tutakusameheni makosa yenu. Tutawazidishia wafanyao mazuri



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 162

فَبَدَّلَ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ مِنۡهُمۡ قَوۡلًا غَيۡرَ ٱلَّذِي قِيلَ لَهُمۡ فَأَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ رِجۡزٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ بِمَا كَانُواْ يَظۡلِمُونَ

Basi wale waliodhulumu miongoni mwao walibadili kauli isiyokuwa ile waliyoambiwa. Basi tukawapelekea adhabu kutoka mbinguni kwa sababu ya walivyokuwa wanadhulumu (nafsi zao)



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 163

وَسۡـَٔلۡهُمۡ عَنِ ٱلۡقَرۡيَةِ ٱلَّتِي كَانَتۡ حَاضِرَةَ ٱلۡبَحۡرِ إِذۡ يَعۡدُونَ فِي ٱلسَّبۡتِ إِذۡ تَأۡتِيهِمۡ حِيتَانُهُمۡ يَوۡمَ سَبۡتِهِمۡ شُرَّعٗا وَيَوۡمَ لَا يَسۡبِتُونَ لَا تَأۡتِيهِمۡۚ كَذَٰلِكَ نَبۡلُوهُم بِمَا كَانُواْ يَفۡسُقُونَ

Na waulize kuhusu mji uliokuwepo kando ya bahari walipokiuka (heshima ya siku ya) Jumamosi wakati samaki wao walipokuwa wanawajia nje nje siku yao ya mapumziko, na siku wasiyopumzika (samaki) hawawajii. Kama hivyo tunawajaribu (tunawapa mtihani) kwa vile walivyokuwa wakifanya uasi



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 164

وَإِذۡ قَالَتۡ أُمَّةٞ مِّنۡهُمۡ لِمَ تَعِظُونَ قَوۡمًا ٱللَّهُ مُهۡلِكُهُمۡ أَوۡ مُعَذِّبُهُمۡ عَذَابٗا شَدِيدٗاۖ قَالُواْ مَعۡذِرَةً إِلَىٰ رَبِّكُمۡ وَلَعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ

Na (kumbuka) wakati kundi miongoni mwao liliposema (kwamba): Kwa nini mnawapa mawaidha watu ambao Allah ni Mwenye kuwaangamiza au kuwaadhibu adhabu kali? Walisema: (Tunawapa mawaidha) Ili uwe udhuru kwa Mola wenu na huwenda nao wakawa wachaMungu



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 165

فَلَمَّا نَسُواْ مَا ذُكِّرُواْ بِهِۦٓ أَنجَيۡنَا ٱلَّذِينَ يَنۡهَوۡنَ عَنِ ٱلسُّوٓءِ وَأَخَذۡنَا ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ بِعَذَابِۭ بَـِٔيسِۭ بِمَا كَانُواْ يَفۡسُقُونَ

Basi walipoyasahau yale waliyokumbushwa tuliwaokoa waliokuwa wanakataza maovu na tuliwachukulia hatua ambao wamedhulumu (nafsi zao kwa kuasi) kwa (kuwapa) adhabu mbaya kwa walivyokuwa wanafanya uasi



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 166

فَلَمَّا عَتَوۡاْ عَن مَّا نُهُواْ عَنۡهُ قُلۡنَا لَهُمۡ كُونُواْ قِرَدَةً خَٰسِـِٔينَ

Basi walipoyapuuza yale waliyokatazwa tuliwaambia: Kuweni manyani dhalili



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 167

وَإِذۡ تَأَذَّنَ رَبُّكَ لَيَبۡعَثَنَّ عَلَيۡهِمۡ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ مَن يَسُومُهُمۡ سُوٓءَ ٱلۡعَذَابِۗ إِنَّ رَبَّكَ لَسَرِيعُ ٱلۡعِقَابِ وَإِنَّهُۥ لَغَفُورٞ رَّحِيمٞ

Na (kumbuka) wakati Mola wako alipotangaza kuwa: Kwa hakika kabisa, atawapelekea watakaowaonjesha adhabu mbaya kabisa mpaka Siku ya Kiyama. Hakika kabisa, Mola wako ni Mwepesi mno wa kuadhibu na pia yeye ni Mwingi wa kusamehe, Rahimu sana



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 168

وَقَطَّعۡنَٰهُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ أُمَمٗاۖ مِّنۡهُمُ ٱلصَّـٰلِحُونَ وَمِنۡهُمۡ دُونَ ذَٰلِكَۖ وَبَلَوۡنَٰهُم بِٱلۡحَسَنَٰتِ وَٱلسَّيِّـَٔاتِ لَعَلَّهُمۡ يَرۡجِعُونَ

Na tuliwakata kata mataifa mbali mbali duniani (tuliwafanya wafarakane makundi makundi). Miongoni mwao wapo walio wema na miongoni mwao wapo kinyume na hivyo. Na tuliwajaribu kwa (mambo) mazuri na mabaya ili wapate kurejea (kwa Mola wao)



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 169

فَخَلَفَ مِنۢ بَعۡدِهِمۡ خَلۡفٞ وَرِثُواْ ٱلۡكِتَٰبَ يَأۡخُذُونَ عَرَضَ هَٰذَا ٱلۡأَدۡنَىٰ وَيَقُولُونَ سَيُغۡفَرُ لَنَا وَإِن يَأۡتِهِمۡ عَرَضٞ مِّثۡلُهُۥ يَأۡخُذُوهُۚ أَلَمۡ يُؤۡخَذۡ عَلَيۡهِم مِّيثَٰقُ ٱلۡكِتَٰبِ أَن لَّا يَقُولُواْ عَلَى ٱللَّهِ إِلَّا ٱلۡحَقَّ وَدَرَسُواْ مَا فِيهِۗ وَٱلدَّارُ ٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لِّلَّذِينَ يَتَّقُونَۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Basi kikafuatia baada yao kizazi kibaya kilichorithi kitabu (Taurati); wanashika anasa za haya maisha duni sana (ya duniani), na huku wanasema: Tutasamehewa (tu, acha tule maisha). Na ikiwajia tena anasa kama hiyo wanaichukua. Hivi haikuchukuliwa kwao ahadi nzito ya kitabu kwamba, wasimsemee Allah isipokuwa haki tu na ilhali wamesoma yaliyomo kwenye kitabu hicho? Na nyumba ya Akhera ni bora kwa wanaomcha Allah. Hivi hamtumii akili?



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 170

وَٱلَّذِينَ يُمَسِّكُونَ بِٱلۡكِتَٰبِ وَأَقَامُواْ ٱلصَّلَوٰةَ إِنَّا لَا نُضِيعُ أَجۡرَ ٱلۡمُصۡلِحِينَ

Na ambao wanakishika vilivyo kitabu (bila ya kukipuuza au kukifanyia mzaha) na wakadumisha Swala, hakika sisi hatupotezi ujira wa watengenezao (mambo ya kumridhisha Allah)



Surah: AL-AARAAF 

Ayah : 171

۞وَإِذۡ نَتَقۡنَا ٱلۡجَبَلَ فَوۡقَهُمۡ كَأَنَّهُۥ ظُلَّةٞ وَظَنُّوٓاْ أَنَّهُۥ وَاقِعُۢ بِهِمۡ خُذُواْ مَآ ءَاتَيۡنَٰكُم بِقُوَّةٖ وَٱذۡكُرُواْ مَا فِيهِ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ

Na (kumbuka) wakati tulipou-nyanyua mlima juu yao ukawa kama kiwingu na wakadhani kuwa utawaangukia (na kuwaambia): Chukueni kwa nguvu yale tuliyo-kupeni, na yakumbukeni yaliomo ndani yake ili muwe wacha Mungu



Surah: YUNUS 

Ayah : 83

فَمَآ ءَامَنَ لِمُوسَىٰٓ إِلَّا ذُرِّيَّةٞ مِّن قَوۡمِهِۦ عَلَىٰ خَوۡفٖ مِّن فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِمۡ أَن يَفۡتِنَهُمۡۚ وَإِنَّ فِرۡعَوۡنَ لَعَالٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَإِنَّهُۥ لَمِنَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Basi hakuna aliyemuamini Musa (pamoja na dalili na hoja zote alizowaonesha) isipokuwa vijana wachache katika kaumu yake huku wakiwa na hofu (ya kumuogopa) Firauni na mamwinyi wao wasiwatese. Na hakika kabisa, Firauni alikuwa mwenye kujikweza ardhini, na kwa yakini kabisa yeye (Firauni) alikuwa miongoni mwa waliokiuka mipaka (katika kufanya uovu)



Surah: YUNUS 

Ayah : 84

وَقَالَ مُوسَىٰ يَٰقَوۡمِ إِن كُنتُمۡ ءَامَنتُم بِٱللَّهِ فَعَلَيۡهِ تَوَكَّلُوٓاْ إِن كُنتُم مُّسۡلِمِينَ

Na Musa alisema: Enyi watu wangu, kama kweli nyinyi mmemuamini Allah, basi mtegemeeni yeye tu, kama nyinyi mkiwa Waislamu (kweli)



Surah: YUNUS 

Ayah : 85

فَقَالُواْ عَلَى ٱللَّهِ تَوَكَّلۡنَا رَبَّنَا لَا تَجۡعَلۡنَا فِتۡنَةٗ لِّلۡقَوۡمِ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Basi wakasema: “Allah tu tunamtegemea. Ewe Mola wetu Mlezi, usitufanye mtihani kwa watu madhalimu”



Surah: YUNUS 

Ayah : 86

وَنَجِّنَا بِرَحۡمَتِكَ مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na utuokoe kwa rehema zako dhidi ya watu makafiri



Surah: YUNUS 

Ayah : 87

وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰ وَأَخِيهِ أَن تَبَوَّءَا لِقَوۡمِكُمَا بِمِصۡرَ بُيُوتٗا وَٱجۡعَلُواْ بُيُوتَكُمۡ قِبۡلَةٗ وَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَۗ وَبَشِّرِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Na tulimpa Wahyi Musa na ndugu yake (Haruna) ya kuwa: Wawekeeni makazi (wajengeeni nyumba) watu wenu (katika mji wa) Misri na zifanyeni nyumba zenu ziwe na mahala pa ibada na simamisheni Swala na wape bishara Waumini



Surah: YUNUS 

Ayah : 88

وَقَالَ مُوسَىٰ رَبَّنَآ إِنَّكَ ءَاتَيۡتَ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَأَهُۥ زِينَةٗ وَأَمۡوَٰلٗا فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا رَبَّنَا لِيُضِلُّواْ عَن سَبِيلِكَۖ رَبَّنَا ٱطۡمِسۡ عَلَىٰٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ وَٱشۡدُدۡ عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ فَلَا يُؤۡمِنُواْ حَتَّىٰ يَرَوُاْ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَلِيمَ

Na Musa alisema: “(Ewe) Mola wetu Mlezi, bila shaka umempa Firauni na mamwinyi wake mapambo na mali nyingi katika maisha ya duniani (na hawakukushukuru). (Ewe) Mola wetu Mlezi, (umewapa hivyo vyote na wanavitumia) ili kuwapoteza (watu) wasiifuate njia yako. (Ewe) Mola wetu Mlezi, zifute Mali zao na mioyo yao ifanye kuwa migumu ili wasiamini hadi waione adhabu iumizayo mno”