Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 100

أَوَكُلَّمَا عَٰهَدُواْ عَهۡدٗا نَّبَذَهُۥ فَرِيقٞ مِّنۡهُمۚ بَلۡ أَكۡثَرُهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Hivi ni kwanini kila watoapo ahadi, kuna kundi miongoni mwao linaivunja ahadi hiyo! Lakini (ukweli ni kwamba) wengi wao hawaamini



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 101

وَلَمَّا جَآءَهُمۡ رَسُولٞ مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِ مُصَدِّقٞ لِّمَا مَعَهُمۡ نَبَذَ فَرِيقٞ مِّنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ كِتَٰبَ ٱللَّهِ وَرَآءَ ظُهُورِهِمۡ كَأَنَّهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Na alipowafikia Mtume kutoka kwa Allah mwenye kusadikisha yale waliyo nayo, kundi miongoni mwa wale waliopewa Kitabu walikitupa Kitabu cha Allah nyuma ya migongo yao kama kwamba hawajui



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 102

وَٱتَّبَعُواْ مَا تَتۡلُواْ ٱلشَّيَٰطِينُ عَلَىٰ مُلۡكِ سُلَيۡمَٰنَۖ وَمَا كَفَرَ سُلَيۡمَٰنُ وَلَٰكِنَّ ٱلشَّيَٰطِينَ كَفَرُواْ يُعَلِّمُونَ ٱلنَّاسَ ٱلسِّحۡرَ وَمَآ أُنزِلَ عَلَى ٱلۡمَلَكَيۡنِ بِبَابِلَ هَٰرُوتَ وَمَٰرُوتَۚ وَمَا يُعَلِّمَانِ مِنۡ أَحَدٍ حَتَّىٰ يَقُولَآ إِنَّمَا نَحۡنُ فِتۡنَةٞ فَلَا تَكۡفُرۡۖ فَيَتَعَلَّمُونَ مِنۡهُمَا مَا يُفَرِّقُونَ بِهِۦ بَيۡنَ ٱلۡمَرۡءِ وَزَوۡجِهِۦۚ وَمَا هُم بِضَآرِّينَ بِهِۦ مِنۡ أَحَدٍ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۚ وَيَتَعَلَّمُونَ مَا يَضُرُّهُمۡ وَلَا يَنفَعُهُمۡۚ وَلَقَدۡ عَلِمُواْ لَمَنِ ٱشۡتَرَىٰهُ مَا لَهُۥ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ مِنۡ خَلَٰقٖۚ وَلَبِئۡسَ مَا شَرَوۡاْ بِهِۦٓ أَنفُسَهُمۡۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ

Na wamefuata yale yanayoso-mwa na Mashetani katika (wakati wa) ufalme wa Suleimani. Na Suleimani hakukufuru, lakini Mashetani ndio waliokufuru; (kwa sababu) wanawafundisha watu uchawi na yaliyoteremshwa kwa Malaika wawili Haruta na Maruta katika mji wa Babil. Na wala hawamfundishi yeyote mpaka wamwambie: Hakika sisi ni mtihani, basi usikufuru. Basi wakajifunza kwao yale yawezayo kumfarakanisha mtu na mkewe. Na wala wao hawana uwezo wa kumdhuru yeyote kwa hayo ila kwa idhini ya Allah tu. Na wanajifunza yale yanayowadhuru na wala hayawanufaishi. Na kwa yakini wamejua kwamba aliyechagua haya hatakuwa na fungu lolote Akhera. Na nikibaya mnokilewalichozichagulianafsizao laiti wangekuwa wanajua



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 103

وَلَوۡ أَنَّهُمۡ ءَامَنُواْ وَٱتَّقَوۡاْ لَمَثُوبَةٞ مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِ خَيۡرٞۚ لَّوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ

Na lau wangeamini na kumcha Allah, bila ya shaka malipo yatokayo kwa Allah yangekuwa bora laiti wangelijua



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 122

يَٰبَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ ٱذۡكُرُواْ نِعۡمَتِيَ ٱلَّتِيٓ أَنۡعَمۡتُ عَلَيۡكُمۡ وَأَنِّي فَضَّلۡتُكُمۡ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

Enyi Wana wa Israili, kum-bukeni neema zangu ambazo nime-kuneemesheni, na nimekufanyeni bora zaidi kuliko walimwengu (wa wakati wenu)



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 123

وَٱتَّقُواْ يَوۡمٗا لَّا تَجۡزِي نَفۡسٌ عَن نَّفۡسٖ شَيۡـٔٗا وَلَا يُقۡبَلُ مِنۡهَا عَدۡلٞ وَلَا تَنفَعُهَا شَفَٰعَةٞ وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ

Na iogopeni siku ambayo nafsi haitaifaa nafsi nyingine (kwa) chochote, na haitakubaliwa nafsi hiyo fidia wala kuombewa msamaha na kamwe hawatanusuriwa



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 246

أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلۡمَلَإِ مِنۢ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ مِنۢ بَعۡدِ مُوسَىٰٓ إِذۡ قَالُواْ لِنَبِيّٖ لَّهُمُ ٱبۡعَثۡ لَنَا مَلِكٗا نُّقَٰتِلۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِۖ قَالَ هَلۡ عَسَيۡتُمۡ إِن كُتِبَ عَلَيۡكُمُ ٱلۡقِتَالُ أَلَّا تُقَٰتِلُواْۖ قَالُواْ وَمَا لَنَآ أَلَّا نُقَٰتِلَ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَقَدۡ أُخۡرِجۡنَا مِن دِيَٰرِنَا وَأَبۡنَآئِنَاۖ فَلَمَّا كُتِبَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقِتَالُ تَوَلَّوۡاْ إِلَّا قَلِيلٗا مِّنۡهُمۡۚ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلظَّـٰلِمِينَ

Je, hukupata habari za mabwana wakubwa wa Wana wa Israili baada ya Musa? Walipomwambia Nabii wao: Tuteulie Mfalme ili tukapigane katika njia ya Allah. Akawaambia: Je, mtakuwa tayari kupigana iwapo mtafaradhishiwa kupigana? Wakasema: Na kwanini tusipigane katika njia ya Allah na ilhali tumetolewa katika makazi yetu na wanetu? Basi walipofaradhishiwa kupigana, waligeuka ila wachache tu miongoni mwao, na Allah anawajua mno madhalimu



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 247

وَقَالَ لَهُمۡ نَبِيُّهُمۡ إِنَّ ٱللَّهَ قَدۡ بَعَثَ لَكُمۡ طَالُوتَ مَلِكٗاۚ قَالُوٓاْ أَنَّىٰ يَكُونُ لَهُ ٱلۡمُلۡكُ عَلَيۡنَا وَنَحۡنُ أَحَقُّ بِٱلۡمُلۡكِ مِنۡهُ وَلَمۡ يُؤۡتَ سَعَةٗ مِّنَ ٱلۡمَالِۚ قَالَ إِنَّ ٱللَّهَ ٱصۡطَفَىٰهُ عَلَيۡكُمۡ وَزَادَهُۥ بَسۡطَةٗ فِي ٱلۡعِلۡمِ وَٱلۡجِسۡمِۖ وَٱللَّهُ يُؤۡتِي مُلۡكَهُۥ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ وَٰسِعٌ عَلِيمٞ

Na Nabii wao akawaambia: Hakika Allah ameshakuteulieni Twaluti kuwa Mfalme. Wakasema: Anawezaje kuwa Mfalme wetu, na ilhali sisi tuna haki zaidi ya Ufalme kuliko yeye, na wala hakupewa wasaa wa mali? Akasema: Hakika Allah ameshakuteulieni na amemzidishia wasaa wa elimu na mwili. Na Allah humpa Ufalme wake amtakaye na Allah ni Mwenye wasaa, Mjuzi mno



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 248

وَقَالَ لَهُمۡ نَبِيُّهُمۡ إِنَّ ءَايَةَ مُلۡكِهِۦٓ أَن يَأۡتِيَكُمُ ٱلتَّابُوتُ فِيهِ سَكِينَةٞ مِّن رَّبِّكُمۡ وَبَقِيَّةٞ مِّمَّا تَرَكَ ءَالُ مُوسَىٰ وَءَالُ هَٰرُونَ تَحۡمِلُهُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لَّكُمۡ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

Na Nabii wao akawaambia: “Hakika alama ya ufalme wake nikukuleteeni sanduku ambalo ndani yake kuna kitulizacho nyoyo zenu kitokacho kwa Mola wenu na mabaki ya yale waliyoyaacha watu wa Musa na watu wa Haruni linalobebwa na Malaika. Bila shaka katika hayo mna dalili kwenu ikiwa ninyi ni waumini



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 249

فَلَمَّا فَصَلَ طَالُوتُ بِٱلۡجُنُودِ قَالَ إِنَّ ٱللَّهَ مُبۡتَلِيكُم بِنَهَرٖ فَمَن شَرِبَ مِنۡهُ فَلَيۡسَ مِنِّي وَمَن لَّمۡ يَطۡعَمۡهُ فَإِنَّهُۥ مِنِّيٓ إِلَّا مَنِ ٱغۡتَرَفَ غُرۡفَةَۢ بِيَدِهِۦۚ فَشَرِبُواْ مِنۡهُ إِلَّا قَلِيلٗا مِّنۡهُمۡۚ فَلَمَّا جَاوَزَهُۥ هُوَ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَعَهُۥ قَالُواْ لَا طَاقَةَ لَنَا ٱلۡيَوۡمَ بِجَالُوتَ وَجُنُودِهِۦۚ قَالَ ٱلَّذِينَ يَظُنُّونَ أَنَّهُم مُّلَٰقُواْ ٱللَّهِ كَم مِّن فِئَةٖ قَلِيلَةٍ غَلَبَتۡ فِئَةٗ كَثِيرَةَۢ بِإِذۡنِ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ مَعَ ٱلصَّـٰبِرِينَ

Basi Twaluti alipoondoka na majeshi alisema: Hakika Allah atakufanyieni mtihani kwa mto, basi atakayekunywa humo si pamoja nami, na asiye yanywa bila shaka yupo pamoja nami, ila atakayeteka kiasi cha kiganja cha mkono wake. Basi walikunywa humo isipokuwa wachache miongoni mwao. Basi alipovuka yeye na walioamini pamoja naye, walisema: Leo hatumuwezi Jaluti na majeshi yake. Wakasema: wale ambao wana yakini ya kukutana na Allah: Makundi mangapi machache yameyashinda makundi mengi kwa idhini ya Allah? Na Allah yupo pamoja na wafanyao subira



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 250

وَلَمَّا بَرَزُواْ لِجَالُوتَ وَجُنُودِهِۦ قَالُواْ رَبَّنَآ أَفۡرِغۡ عَلَيۡنَا صَبۡرٗا وَثَبِّتۡ أَقۡدَامَنَا وَٱنصُرۡنَا عَلَى ٱلۡقَوۡمِ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na walipotoka (hadharani) kupambana Na Jaluti Na majeshi yake, walisema: Mola wetu! Tumi-minie subira, na uiimarishe miguu yetu na utupe ushindi dhidi ya watu makafiri



Surah: AL-BAQARAH 

Ayah : 251

فَهَزَمُوهُم بِإِذۡنِ ٱللَّهِ وَقَتَلَ دَاوُۥدُ جَالُوتَ وَءَاتَىٰهُ ٱللَّهُ ٱلۡمُلۡكَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَعَلَّمَهُۥ مِمَّا يَشَآءُۗ وَلَوۡلَا دَفۡعُ ٱللَّهِ ٱلنَّاسَ بَعۡضَهُم بِبَعۡضٖ لَّفَسَدَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ ذُو فَضۡلٍ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

Basi waliwashinda kwa idhini ya Allah na Daudi akamuua Jaluti, na Allah akampa (Daudi) ufalme na utume na akamfundisha aliyoyataka. Na kama Allah asingewakinga watu baadhi yao kwa wengine, bila shaka ardhi ingeliharibika, lakini Allah ni Mwenye hisani kubwa mno kwa walimwengu



Surah: AL-IMRAN 

Ayah : 93

۞كُلُّ ٱلطَّعَامِ كَانَ حِلّٗا لِّبَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ إِلَّا مَا حَرَّمَ إِسۡرَـٰٓءِيلُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ مِن قَبۡلِ أَن تُنَزَّلَ ٱلتَّوۡرَىٰةُۚ قُلۡ فَأۡتُواْ بِٱلتَّوۡرَىٰةِ فَٱتۡلُوهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Aina zote za vyakula zilikuwa halali kwa Wana wa Israili, isipokuwa tu vile (vyakula) ambavyo Israili (Yakubu) alijiharamishia mwenyewe kabla ya kuteremshwa kwa Taurati. Sema: Basi ileteni Taurati muisome ikiwa nyinyi ni wa kweli



Surah: AL-IMRAN 

Ayah : 94

فَمَنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ مِنۢ بَعۡدِ ذَٰلِكَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ

Basi watakaomzulia Allah uongo baada ya haya basi hao ndio madhalimu hasa



Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 12

۞وَلَقَدۡ أَخَذَ ٱللَّهُ مِيثَٰقَ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ وَبَعَثۡنَا مِنۡهُمُ ٱثۡنَيۡ عَشَرَ نَقِيبٗاۖ وَقَالَ ٱللَّهُ إِنِّي مَعَكُمۡۖ لَئِنۡ أَقَمۡتُمُ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتَيۡتُمُ ٱلزَّكَوٰةَ وَءَامَنتُم بِرُسُلِي وَعَزَّرۡتُمُوهُمۡ وَأَقۡرَضۡتُمُ ٱللَّهَ قَرۡضًا حَسَنٗا لَّأُكَفِّرَنَّ عَنكُمۡ سَيِّـَٔاتِكُمۡ وَلَأُدۡخِلَنَّكُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ فَمَن كَفَرَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ مِنكُمۡ فَقَدۡ ضَلَّ سَوَآءَ ٱلسَّبِيلِ

Na kwa yakini kabisa, Allah alifunga ahadi na Wana wa Israil, na tukatuma miongoni mwao viongozi kumi na mbili (ili wawafundishe utekelezaji wa ahadi hiyo ya Allah) na Allah akasema: Kwa yakini mimi niko pamoja nanyi. Kwa yakini kabisa, kama mkisimamisha Swala na mkitoa Zaka na mkiwaamini Mitume wangu na mkiwapa nguvu (mkiwaunga mkono) na mkimkopesha Allah mkopo mzuri, bila shaka yoyote nitakufutieni maovu yenu na nitakuingizeni katika Pepo zipitazo mito mbele yake. Basi atakayekufuru miongoni mwenu baada ya (makubaliano) hayo, bila shaka amepotea njia ya sawa



Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 13

فَبِمَا نَقۡضِهِم مِّيثَٰقَهُمۡ لَعَنَّـٰهُمۡ وَجَعَلۡنَا قُلُوبَهُمۡ قَٰسِيَةٗۖ يُحَرِّفُونَ ٱلۡكَلِمَ عَن مَّوَاضِعِهِۦ وَنَسُواْ حَظّٗا مِّمَّا ذُكِّرُواْ بِهِۦۚ وَلَا تَزَالُ تَطَّلِعُ عَلَىٰ خَآئِنَةٖ مِّنۡهُمۡ إِلَّا قَلِيلٗا مِّنۡهُمۡۖ فَٱعۡفُ عَنۡهُمۡ وَٱصۡفَحۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Basi kwa sababu ya kuvunja kwao makubaliano yao, tuliwalaani na kuzifanya ngumu nyoyo zao; wanayapotosha maneno ya (Allah)[1] katika mahali pake na wameacha sehemu (kubwa) ya yale waliyokumbushwa. Na bado unaendelea kupata habari za khiyana yao isipokuwa wachache miongoni mwao. Basi wasamehe na wapuuze. Hakika, Allah anawapenda wafanyao mazuri


1- - Yaliyomo katika Torati na Injili.


Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 20

وَإِذۡ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوۡمِهِۦ يَٰقَوۡمِ ٱذۡكُرُواْ نِعۡمَةَ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡ إِذۡ جَعَلَ فِيكُمۡ أَنۢبِيَآءَ وَجَعَلَكُم مُّلُوكٗا وَءَاتَىٰكُم مَّا لَمۡ يُؤۡتِ أَحَدٗا مِّنَ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na (kumbukeni) Musa alipowaambia watu wake: “Enyi watu wangu, kumbukeni neema za Allah kwenu; alipofanya kwenu Manabii na akakufanyeni wafalme na akakupeni (mambo) ambayo hakumpa yeyote katika walimwengu (wote wa zama zenu)



Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 21

يَٰقَوۡمِ ٱدۡخُلُواْ ٱلۡأَرۡضَ ٱلۡمُقَدَّسَةَ ٱلَّتِي كَتَبَ ٱللَّهُ لَكُمۡ وَلَا تَرۡتَدُّواْ عَلَىٰٓ أَدۡبَارِكُمۡ فَتَنقَلِبُواْ خَٰسِرِينَ

“Enyi watu wangu, Ingieni katika Ardhi Takatifu (Baytulmaqdis) ambayo Allah amekuandikieni na msirudi nyuma (kupigana na Wakanani) mtakuwa wenye kula hasara (mkifanya hivyo)



Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 22

قَالُواْ يَٰمُوسَىٰٓ إِنَّ فِيهَا قَوۡمٗا جَبَّارِينَ وَإِنَّا لَن نَّدۡخُلَهَا حَتَّىٰ يَخۡرُجُواْ مِنۡهَا فَإِن يَخۡرُجُواْ مِنۡهَا فَإِنَّا دَٰخِلُونَ

Wakasema: Ewe Musa, hakika humo kuna watu majabari[1], na sisi hatutaingia humo mpaka watoke humo (na watukabidhi mji kwa amani). Wakitoka humo, basi sisi bila ya shaka tutaingia


1- - Watu wenye miili mikubwa, wababe na madhalimu.


Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 23

قَالَ رَجُلَانِ مِنَ ٱلَّذِينَ يَخَافُونَ أَنۡعَمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمَا ٱدۡخُلُواْ عَلَيۡهِمُ ٱلۡبَابَ فَإِذَا دَخَلۡتُمُوهُ فَإِنَّكُمۡ غَٰلِبُونَۚ وَعَلَى ٱللَّهِ فَتَوَكَّلُوٓاْ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

Watu wawili miongoni mwa wale waogopao (kuhalifu amri za Allah na Mtume wake) ambao Allah amewaneemesha walisema: Wavamieni kupitia kwenye huo mlango; maana mtakapowavamia (kupitia hapo mlangoni), kwa yakini nyinyi mtashinda. Na mtegemeeni Allah tu ikiwa nyinyi ni waumini



Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 24

قَالُواْ يَٰمُوسَىٰٓ إِنَّا لَن نَّدۡخُلَهَآ أَبَدٗا مَّا دَامُواْ فِيهَا فَٱذۡهَبۡ أَنتَ وَرَبُّكَ فَقَٰتِلَآ إِنَّا هَٰهُنَا قَٰعِدُونَ

Wakasema: “Ewe Musa, sisi hatutaingia humo kamwe madamu wao bado wamo humo. Basi nenda wewe na Mola wako mkapigane, sisi ni wenye kuketi hapa (hatuendi kokote).”



Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 25

قَالَ رَبِّ إِنِّي لَآ أَمۡلِكُ إِلَّا نَفۡسِي وَأَخِيۖ فَٱفۡرُقۡ بَيۡنَنَا وَبَيۡنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلۡفَٰسِقِينَ

(Musa) Akasema: (Ewe) Mola wangu, hakika mimi similiki isipokuwa nafsi yangu na ndugu yangu; basi tutenganishe na hawa watu mafasiki (waovu)



Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 26

قَالَ فَإِنَّهَا مُحَرَّمَةٌ عَلَيۡهِمۡۛ أَرۡبَعِينَ سَنَةٗۛ يَتِيهُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِۚ فَلَا تَأۡسَ عَلَى ٱلۡقَوۡمِ ٱلۡفَٰسِقِينَ

(Allah) Akasema: “Basi wame-haramishiwa (ardhi) hiyo kwa muda wa miaka arobaini; wakitangatanga ardhini. Basi usiwasikitikie watu mafasiki (waovu)



Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 32

مِنۡ أَجۡلِ ذَٰلِكَ كَتَبۡنَا عَلَىٰ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ أَنَّهُۥ مَن قَتَلَ نَفۡسَۢا بِغَيۡرِ نَفۡسٍ أَوۡ فَسَادٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَكَأَنَّمَا قَتَلَ ٱلنَّاسَ جَمِيعٗا وَمَنۡ أَحۡيَاهَا فَكَأَنَّمَآ أَحۡيَا ٱلنَّاسَ جَمِيعٗاۚ وَلَقَدۡ جَآءَتۡهُمۡ رُسُلُنَا بِٱلۡبَيِّنَٰتِ ثُمَّ إِنَّ كَثِيرٗا مِّنۡهُم بَعۡدَ ذَٰلِكَ فِي ٱلۡأَرۡضِ لَمُسۡرِفُونَ

Kwa sababu ya hayo[1], tume-waandikia (tumewafaradhishia) Wana wa Israil ya kwamba, aliyeua nafsi (ya mtu) bila ya (yeye kuua) nafsi au kufanya uovu katika nchi, basi ni kama ameua watu wote. Na mwenye kuihuisha (kuiokoa nafsi isife) ni kama ameokoa watu wote. Na hakika waliwajia Mitume wetu na hoja za wazi, kisha wengi miongoni mwao baada ya hayo wakawa wenye kufanya yaliyovuka mipaka katika ardhi


1- - Kosa la mauaji yaliyofanywa na mmoja wa watoto wa Mtume Adamu.


Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 70

لَقَدۡ أَخَذۡنَا مِيثَٰقَ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ وَأَرۡسَلۡنَآ إِلَيۡهِمۡ رُسُلٗاۖ كُلَّمَا جَآءَهُمۡ رَسُولُۢ بِمَا لَا تَهۡوَىٰٓ أَنفُسُهُمۡ فَرِيقٗا كَذَّبُواْ وَفَرِيقٗا يَقۡتُلُونَ

Kwa hakika kabisa, tulichukua ahadi ya Wana wa Israili[1] na tuliwapelekea Mitume. Kila alipowajia Mtume na yale ambayo nafsi zao haziyapendi wengine waliwapinga na wengine waliwauwa


1- - Ya kumuamini Allah na Mtume wake.


Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 71

وَحَسِبُوٓاْ أَلَّا تَكُونَ فِتۡنَةٞ فَعَمُواْ وَصَمُّواْ ثُمَّ تَابَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡ ثُمَّ عَمُواْ وَصَمُّواْ كَثِيرٞ مِّنۡهُمۡۚ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِمَا يَعۡمَلُونَ

Na walidhani kuwa hakutakuwa na mtihani (adhabu yoyote); kwasababu hiyo wakawa vipofu (wa kutoiona haki) na viziwi (wa kutoisikia haki). Kisha Allah akapokea Toba yao. Kisha wengi katika wao wakawa tena vipofu na viziwi. Na Allah ni Mwenye kuyaona hayo wayatendayo



Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 78

لُعِنَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۢ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ عَلَىٰ لِسَانِ دَاوُۥدَ وَعِيسَى ٱبۡنِ مَرۡيَمَۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَواْ وَّكَانُواْ يَعۡتَدُونَ

Wamelaaniwa waliokufuru miongoni mwa Wana wa Israili kupitia ulimi wa Daudi na Issa Mwana wa Mariamu. Hayo ni kwasababu waliasi na walikuwa wanachupa mipaka



Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 79

كَانُواْ لَا يَتَنَاهَوۡنَ عَن مُّنكَرٖ فَعَلُوهُۚ لَبِئۡسَ مَا كَانُواْ يَفۡعَلُونَ

Walikuwa hawakatazani maovu waliyokuwa wakiyafanya. Kwa yakini kabisa, ni maovu makubwa sana hayo waliyokuwa wanayafanya!



Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 80

تَرَىٰ كَثِيرٗا مِّنۡهُمۡ يَتَوَلَّوۡنَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ لَبِئۡسَ مَا قَدَّمَتۡ لَهُمۡ أَنفُسُهُمۡ أَن سَخِطَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡ وَفِي ٱلۡعَذَابِ هُمۡ خَٰلِدُونَ

Utawaona wengi wao wana-wafanya makafiri marafiki (wao) wa ndani. Kwa yakini kabisa, ni maovu sana hayo yaliyotangulia kufanywa na nafsi zao hadi Allah amewakasirikia, na watadumu milele katika adhabu



Surah: AL-MAIDA 

Ayah : 81

وَلَوۡ كَانُواْ يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلنَّبِيِّ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡهِ مَا ٱتَّخَذُوهُمۡ أَوۡلِيَآءَ وَلَٰكِنَّ كَثِيرٗا مِّنۡهُمۡ فَٰسِقُونَ

Na lau wangelimwamini Allah, na (huyu) Nabii, na yaliyoteremshwa kwake, wasingewafanya hao (makafiri) wapenzi wa ndani, lakini wengi katika wao ni waovu