Surata: NUUH 

O versículo : 1

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوۡمِهِۦٓ أَنۡ أَنذِرۡ قَوۡمَكَ مِن قَبۡلِ أَن يَأۡتِيَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Hakika, Sisi Tulimtuma Nuhu kwa watu wake (tukamwambia) kwamba: Waonye watu wako kabla haijawafikia adhabu iumizayo sana



Surata: NUUH 

O versículo : 2

قَالَ يَٰقَوۡمِ إِنِّي لَكُمۡ نَذِيرٞ مُّبِينٌ

(Nuhu) Akasema: Enyi watu wangu, hakika mimi kwenu ni muonyaji wa dhahiri (wa wazi) kwenu



Surata: NUUH 

O versículo : 3

أَنِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ وَٱتَّقُوهُ وَأَطِيعُونِ

(Nakuonyeni) Kwamba muabuduni Allah na mcheni (muogopeni) na mnitii



Surata: NUUH 

O versículo : 4

يَغۡفِرۡ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمۡ وَيُؤَخِّرۡكُمۡ إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمًّىۚ إِنَّ أَجَلَ ٱللَّهِ إِذَا جَآءَ لَا يُؤَخَّرُۚ لَوۡ كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Atakusameheni madhambi yenu, na atakuahirisheni mpaka muda uliowekwa. Hakika muda wa Allah ukifika haucheleweshwi, lau kama mngekuwa mnajua



Surata: NUUH 

O versículo : 5

قَالَ رَبِّ إِنِّي دَعَوۡتُ قَوۡمِي لَيۡلٗا وَنَهَارٗا

(Nuhu) Akasema: Mola wangu! Hakika mimi nimewalingania watu wangu usiku na mchana



Surata: NUUH 

O versículo : 6

فَلَمۡ يَزِدۡهُمۡ دُعَآءِيٓ إِلَّا فِرَارٗا

Lakini haikuwazidishia wito wangu isipokuwa kukimbia



Surata: NUUH 

O versículo : 7

وَإِنِّي كُلَّمَا دَعَوۡتُهُمۡ لِتَغۡفِرَ لَهُمۡ جَعَلُوٓاْ أَصَٰبِعَهُمۡ فِيٓ ءَاذَانِهِمۡ وَٱسۡتَغۡشَوۡاْ ثِيَابَهُمۡ وَأَصَرُّواْ وَٱسۡتَكۡبَرُواْ ٱسۡتِكۡبَارٗا

Na hakika Mimi kila nilipowaita ili Uwasamehe; huweka vidole vyao masikioni mwao na wakajifunika nguo zao na wakashikilia (kukanusha) wakafanya kiburi kikubwa



Surata: NUUH 

O versículo : 8

ثُمَّ إِنِّي دَعَوۡتُهُمۡ جِهَارٗا

Kisha hakika mimi niliwalingania kwa waziwazi



Surata: NUUH 

O versículo : 9

ثُمَّ إِنِّيٓ أَعۡلَنتُ لَهُمۡ وَأَسۡرَرۡتُ لَهُمۡ إِسۡرَارٗا

Kisha nikawatangazia kwa sauti, halafu tena nikasema nao kwa siri



Surata: NUUH 

O versículo : 10

فَقُلۡتُ ٱسۡتَغۡفِرُواْ رَبَّكُمۡ إِنَّهُۥ كَانَ غَفَّارٗا

Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe



Surata: NUUH 

O versículo : 11

يُرۡسِلِ ٱلسَّمَآءَ عَلَيۡكُم مِّدۡرَارٗا

Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo (Yenye kuendelea)



Surata: NUUH 

O versículo : 12

وَيُمۡدِدۡكُم بِأَمۡوَٰلٖ وَبَنِينَ وَيَجۡعَل لَّكُمۡ جَنَّـٰتٖ وَيَجۡعَل لَّكُمۡ أَنۡهَٰرٗا

Na Atakuongezeeni mali na wana, na Atakupeni mabustani na Atakufanyieni mito



Surata: NUUH 

O versículo : 13

مَّا لَكُمۡ لَا تَرۡجُونَ لِلَّهِ وَقَارٗا

Mna nini hamweki heshima ya Allah?



Surata: NUUH 

O versículo : 14

وَقَدۡ خَلَقَكُمۡ أَطۡوَارًا

Na hali Amekuumbeni hatua baada ya hatua?



Surata: NUUH 

O versículo : 15

أَلَمۡ تَرَوۡاْ كَيۡفَ خَلَقَ ٱللَّهُ سَبۡعَ سَمَٰوَٰتٖ طِبَاقٗا

Kwani hamwoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyo ziumba mbingu saba kwa matabaka?



Surata: NUUH 

O versículo : 16

وَجَعَلَ ٱلۡقَمَرَ فِيهِنَّ نُورٗا وَجَعَلَ ٱلشَّمۡسَ سِرَاجٗا

Na Akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na Akalifanya jua ni taa yenye mwanga mkali?



Surata: NUUH 

O versículo : 17

وَٱللَّهُ أَنۢبَتَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ نَبَاتٗا

Na Allah amekuotesheni (Amekuanzisheni vizuri katika udongo) wa ardhi kama mimea



Surata: NUUH 

O versículo : 18

ثُمَّ يُعِيدُكُمۡ فِيهَا وَيُخۡرِجُكُمۡ إِخۡرَاجٗا

Kisha Atakurudisheni humo na Atakutoeni tena mtoke (kuwa hai)



Surata: NUUH 

O versículo : 19

وَٱللَّهُ جَعَلَ لَكُمُ ٱلۡأَرۡضَ بِسَاطٗا

Na Allah Amekufanyieni ardhi kuwa (kama) busati



Surata: NUUH 

O versículo : 20

لِّتَسۡلُكُواْ مِنۡهَا سُبُلٗا فِجَاجٗا

Ili mtembee humo katika njia zilizo pana



Surata: NUUH 

O versículo : 21

قَالَ نُوحٞ رَّبِّ إِنَّهُمۡ عَصَوۡنِي وَٱتَّبَعُواْ مَن لَّمۡ يَزِدۡهُ مَالُهُۥ وَوَلَدُهُۥٓ إِلَّا خَسَارٗا

Nuhu akasema: Mola wangu! Hakika hao wameniasi, na wamemfuata yule ambaye mali yake na wanawe hawakumzidishia ila khasara tu



Surata: NUUH 

O versículo : 22

وَمَكَرُواْ مَكۡرٗا كُبَّارٗا

Na wakapanga vitimbi vikubwa



Surata: NUUH 

O versículo : 23

وَقَالُواْ لَا تَذَرُنَّ ءَالِهَتَكُمۡ وَلَا تَذَرُنَّ وَدّٗا وَلَا سُوَاعٗا وَلَا يَغُوثَ وَيَعُوقَ وَنَسۡرٗا

Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda wala Suwaa’ wala Yaghutha, wala Yau’qa, wala Nasra.[1]


1- - Wadda, Su’waa’a, Yaghuwtha, Ya’uwqa, Nasraa: ni majina ya masanamu waliyokuwa wakiyaabudu watu wa Nabii Nuhu, haya masanamu yalikuwa makubwa na matukufu zaidi kwao, na kwaajili hiyo yalihusishwa kwa kutajwa hapa, na asili yake ni kama vile alivyosema U’rwah bin Zubeyri-


Surata: NUUH 

O versículo : 24

وَقَدۡ أَضَلُّواْ كَثِيرٗاۖ وَلَا تَزِدِ ٱلظَّـٰلِمِينَ إِلَّا ضَلَٰلٗا

Na hao walikwisha wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea



Surata: NUUH 

O versículo : 25

مِّمَّا خَطِيٓـَٰٔتِهِمۡ أُغۡرِقُواْ فَأُدۡخِلُواْ نَارٗا فَلَمۡ يَجِدُواْ لَهُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ أَنصَارٗا

Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa Motoni, wala hawakuwapata wa kuwanusuru badala ya Allah



Surata: NUUH 

O versículo : 26

وَقَالَ نُوحٞ رَّبِّ لَا تَذَرۡ عَلَى ٱلۡأَرۡضِ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ دَيَّارًا

Na Nuh’u akasema: Mola wangu Mlezi! Usimwache juu ya ardhi mkaazi wake yeyote katika makafiri!



Surata: NUUH 

O versículo : 27

إِنَّكَ إِن تَذَرۡهُمۡ يُضِلُّواْ عِبَادَكَ وَلَا يَلِدُوٓاْ إِلَّا فَاجِرٗا كَفَّارٗا

Hakika Wewe Ukiwaacha, watawapoteza waja Wako, na wala hawatozaa isipokuwa mtendaji dhambi, kafiri mkanushaji mno



Surata: NUUH 

O versículo : 28

رَّبِّ ٱغۡفِرۡ لِي وَلِوَٰلِدَيَّ وَلِمَن دَخَلَ بَيۡتِيَ مُؤۡمِنٗا وَلِلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِۖ وَلَا تَزِدِ ٱلظَّـٰلِمِينَ إِلَّا تَبَارَۢا

Eee Mola wangu! Nisamehe Mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wote wanawake. Na wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea, (na kuteketea kabisa)